< Revelation 13 >
1 And I stood upon the sand of the sea, and saw a savage beast ascending out of the sea, having seven heads and ten horns; and upon its horns were ten diadems; and on its heads were the named of defamation.
Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari. Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru.
2 And the beast which I saw was like a leopard, and its feet were like those of a bear, and its mouth like the mouth of a lion; and the dragon gave it his power, and his throne, and great authority.
Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa.
3 And I saw one of its heads wounded, as it were, to death; and yet its mortal wound was healed. And the whole earth wondered, and followed after the wild beast;
Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama.
4 and they worshiped the dragon who gave authority to the wild beast, saying, Who is like to the beast? who can war against it?
Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”
5 And there was given to it a mouth speaking great things, and defamation: and there was given to it power to practice forty-two months--
Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
6 and it opened its mouth to utter defamation against God; to defame his name and his tabernacle, and those that dwell in heaven.
Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni.
7 And it was given to it to make war with the saints, and to overcome them: and there was given to it power over every tribe, and tongue, and nation.
Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa.
8 And all the inhabitants of the earth shall worship it, whose names are not written in the book of life of the Lamb, that was slain from the beginning of the world.
Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
9 If any one has an ear, let him hear.
Yeye aliye na sikio na asikie.
10 If any one lead them into captivity, he shall be led into captivity: if any one slay with the sword, he shall himself be slain with the sword. Here is the patience and the faith of the saints.
Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka, atachukuliwa mateka. Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.
11 And I saw another beast ascending out of the earth, and it had two horns like a lamb: but it spoke like a dragon.
Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka.
12 And it exercises all the power of the first beast, in its presence; and it makes the earth, and those that dwell in it, to worship the first beast, whose deadly wound was healed.
Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
13 And it does great miracles, so as to make fire come down from heaven to earth, before men;
Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi.
14 and it deceives the inhabitants of the earth by signs which it is given it to do before the beast; commanding the inhabitants of the earth to make an image of the beast that had the wound of the sword, and lived.
Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi.
15 And it was given to it to give breath to the image of the beast, that the image of the beast might speak, and cause as many as will not worship the image of the beast to be put to death.
Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa.
16 And he causes all, both small and great, rich and poor, freemen and slaves, to receive the mark on their right hand, or on their foreheads;
Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso,
17 and that no one should be able to buy or sell, but one who has the mark, the name of the beast, or the number of its name.
ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.
18 Here is wisdom: let him who has understanding, compute the number of the beast; for it is the number of a man; and its number is six hundred and sixty-six.
Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.