< Luke 6 >

1 On the Sabbath called second prime, as Jesus was passing through the cornfields, his disciples plucked the ears of corn, and rubbed them in their hands and eat them.
Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2 And some Pharisees said to them, Why do you that which it is not lawful to do on the Sabbath?
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
3 Jesus replying, said to them, Did you never read what David and his attendants did, when they were hungry;
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4 how he entered the mansion of God, and took and eat the loaves of the presence, and gave also of this bread to his attendants; though it can not be lawfully eat by any but the priests?
Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
5 He added, The Son of Man is master even of the Sabbath.
Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
6 It happened also on another Sabbath, that he went into the synagogue and taught; and a man was there whose right hand was blasted.
Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 Now the Scribes and the Pharisees watched, to see whether he would heal on the Sabbath, that they might find matter for accusing him.
Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8 But he, knowing their thoughts, said to the man, whose hand was blasted, Arise, and stand in the middle. And he arose and stood.
Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9 Then Jesus said to them, I would ask you, What is it lawful to do on the Sabbath? Good or ill? To save, or to destroy?
Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 And, looking around on them all, he said to the man, stretch out your hand; and in doing this, his hand was rendered sound like the other.
Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11 But they were filled with madness, and consulted together, what they should do to Jesus.
Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12 In those days, Jesus retired to a mountain to pray, and spent the whole night in an oratory.
Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 When it was day, he called to him his disciples; and of them he chose twelve, whom he named Apostles.
Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14 Simon, whom he also named Peter, and Andrew, his brother, James, and John, Philip, and Bartholomew;
Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15 Matthew, and Thomas, James, son of Alpheus, and Simon called the Zealous,
Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16 Judas, brother of James, and Judas Iscariot, who proved a traitor.
Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17 Afterward, Jesus, coming down with them, stopped on a plain, where a company of his disciples, with a vast multitude from all parts of Judea, Jerusalem, and the maritime country of Tyre and Sidon,
Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18 were come to hear him, and to be healed of their diseases. Those also who were infested with unclean spirits, came, and were cured.
Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19 And every one strove to touch him, because a virtue came from him, which healed them all.
Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20 Then fixing his eyes on his disciples, he said, Happy you poor, for the kingdom of God is yours!
Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Happy you that hunger now, for you shall be satisfied! Happy you that weep now, for you shall laugh!
Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22 Happy shall you be when men shall hate you, and separate your from their society; yes, reproach and defame you, on account of the Son of Man!
“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23 Rejoice on that day, and triumph, knowing that your reward in heaven is great! for thus did their fathers treat the prophets.
Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24 But alas, for you rich; for you have received your comforts!
Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 Alas, for you that are full; for you shall hunger! Alas, for you who laugh now; for you shall mourn and weep!
Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26 Alas, when all men shall speak well of you; for so did their fathers of the false prophets.
Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 But I charge you, my hearers, love your enemies, do good to them who hate you,
“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28 bless them who curse you, pray for them who traduce you.
Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29 To him who smites you on one cheek, present the other; and from him who takes your mantle, withhold not your coat.
Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30 Give to every one who asks you; and from him who takes away your goods, do not demand them back.
Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31 And as you would that men should do to you, do you likewise to them.
Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32 For if you love those who love you, what thanks are you entitled to, since even sinners love those who love them?
“Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33 And if you do good to those who do good to you, what thanks are you entitled to, since even sinners do the same?
Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34 And if you lend to those from whom you hope to receive, what thanks are you entitled to, since even sinners lend to sinners, that they may received as much in return.
Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35 But love your enemies, do good and lend, nowise despairing; and your reward shall be great; and you shall be sons of the Most High; for he is kind to the ungrateful and malignant.
Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36 Be therefore merciful, as your Father is merciful.
Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 Judge not, and you shall not be judged; condemn not, and you shall not be condemned; release, and you shall be released;
“Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 give, and you shall get: good measure, pressed down and shaken, and heaped, shall be poured into your lap; for the very measure you give to others you yourself shall receive.
Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
39 He also used this comparison: Can the blind guide the blind? Will not both fall into a ditch?
Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40 The disciple is not above his teacher; but every finished disciple shall be as his teacher.
Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41 And why do you observe the mote in your brother's eyes; but perceive not the splinter in your own eye?
Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 Or how can you say to your brothers, Brother, let me take out the mote which is in your eye, not considering that there is a splinter out of your own eye; then you will see to take out the mote which is in your brother's eyes.
Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43 That is not a good tree which yields bad fruit; nor is that a bad tree which yields good fruit.
“Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44 For every tree is known by its own fruit. Figs are not gathered off thorns; nor grapes off a bramble-bush.
Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45 The good man, out of the good treasure of his heart, brings that which is good: the bad man out of the bad treasure of his heart, brings that which is bad; for it is out of the fulness of the heart that the mouth speaks.
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46 But why do you, in addressing me, cry, Master, Master, and obey not my commands!
“Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47 Whoever comes to me and hears my precepts, and practices them, I will show you whom he resembles:
Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48 he resembles a man who built a house, and digging deep, laid the foundation upon the rock: and when an inundation came, the torrent broke upon that house, but could not shake it; for it was founded upon rock.
Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49 But he who hears, and does not practice, resembles a man, who, without laying a foundation, built a house upon the earth: which, when the torrent broke against it, fell, and became a great pile of ruins.
Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”

< Luke 6 >