< Revelation 10 >
1 And I saw another mighty angel descending from heaven, clothed with a cloud; and a rainbow was about his head, and his face was as the sun, and his feet like pillars of fire.
Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingʼaa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
2 And he had in his hand a little book, open; and he put his right foot upon the sea, and the left upon the earth.
Mkononi mwake alikuwa ameshika kijitabu kilichokuwa kimefunguliwa. Akauweka mguu wake wa kuume juu ya bahari na mguu wake wa kushoto akauweka juu ya nchi kavu.
3 And he cried out with a loud voice, as when a lion roars: and when he cried, the seven thunders uttered their voices.
Naye akapiga kelele kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopiga kelele, zile radi saba zikatoa ngurumo zake.
4 And when the seven thunders had spoken, I was about to write: and I heard a voice from heaven, saying, Seal up what the seven thunders have spoken, and write it not.
Nazo zile radi saba zilipotoa ngurumo, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Yatie muhuri hayo yaliyosemwa na hizo radi saba na usiyaandike.”
5 And the angel, whom I saw standing on the sea and on the earth, lifted up his hand toward heaven,
Kisha yule malaika niliyekuwa nimemwona akiwa amesimama juu ya bahari na juu ya nchi akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni.
6 and swore by him that lives for ever and ever, who created the heaven, and those things which are in it; and the sea, and the things which are in it; and the earth, and the things which are in it; that there should be no longer delay. (aiōn )
Naye akaapa kwa Yule aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote viijazavyo, pamoja na bahari na vyote vilivyomo ndani yake, akasema, “Hakuna kungoja tena! (aiōn )
7 But in the days of the voice of the seventh angel; when he shall begin to sound, then the secret of God, as he had revealed its glad tidings to his servants the prophets, should be fulfilled.
Lakini katika siku zile ambazo huyo malaika wa saba atakapokaribia kuipiga hiyo tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa, kama vile alivyowatangazia watumishi wake manabii.”
8 And the voice which I heard from heaven spoke to me again, and said, Go, take the little book, which is open, out of the hand of the angel which stands upon the sea and upon the earth.
Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni ikasema nami tena ikaniambia, “Nenda, chukua kile kitabu kilichofunguliwa kilichoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
9 And I went to the angel, and said to him, Give me the little book. And he said to me, Take it, and eat it up; and it shall embitter your stomach, but in your mouth it shall be as sweet as honey.
Basi nikamwendea nikamwomba yule malaika anipe kile kitabu kidogo. Akaniambia, “Chukua na ukile. Kitakuwa kichungu tumboni mwako, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.”
10 And I took the little book out of the hand of the angel, and eat it up; and in my mouth it was sweet as honey, but when I had eaten it, my stomach was bitter.
Hivyo nikakichukua kile kitabu kidogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila. Kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu, lakini baada ya kukila, tumbo langu likatiwa uchungu.
11 And he said to me, You must again prophesy to many people, and nations, and tongues, and kings.
Kisha nikaambiwa, “Imekupasa kutoa unabii tena kuhusu makabila mengi, mataifa, lugha na wafalme.”