< Acts 27 >
1 When it was decided that we should sail for Italy, they proceeded to hand over Paul and a few other prisoners to the custody of Julius, a centurion of the Imperial Regiment.
Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho “Kikosi cha Augusto.”
2 We embarked in a ship of Adramyttium which was about to sail to the ports of the province of Asia, and put to sea. Aristarchus, a Macedonian of Thessalonica, accompanied us.
Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
3 The next day we touched at Sidon. There Julius treated Paul kindly, and gave him leave to visit his friends and refresh himself.
Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
4 Putting to sea from thence we sailed under the lee of Cyprus, because the winds were against us;
Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
5 and after sailing across the Cilician and Pamphylian waters, we came to Myra, in Lycia.
Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
6 And there the centurion found an Alexandrian ship bound for Italy, and put us on board of her.
Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
7 For many days we sailed slowly, and then arrived with difficulty over against Cnidus; from this point, as the wind did not further favor us, we ran under the lee of Crete, off Cape Salmone;
Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
8 and coasting along with difficulty we reached a place called Fair Havens, not far from the town of Lasea.
Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo “Bandari Nzuri”, karibu na mji wa Lasea.
9 By this time the season was far advanced, and sailing had become dangerous (for the Autumn Fast was past); so Paul began to warn them.
Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
10 "Sirs," he said to them, "I perceive that the voyage will be attended with injury and serious loss, not only to the cargo and to the ship, but also to our own lives."
“Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu.”
11 But the centurion paid greater heed to the master and to the owner than to anything that was spoken by Paul;
Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
12 and as the harbor was ill adapted for winter quarters, the majority advised putting out to sea from thence, to see whether they could get to Phoenix and winter there, a harbor on the coast of Crete facing northeast and southeast.
Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
13 And when the south wind blew softly, supposing that they had obtained their purpose, they weighed anchor and sailed along Crete, close in shore.
Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
14 But it was not long before a furious wind, called Euroclydon, rushed down from the island;
Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao “Upepo wa Kaskazi” ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
15 when the ship was caught and could not face the wind, we gave way to it, and let her drive.
Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
16 Then we ran under the lee of a little island named Claudia, where with great difficulty we were able to secure the ship’s boat.
Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
17 After hauling it aboard, they used ropes to undergird the ship, and since they were fearful lest they should be driven upon the Syrtes, they lowered the gear and lay to.
Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
18 And as we were being terribly battered by the storm, the next day they began to throw the freight overboard,
Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
19 and on the third day with their own hands they threw the ship’s tackling overboard.
Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
20 Then when for many days neither sun nor stars were seen, and a great tempest still beat upon us, all hope that we should be saved was now taken away from us.
Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
21 When for a long time they had been without food, Paul stood among them and said. "Men, you ought to have listened to me, and not have set sail from Crete, and so have spared yourselves this injury and loss.
Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, “Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
22 "But now take courage. There will be no loss of life among you, but only of the ship,
Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
23 "for last night an angel of the God whose I am and whom I serve, stood by me and said.
Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
24 "‘Fear not, Paul; you must stand before Caesar. Behold, God has granted you the lives of all who are sailing with you.’
akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
25 "So take courage, men! I believe God, I believe that things will turn out exactly as it has been told me.
Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
26 "But we must be cast upon a certain island."
Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani.”
27 It was now the fourteenth night, and we were drifting through the Adriatic Sea when, about midnight, the sailors began to suspect that they were drawing near to some land.
Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
28 So they sounded and found twenty fathoms; and after a little they sounded again, and found fifteen fathoms.
Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
29 Then, fearing lest we should run ashore on the rocks, they threw out four anchors from the stern, and longed for day to come.
Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
30 And when the sailors were trying to flee from the ship, and had lowered the boat into the sea under pretext of laying anchors from the bow,
Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
31 Paul said to the centurion and to the soldiers, "Unless these men remain on the ship, you cannot be saved."
Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, “Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka.”
32 Then the soldiers cut the ropes of the ship’s boat and let her fall off.
Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
33 And while day was dawning, Paul kept urging them all to take some food. "This is the fourteenth day," he said, "that you have been on the watch, fasting, having eaten nothing.
Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: “Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
34 "So I beg you to take some food, for this is for your safety. For there shall not a hair perish from the head of any one of you."
Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.”
35 When he had so said and had taken bread, he gave thanks to God before them all, and broke it and began to eat.
Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
36 Then they all cheered up and themselves took food.
Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
37 There were in the ship two hundred and seventy-six souls, all told.
Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
38 After eating a hearty meal, they began to lighten the ship by throwing the wheat overboard.
Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
39 When it was day they tried in vain to recognize the land, but they spied an inlet with a sandy beach, and they began conferring to see whether they could drive the ship into it.
Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
40 They cast off the anchors and left them in the sea, and unloosing at the same time the ropes that tied the rudders, they hoisted the foresail to the breeze, and headed for the beach.
Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
41 But coming to a place where two seas met, they ran the ship aground; the bow struck and remained fixed, but the stern began to break up under the violence of the waves.
Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
42 Now the soldiers were planning to kill the prisoners, lest any of them should swim off and so escape.
Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
43 But the centurion kept them from their purpose, because he wished to save Paul. He gave orders that those who could swim should first jump overboard and get to land;
Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
44 and that the rest should follow, some on planks and some on other bits of wreckage. And so it came to pass that all escaped safe to the land.
na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.