< Revelation 6 >
1 And I saw, when the Lamb opened one of the seals; and I heard one of the four living creatures, which said, as with a voice of thunder, Come and see.
Kisha nikaangalia wakati Mwana-Kondoo akivunja ile lakiri ya kwanza miongoni mwa zile saba. Ndipo nikasikia mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akisema kwa sauti kama ya radi: “Njoo!”
2 And I saw, and behold, a white horse; and he who sat upon it, had a bow, and there was given him a crown; and he went forth conquering, and to conquer.
Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mweupe! Yeye aliyempanda alikuwa na upinde, naye akapewa taji, akampanda akatoka akiwa kama mshindi aelekeaye katika kushinda.
3 And when he opened the second seal, I heard the second living creature, saying, Come--
Alipoivunja ile lakiri ya pili, nikamsikia yule kiumbe wa pili mwenye uhai akisema, “Njoo!”
4 And another horse came out, which was red; and it was given to him who sat upon it, to take peace from the earth, and that they should slay each other; and there was given to him a great sword.
Ndipo akatokea farasi mwingine mwekundu sana. Yeye aliyempanda akapewa uwezo wa kuondoa amani duniani na kuwafanya watu wauane. Yeye akapewa upanga mkubwa.
5 And when he had opened the third seal, I heard the third living creature, saying, Come and see. And I saw, and behold, a black horse; and he who sat upon it, has a pair of scales in his hand.
Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tatu, nikamsikia yule kiumbe wa tatu mwenye uhai akisema, “Njoo!” Nikatazama, na mbele yangu alikuwepo farasi mweusi! Yeye aliyempanda alikuwa na mizani mkononi mwake.
6 And I heard a voice in the midst of the four living creatures, saying, A chenix of wheat for a denarius, and three chenices of barley for a denarius; you see that you injure not the oil, nor the wine.
Ndipo nikasikia kile kilichokuwa kama sauti katikati ya wale viumbe wanne wenye uhai ikisema, “Kipimo kimoja cha ngano kwa mshahara wa kibarua wa siku moja, na vipimo vitatu vya shayiri kwa mshahara wa kibarua cha siku moja. Lakini usiharibu mafuta wala divai!”
7 And when he opened the fourth seal, I heard the voice of the fourth living creature, saying, Come and see.
Alipovunja ile lakiri ya nne, nikasikia sauti ya yule kiumbe wa nne mwenye uhai ikisema, “Njoo!”
8 And I saw, and behold, a pale horse; and as for him who sat on it, his name was Death; and Hades followed him: and there was given to him power to slay the fourth part of the earth with the sword, and with famine, and with death, and with the wild beasts of the field. (Hadēs )
Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mwenye rangi ya kijivujivu! Yeye aliyempanda aliitwa Mauti, naye Kuzimu alikuwa akimfuata nyuma yake kwa karibu. Wakapewa mamlaka juu ya robo ya dunia, kuua kwa upanga, njaa, tauni na kwa wanyama wakali wa dunia. (Hadēs )
9 And when he opened the fifth sea, I saw, under the altar, the souls of those who were slaughtered on account of the word of God, and the testimony which they held.
Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tano, nikaona chini ya madhabahu, roho za wale waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu na kwa ajili ya ushuhuda walioutunza.
10 And they cried with a loud voice, and said, How long, O sovereign Lord, holy and true, before thou dost judge, and avenge our blood upon those who dwell on the earth?
Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, “Hata lini, Ee Bwana Mwenyezi, uliye mtakatifu na mwaminifu, hutawahukumu na kulipiza kisasi juu ya watu waishio duniani kwa ajili ya damu yetu?”
11 And there were given to each of them white robes; and it was said to them, that they should rest yet a while, till the number of their fellow-servants and brethren who should be killed, as they had been, should be completed.
Kisha kila mmoja wao akapewa joho jeupe na wakaambiwa wangoje kwa muda kidogo zaidi, mpaka idadi ya ndugu zao na watumishi wenzao watakaouawa kama wao walivyouawa, itakapotimia.
12 And I saw, when he opened the sixth seal, and there was an earthquake; and the sun became black as sackcloth of hair; and the moon became as blood;
Nikatazama akiivunja ile lakiri ya sita. Pakatokea tetemeko kuu la nchi, na jua likawa jeusi kama nguo ya gunia iliyotengenezwa kwa singa za mbuzi, na mwezi wote ukawa mwekundu kama damu.
13 and the stars fell from heaven, on the earth, as fig tree drops its untimely figs, being shaken by a mighty wind:
Nyota zilizo angani zikaanguka ardhini kama vile matunda ya mtini yasiyokomaa yaangukavyo wakati mti wake unapotikiswa na upepo mkali.
14 and the heavens passed away like a scroll, when it is rolled up; and every mountain, and island, was moved out of its place:
Anga ikatoweka kama vile karatasi isokotwavyo, na kila mlima na kila kisiwa kikaondolewa mahali pake.
15 and the kings of the earth, and the grandees, and the rich men, and the chief officers, and the powerful men, and every slave, and every freeman, hid themselves in the caves, and rocks of the mountains:
Ndipo wafalme wa dunia, wakuu wote, majemadari, matajiri, wenye nguvu na kila mtu, mtumwa na mtu huru, wakajificha katika mapango na kwenye miamba ya milima.
16 and they said to the mountains, and the rocks, Fall on us, and hide us from the face of him who sits on the throne, and from the wrath of the Lamb!
Wakaiita milima na miamba wakisema, “Tuangukieni, mkatufiche na uso wake yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na mkatuepushe na ghadhabu ya Mwana-Kondoo!
17 for the great day of his wrath is come, and who shall be able to stand?
Kwa maana siku ile kuu ya ghadhabu yao imewadia. Je, ni nani awezaye kustahimili?”