< Colossians 1 >

1 Paul, an apostle of Jesus Christ, by the will of God, and Timothy our brother,
Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu:
2 to the holy and believing brothers in Christ who are in Colosse. Grace to you, and peace, from God our Father.
Kwa ndugu watakatifu na waaminifu katika Kristo, waishio Kolosai: Neema na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu ziwe nanyi.
3 Whenever I pray for you I am continually thanking God, the Father of our Lord Jesus Christ
Siku zote tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, tunapowaombea ninyi,
4 (since I heard of your faith in Christ Jesus and your love to all the saints)
kwa sababu tumesikia kuhusu imani yenu katika Kristo Yesu, na upendo wenu mlio nao kwa watakatifu wote:
5 because of the hope laid up for you in heaven. Long ago you heard of this hope in the message which came to you of the truth of the gospel.
imani na upendo ule utokao katika tumaini mlilowekewa akiba mbinguni, na ambalo mmesikia habari zake katika neno la kweli, yaani, ile Injili
6 And just as it is spreading through the whole world, bearing fruit and increasing, so also is it among you, from the day in which you heard it, and came truly to know the grace of God,
iliyowafikia ninyi. Duniani kote Injili hii inazaa matunda na kuenea kama ilivyokuwa kwenu tangu siku ile mlipoisikia na kuielewa neema ya Mungu katika kweli yote.
7 as you learned it from Epaphras, our dearly loved fellow slave. He is a faithful minister of Jesus Christ in your behalf,
Mlijifunza habari zake kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu mpendwa, yeye aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yenu,
8 and it is he who has told me of your love for me in the spirit.
ambaye pia ametuambia kuhusu upendo wenu katika Roho.
9 For this reason from the day I heard of it I have never ceased to pray for you, asking God to fill you with the knowledge of his will with every kind of wisdom and spiritual insight;
Kwa sababu hii, tangu siku ile tuliposikia habari zenu, hatujakoma kuomba kwa ajili yenu na kumsihi Mungu awajaze ninyi maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote ya kiroho na ufahamu.
10 that you may walk worthy of the Lord in every kind of pleasing; that you may be fruitful in every kind of good work, and may increase in the knowledge of God;
Nasi tunaomba haya ili mpate kuishi maisha yanayostahili mbele za Bwana, na mpate kumpendeza kwa kila namna: mkizaa matunda kwa kila kazi njema, mkikua katika kumjua Mungu,
11 that you may be strengthened in every kind of strength by the might of his glory for every kind of patience and fortitude with good cheer.
mkiwa mmetiwa nguvu kwa uwezo wote kwa kadiri ya nguvu yake yenye utukufu, ili mpate kuwa na wingi wa saburi na uvumilivu. Nanyi kwa furaha
12 I ask that you may give thanks to the Father who has made us fit to receive our share of the heritage of the saints in the light.
mkimshukuru Baba, ambaye amewastahilisha kushiriki katika urithi wa watakatifu katika ufalme wa nuru.
13 For he has delivered us out of the dominion of the darkness, and transplanted us into the kingdom of his dear Son,
Kwa maana ametuokoa kutoka ufalme wa giza na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mpendwa,
14 in whom we have redemption, the forgiveness of our sins.
ambaye katika yeye tunao ukombozi, yaani msamaha wa dhambi.
15 He is a visible image of the invisible God, the firstborn of all creation;
Yeye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 for in him was the universe created, things in heaven and on earth, the seen and the unseen, thrones, or dominions, or principalities, or powers; by him and for him all have been created;
Kwake yeye vitu vyote vilivyoko mbinguni na juu ya nchi viliumbwa: vitu vinavyoonekana na visivyoonekana, viwe ni viti vya enzi au falme, au wenye mamlaka au watawala; vitu vyote viliumbwa na yeye na kwa ajili yake.
17 and HE IS before all, and in him all things subsist.
Yeye alikuwepo kabla ya vitu vyote, na katika yeye vitu vyote vinashikamana pamoja.
18 He is the head of his Body, the Church. He is the beginning, the firstborn from the dead, in order that in all things he may become preeminent.
Yeye ndiye kichwa cha mwili, yaani kanisa, naye ndiye mwanzo na mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, ili yeye awe mkuu katika vitu vyote.
19 For in him all the divine fulness chose to dwell;
Kwa kuwa ilimpendeza Mungu kwamba utimilifu wake wote ukae ndani yake,
20 and by him it chose to reconcile all things alike on earth or in heaven to himself; making peace by him, through the blood of his cross.
na kwa njia yake aweze kuvipatanisha vitu vyote na yeye mwenyewe, viwe ni vitu vilivyo duniani au vilivyo mbinguni, kwa kufanya amani kwa damu yake, iliyomwagika msalabani.
21 And you, alienated as you once were, hostile at heart in your evil deeds,
Hapo kwanza mlikuwa mmetengana na Mungu, na mlikuwa adui zake katika nia zenu kwa sababu ya mienendo yenu mibaya.
22 he has now in his human body reconciled to God by his death, in order that he may bring you into his presence, holy and unblemished and irreproachable.
Lakini sasa Mungu amewapatanisha ninyi kwa njia ya mwili wa Kristo kupitia mauti, ili awalete mbele zake mkiwa watakatifu, bila dosari wala lawama,
23 And this he will do if, indeed, you continue in the faith, firmly founded and stedfast, and never moved away from the hope of the gospel which you heard, and which has been proclaimed to every creature under heaven, that gospel of which I, Paul, was made a minister.
ikiwa mnaendelea katika imani yenu mkiwa imara na thabiti, pasipo kuliacha tumaini lililoahidiwa katika Injili. Hii ndiyo ile Injili mliyoisikia, ambayo imehubiriwa kwa kila kiumbe chini ya mbingu, na ambayo mimi Paulo nimekuwa mtumwa wake.
24 I am now rejoicing in my sufferings on your behalf; and I am filling up in my own body what is yet lacking of the sufferings of Christ in behalf of the church, his Body.
Sasa nafurahia kule kuteseka kwangu kwa ajili yenu, na katika mwili wangu ninatimiliza yale yaliyopungua katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kanisa.
25 It is of this I was made a minister, according to the stewardship entrusted to me by God for you, fully to declare God’s message;
Mimi nimekuwa mtumishi wa kanisa kwa wajibu alionipa Mungu ili kuwaletea ninyi Neno la Mungu kwa ukamilifu:
26 that secret truth, which, although hidden from ages and generations of old, has now been made manifest to his saints. (aiōn g165)
Hii ni siri iliyokuwa imefichika tangu zamani na kwa vizazi vingi, lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu. (aiōn g165)
27 To them God willed to make known among the Gentiles how glorious are the riches of that secret truth, which is "Christ in you, the hope of glory."
Kwao, Mungu amechagua kujulisha miongoni mwa watu wa Mataifa utukufu wa utajiri wa siri hii, ambayo ni Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu.
28 Him I am ever proclaiming, warning every one and teaching every one, in all wisdom; that I may bring every man into his presence, full grown in Christ.
Yeye ndiye tunayemtangaza, tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu kwa hekima yote ili tuweze kumleta kila mmoja akiwa amekamilika katika Kristo.
29 For that end I am ever toiling, wrestling with all that energy of his which is mightily at work within me.
Kwa ajili ya jambo hili, ninajitaabisha, nikijitahidi kwa kadiri ya nguvu zake ambazo hutenda kazi ndani yangu kwa uweza mwingi.

< Colossians 1 >