< John 3 >

1 Now there was one of the Pharisees named Nicodemus, a ruler among the Jews.
Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi lililotawala.
2 This man came to Jesus by night, and said to him. "Rabbi, we know that you are a teacher sent from God; for no man can do these signs which you are continually doing, unless God is with him."
Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”
3 "In very truth I tell you," answered Jesus, "that unless a man is born from above, he cannot see the kingdom of God."
Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”
4 "How can a man be born when he is old?" Nicodemus replied; "Can he enter a second time into his mother’s womb, and be born?"
Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”
5 "I tell you solemnly," Jesus answered, "that unless a man is born of water and the Spirit, he cannot enter the kingdom of God.
Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho.
6 What is born of the flesh is flesh; and what is born of the Spirit is spirit.
Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho.
7 Marvel not at my telling you, ‘You must all be born again from above.’
Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’
8 The wind blows where it wills, and you hear its voice, but you do not know where it comes from or where it is going. So it is with every one who has been born of the Spirit."
Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”
9 "How can this be?" said Nicodemus in reply.
Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
10 "Are you the Teacher of Israel, and yet you do not understand these things?" said Jesus.
Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya?
11 "Most solemnly I tell you we are speaking of what we know, and it is about that of which we were eyewitnesses that we give testimony. Yet all of you reject our testimony.
Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu.
12 If I have told you earthly things and yet none of you believe me, how will you believe if I tell you concerning heavenly things?
Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni?
13 There is no one gone up to heaven, except the One who came down from heaven - the Son of man himself.
Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.
14 And just as Moses lifted up the serpent in the wilderness, so must the Son of man be lifted up,
Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu.
15 in order that every one who believes in him may have eternal life. (aiōnios g166)
Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
16 "For God so loved the world that he gave his only begotten Son, that whoever trusts in him should not perish, but have eternal life. (aiōnios g166)
“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
17 For God did not send his Son into the world to condemn the world, but that the world through him might be saved.
Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa.
18 He who trusts in him is not condemned, but he who does not trust has already been condemned, because he has not put his trust in the name of the only begotten Son of God.
Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
19 And this is the condemnation, that Light is come into the world, and men loved darkness rather than light, because their deeds were evil.
Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu.
20 For every one who practises wrong hates light, and does not come to the light, lest his actions be exposed;
Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe.
21 but he who does what is true, comes to the light, in order that his actions may be shown to have been wrought in God."
Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”
22 After this Jesus and his disciples went into the countryside of Judea, and there he was staying with them and baptizing.
Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza.
23 John also was baptizing in Aenon, near Salim, because there were many streams there, and people kept coming to receive baptism.
Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa.
24 (For John had not yet been thrown into prison.)
(Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani).
25 Then some of John’s disciples got into a controversy with a Jew in regard to purification; so they came to John and said to him.
Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso.
26 "Rabbi, see! The man who was with you on the other side of Jordan, and to whom you yourself have borne testimony, is now baptizing, and everybody is coming to him."
Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”
27 In reply John said. "A man cannot obtain anything unless it has been granted to him from heaven.
Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni.
28 You yourselves are my witnesses that I said, ‘I am not the Christ, but have been sent before him.’
Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo, ila nimetumwa nimtangulie.’
29 He who has the bride is the bridegroom, but the friend of the bridegroom, who stands and hears him, rejoices greatly because of the bridegroom’s voice. So then this joy of mine has now complete fulfilment.
Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika.
30 He must increase, but I must decrease.
Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”
31 "He that comes from above is above all; but one who is of the earth, of the earth he is, and of the earth he speaks. He who comes from heaven is above all.
“Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote.
32 He bears testimony to what he has heard and seen, yet no one receives his testimony.
Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake.
33 Whoever does receive it has set his seal that God is true.
Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli.
34 For he whom God sent utters the words of God; for God does not give the Spirit sparingly.
Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo.
35 the Father loves the Son and has committed everything into his hands.
Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake.
36 Whoever believes in the Son has eternal life, but he who disobeys the Son shall not see life, but he who disobeys the Son shall not see life, but the wrath of God abides upon him." (aiōnios g166)
Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.” (aiōnios g166)

< John 3 >