< Revelation 9 >

1 And the fifth angel sounded; and I saw a Star fall from the heaven to the earth; and there was given to him the key of the bottomless pit. (Abyssos g12)
Malaika wa tano akaipiga tarumbeta yake, nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka toka angani hadi ardhini. Nyota hiyo ilipewa ufunguo wa lile Shimo. (Abyssos g12)
2 And he opened the bottomless pit, and smoke ascended from the pit, as the smoke of a great furnace: and the sun and the air were darkened by the smoke of the pit. (Abyssos g12)
Alipolifungua hilo Shimo, moshi ukapanda kutoka humo kama moshi wa tanuru kubwa sana. Jua na anga vikatiwa giza na ule moshi uliotoka katika hilo Shimo. (Abyssos g12)
3 And out of the smoke there came locusts upon the earth; and power was given to them, as scorpions of the earth have power.
Ndipo katika ule moshi wakatoka nzige wakaenda juu ya nchi, nao wakapewa nguvu kama zile za nge wa duniani.
4 And it was said to them that they should not injure the grass of the earth, nor any green thing, nor any tree; but the men who had not the seal of God in their foreheads.
Wakaambiwa wasidhuru nyasi ya nchi, wala mmea wala mti wowote, bali wawadhuru tu wale watu ambao hawana muhuri wa Mungu kwenye vipaji vya nyuso zao.
5 And it was not given to them to kill them, but to torment them five months: and their torment was like that of a scorpion when it stings a man.
Wakaruhusiwa kuwatesa kwa muda wa miezi mitano, lakini wasiwaue. Uchungu wa kuuma kwao ulikuwa kama ule wa mtu aumwapo na nge.
6 And in these days men shall seek death, and shall not find it: and they shall desire to die, and death shall fly from them.
Katika siku hizo watu watatafuta kifo lakini hawatakiona, watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.
7 And the resemblance of the locusts was like horses prepared for war; and on their heads were, as it were, crowns of gold; and and their faces were like the faces of men:
Wale nzige walikuwa na umbo kama la farasi waliotayarishwa kwa ajili ya vita. Kwenye vichwa vyao kulikuwa na kitu kama taji za dhahabu na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
8 and they had tresses, like the tresses of women; and their teeth were like the teeth of lions.
Walikuwa na nywele kama za wanawake, na meno yao yalikuwa kama ya simba.
9 And they had breastplates like breastplates of iron; and the noise of their wings was like the noise of chariots, and many horses rushing to war.
Walikuwa na dirii kama za chuma, na sauti za mabawa yao zilikuwa kama ngurumo za farasi wengi na magari mengi yakikimbilia vitani.
10 And they had tails like scorpions, and their stings were in their tails; and their power was to hurt men five months.
Walikuwa na mikia yenye miiba ya kuumia kama nge. Nguvu yao ya kutesa watu kwa huo muda wa miezi mitano ilikuwa katika hiyo mikia yao.
11 For they had a king over them, the angel of the bottomless pit, whose name, in the Hebrew language, is Abaddon; and in the Greek, he has the name Apollyon. (Abyssos g12)
Walikuwa na mfalme wao, ambaye ni malaika wa lile Shimo, ambaye jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani ni Apolioni. (Abyssos g12)
12 One woe is gone, and behold other two woes, besides it, yet coming.
Ole ya kwanza imepita, bado nyingine mbili zinakuja.
13 And the sixth angel sounded; and I heard a voice from the four horns of the golden altar which was before God,
Malaika wa sita akaipiga tarumbeta yake, nami nikasikia sauti ikitoka katika zile pembe za madhabahu ya dhahabu iliyoko mbele za Mungu.
14 saying to the sixth angel, who had the trumpet, Loose the four angels who are bound by the great river Euphrates.
Ile sauti ikamwambia yule malaika wa sita mwenye tarumbeta, “Wafungulie wale malaika wanne waliofungwa kwenye ule mto mkubwa Frati.”
15 And the four angels were loosed, who were prepared for an hour, and a day, and a month, and a year, to kill a third part of men.
Basi wale malaika wanne, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ajili ya saa hiyo, na siku hiyo, na mwezi huo, na mwaka huo ili wawaue theluthi ya wanadamu wakafunguliwa.
16 And the number of the horsemen was two myriads of myriads: I heard the number of them.
Idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa 200,000,000. Nilisikia idadi yao.
17 And I saw the horses, and those who sat upon them, thus in their appearance; having breastplates of fire, and hyacinth, and brimstone: and the heads of the horses were like the heads of lions, and out of their mouths went fire, and smoke, and brimstone.
Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika maono yangu: Wapanda farasi walivaa dirii vifuani zenye rangi nyekundu sana kama ya moto na yakuti samawi na kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vichwa vya simba, na moto, moshi na kiberiti vilitoka vinywani mwao.
18 With these three--by the fire, by the smoke, and by the brimstone--that went out of their mouths, they slew a third part of men.
Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo hayo matatu, yaani, huo moto, moshi na kiberiti, vilivyotoka kwenye vinywa vya hao farasi.
19 And their powers are in their mouths, and in their tails; and their tails are like serpents, having heads, and with them they injure.
Nguvu za hao farasi zilikuwa katika vinywa vyao na kwenye mikia yao, kwa sababu mikia yao ilikuwa kama nyoka, yenye vichwa ambayo waliitumia kudhuru.
20 Yet the remainder of men, who died not by these plagues, did not reform from the works of their hands, that they might not worship demons, and idols of gold, and silver, and brass, and stone, and wood; which can neither see, nor hear, nor walk.
Wanadamu waliosalia, ambao hawakuuawa katika mapigo hayo, bado walikataa kutubia kazi za mikono yao na hawakuacha kuabudu mashetani na sanamu za dhahabu, za fedha, za shaba, za mawe na za miti, ambazo haziwezi kuona, kusikia wala kutembea.
21 And they reformed not from their murders, and their magical incantations; nor from their fornication, nor their thefts.
Wala hawakutubu na kuacha matendo yao ya uuaji, uchawi, uasherati wala wizi wao.

< Revelation 9 >