< Romans 8 >
1 There is, then, no condemnation, now, to those who are in Christ Jesus.
Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu ya adhabu kwa wale walio ndani ya Kristo Yesu, wale ambao hawaenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho.
2 For the law of the Spirit of Life by Christ Jesus, has freed me from the law of sin, and of death.
Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima katika Kristo Yesu imeniweka huru mbali na sheria ya dhambi na mauti.
3 For what the law could not accomplish in that it was weak through the flesh; God sending his own Son, in the likeness of sinful flesh, accomplished; and by an offering for sin, condemned sin in the flesh.
Kwa maana kile ambacho sheria haikuwa na uwezo wa kufanya, kwa vile ilivyokuwa dhaifu katika mwili, Mungu kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe kwa mfano wa mwanadamu mwenye mwili ulio wa dhambi na kwa ajili ya dhambi, yeye aliihukumu dhambi katika mwili,
4 That the righteousness of the law might be fulfilled by us, who walk not according to the flesh, but according to the Spirit.
ili kwamba haki ipatikanayo kwa sheria itimizwe ndani yetu sisi, ambao hatuenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho.
5 Now, they who live according to the flesh, mind the things of the flesh; and they who live according to the Spirit, the things of the Spirit.
Kwa maana wale wanaoishi kwa kuufuata mwili huziweka nia zao katika vitu vya mwili, lakini wale wanaoishi kwa kufuata Roho, huziweka nia zao katika mambo ya Roho.
6 But the mind of the flesh is death; and the mind of the Spirit is life and peace:
Kwa maana kuwa na nia ya mwili ni mauti, bali kuwa na nia inayoongozwa na Roho ni uzima na amani.
7 because the mind of the flesh is enmity toward God: for, to the law of God it is not subject; neither, indeed, can be.
Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui na Mungu, kwa maana haiitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii.
8 Those, then, who are in the flesh, can not please God.
Wale wanaotawaliwa na mwili, hawawezi kumpendeza Mungu.
9 Now, you are not in the flesh, but in the Spirit; because the Spirit of God dwells in you. But, if any one have not the Spirit of Christ, he is none of his.
Lakini ninyi, hamtawaliwi na mwili, bali na Roho, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Mtu yeyote ambaye hana Roho wa Kristo, yeye si wa Kristo.
10 And if Christ be in you, the body, indeed, is dead, with respect to sin; but the Spirit is life, with respect to righteousness.
Lakini kama Kristo anakaa ndani yenu, miili yenu imekufa kwa sababu ya dhambi, lakini roho zenu zi hai kwa sababu ya haki.
11 For, if the Spirit of him, who raised up Jesus from the dead, dwell in you; he who raised up Christ from the dead, will make even your mortal bodies alive, through his Spirit, who dwells in you.
Nanyi ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu ataihuisha pia miili yenu ambayo hufa, kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
12 Well, then, brethren, we are not debtors to the flesh, to live according to the flesh.
Kwa hiyo ndugu zangu, sisi tu wadeni, si wa mwili, ili tuishi kwa kuufuata mwili,
13 Wherefore, if you live according to the flesh, you shall die; but if, through the Spirit, you put to death the deeds of the body, you shall live.
kwa maana mkiishi kwa kuufuata mwili, mtakufa, lakini kama mkiyaua matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.
14 Because, as many as are led by the Spirit of God, these are the sons of God.
Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio watoto wa Mungu.
15 For you have not received the spirit of bondage, again, to fear; but you have received the spirit of adoption, by which we cry, Abba, Father.
Kwa maana hamkupokea roho ya utumwa iwaleteayo tena hofu, bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambaye kwa yeye twalia, “Abba, yaani, Baba,”
16 Also this spirit bears witness, together with our spirit, that we are children of God.
Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kwamba sisi tu watoto wa Mungu.
17 And if children, then heirs; heirs, indeed, of God, and joint heirs with Christ; if, indeed, we suffer with him, that with him also we may be glorified.
Hivyo, ikiwa sisi ni watoto, basi tu warithi, warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo, naam, tukiteswa pamoja naye tupate pia kutukuzwa pamoja naye.
18 However, I esteem not the sufferings of the present time, as worthy of comparison with the glory, which is hereafter to be revealed in us.
Nayahesabu mateso yetu ya wakati huu kuwa si kitu kulinganisha na utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
19 For the earnest expectation of the creature, is waiting for the revelation of the sons of God.
Kwa maana viumbe vyote vinangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa watoto wa Mungu.
20 For the creature was subjected to frailty, (not of its own choice, but by him who has subjected it, ) in hope,
Kwa kuwa viumbe vyote viliwekwa chini ya ubatili, si kwa chaguo lao, bali kwa mapenzi yake yeye aliyevitiisha katika tumaini,
21 that it may be liberated, from the bondage of a perishing state, and brought into the glorious liberty of the sons of God.
ili kwamba viumbe vyote vipate kuwekwa huru kutoka kwa utumwa wa kuharibika na kupewa uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.
22 Besides, we know, that the whole creation sigh together, and travail in anguish till the present time.
Kwa maana twajua ya kuwa hata sasa viumbe vyote vimekuwa vikilia kwa maumivu kama utungu wa mwanamke wakati wa kuzaa.
23 And not only they, but ourselves also, who have the first fruit of the Spirit; even we ourselves, groan within ourselves, waiting for the adoption; namely, the redemption of our body.
Wala si hivyo viumbe peke yao, bali hata sisi ambao ndio matunda ya kwanza ya Roho, kwa ndani tunalia kwa uchungu tukisubiri kwa shauku kufanywa wana wa Mungu, yaani, ukombozi wa miili yetu.
24 For even we are saved by hope. Now, hope that is attained, is not hope; for who can hope for that which he enjoys?
Kwa kuwa tuliokolewa kwa tumaini hili. Lakini kama kinachotumainiwa kikionekana hakiwi tumaini tena. Je, kuna mtu anayetumaini kupata kitu alicho nacho tayari?
25 But if we hope for that which we do not enjoy, then, with patience, we wait for it.
Lakini tunapotumaini kupata kitu ambacho hatuna, basi twakingojea kwa saburi.
26 In like manner, also, the Spirit helps our infirmities; for we know not what we should pray for, as we ought; however, the Spirit himself intercedes for us, in sighs, which can not be uttered.
Vivyo hivyo, Roho hutusaidia katika udhaifu wetu, kwa sababu hatujui kuomba ipasavyo. Lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa uchungu usioweza kutamkwa.
27 But he who searches the hearts, knows the mind of the Spirit; that, according to the will of God, he makes intercession for the saints.
Naye Mungu aichunguzaye mioyo, anaijua nia ya Roho, kwa sababu Roho huwaombea watakatifu sawasawa na mapenzi ya Mungu.
28 Besides, we know, that all things work together for good, to them who love God; to them, who are called according to his purpose.
Nasi tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hutenda kazi pamoja na wote wampendao, katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.
29 For, whom he foreknew, he also predestinated to be conformed to the image of his Son; that he might be the first born among many brethren.
Maana wale Mungu aliowajua tangu mwanzo, pia aliwachagua tangu mwanzo, wapate kufanana na mfano wa Mwanawe, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
30 Moreover, whom he predestinated, them he also called; and whom he called, them he also justified; and whom he justified, them he also glorified.
Nao wale Mungu aliotangulia kuwachagua, akawaita, wale aliowaita pia akawahesabia haki, nao wale aliowahesabia haki, pia akawatukuza.
31 What shall we say, then, to these things? Since God is for us, who can be against us?
Tuseme nini basi kuhusu haya? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, ni nani awezaye kuwa kinyume chetu?
32 He, certainly, who spared not his own Son, but delivered him up for us all; how will he not, with him, also, graciously give us all things?
Ikiwa Mungu hakumhurumia Mwanawe, bali alimtoa kwa ajili yetu sote, atakosaje basi kutupatia vitu vyote kwa ukarimu pamoja naye?
33 Who will bring an accusation against the elect of God? Is it God who justifies them?
Ni nani atakayewashtaki wale ambao Mungu amewateua? Ni Mungu mwenyewe ndiye mwenye kuwahesabia haki.
34 Who is he, who condemns them? It is Christ, who died; or rather, who has risen: who also, is at the right hand of God; and who makes intercession for us?
Ni nani basi atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu aliyekufa, naam, zaidi ya hayo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yuko mkono wa kuume wa Mungu, naye pia anatuombea.
35 Who will separate us from the love of Christ? Will affliction, or distress, or persecution, or famine, or nakedness, or peril, or sword?
Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je, ni shida au taabu au mateso au njaa au uchi au hatari au upanga?
36 As it is written, "Truly, for thy sake, we are put to death all the day long; we are accounted as sheep for the slaughter."
Kama ilivyoandikwa: “Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.”
37 Nay, in all these things, we do more than overcome, through him who has loved us.
Lakini katika mambo haya yote tunashinda, naam na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.
38 For I am persuaded, that neither death, nor life; neither angels, nor principalities; nor powers; neither things present, nor to come;
Kwa maana nimekwisha kujua kwa hakika ya kuwa sio mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuja, wala wenye uwezo,
39 neither hight, nor depth; nor any created thing, shall be able to separate us from the love of God, which is in Christ Jesus our Lord.
wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kingine chochote zitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu, Bwana wetu.