< Matthew 11 >
1 When Jesus had made an end of instructing his twelve disciples, he departed thence, to teach and give warning in the cities.
Baada ya Yesu kumaliza kutoa maagizo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka hapo akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.
2 Now John, having heard in prison of the works of the Messiah, sent two of his disciples,
Yohana aliposikia akiwa gerezani mambo ambayo Kristo alikuwa akiyafanya, aliwatuma wanafunzi wake
3 who asked him, Are you he that comes, or must we expect another?
ili wakamuulize, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
4 Jesus answering, said to them, Go, and relate to John, what you have heard and seen.
Yesu akajibu, “Rudini mkamwambie Yohana yale mnayosikia na kuyaona:
5 The blind are made to see, the lame to walk; lepers are cleansed; the deaf hear; the dead are raised; and good news is brought to the poor;
Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
6 and happy is he, to whom I shall not prove a stumbling block.
Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
7 When they were departed, Jesus said to the people concerning John, What did you go out into the wilderness to behold? A reed shaken by the wind?
Wale wanafunzi wa Yohana walipokuwa wanaondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
8 But what did you go out to see? A man effeminately dressed? It is king's palaces that such frequent.
Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari wako katika majumba ya wafalme.
9 What did you go to see? A prophet? Yes, I tell you, and something superior to a prophet:
Basi mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
10 for this is he, concerning whom it is written, "Behold I will send my angel before you, who shall prepare your way."
Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
11 Indeed, I say to you, among those that are born of women, there has not arisen a greater than John the Immerser. Yet the least in the Reign of Heaven is greater than he.
Amin, nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hajatokea mtu aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni ni mkuu kuliko Yohana.
12 From the first appearing of John the Immerser until now, the kingdom of heaven is invaded, and invaders take possession by force.
Tangu siku za Yohana Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wanauteka.
13 For till John appeared, all the prophets and the law were your instructions:
Kwa maana manabii wote na Sheria walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
14 and, if you will bear to be told it, this is the Elijah that was to come.
Ikiwa mko tayari kukubali hilo, yeye ndiye yule Eliya ambaye manabii walikuwa wamesema angekuja.
15 Whoever has ears to hear, let him hear.
Yeye aliye na masikio, na asikie.
16 But to what shall I liken this generation? It is like boys in the market places, to whom their playfellows complain,
“Lakini kizazi hiki nikifananishe na nini? Kinafanana na watoto waliokaa sokoni wakiwaita wenzao na kuwaambia,
17 saying, We have played to you upon the pipe, but you have not danced; we have sung mournful songs to you, but you have not lamented.
“‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkuomboleza.’
18 For John came abstaining from meat and drink, and they say, He has a demon;
Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali wala hanywi, nao wanasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
19 the Son of Man came using meat and drink, and they say, He is a lover of banquets and wine, a companion of publicans and sinners. But wisdom is justified by her children.
Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nao wanasema, ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’ Lakini hekima huthibitishwa kuwa kweli kwa matendo yake.”
20 Then he began to reproach the cities, in which most of his miracles had been performed, because they reformed not.
Ndipo Yesu akaanza kushutumu miji ambamo alifanya miujiza yake mingi kuliko kwingine, kwa maana watu wake hawakutubu.
21 Alas for thee, Chorazin! Alas for thee, Bethsaida! for if the miracles which have been performed in you, had been performed in Tyre and Sidon, they had reformed long ago in sackcloth and ashes.
“Ole wako, Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
22 Know, therefore, that the condition of Tyre and Sidon, on the day of judgment, shall be more tolerable than yours.
Lakini nawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
23 And thou, Capernaum, which hast been exalted to heaven, shalt be brought down to Hades; for, if the miracles which have been performed in thee, had been performed in Sodom, it had remained till now. (Hadēs )
Nawe Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu. Miujiza iliyofanyika kwako ingefanyika huko Sodoma, mji huo ungalikuwepo hadi leo. (Hadēs )
24 Know, therefore, that the condition of Sodom, on the day of judgment, shall be more tolerable than thine.
Lakini nakuambia kwamba, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ya hukumu kuliko wewe.”
25 On that occasion Jesus said, I adore thee, O Father, Lord of heaven and earth, because, having concealed these things from sages and the learned, thou hast revealed them to babes:
Wakati huo Yesu alisema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo.
26 yes, Father, because such is thy pleasure.
Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
27 My Father has imparted everything to me; and no one knows the Son, except the Father; neither knows any one the Father, except the Son, and he to whom the Son will reveal him.
“Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: Hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.
28 Come to me, all you who toil and are burdened, and I will give you rest.
“Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Take my yoke upon you, and be taught by me; for I am meek and condescending: and your souls shall find relief.
Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu.
30 For my yoke is easy and my burden is light.
Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”