< Luke 16 >

1 He said, likewise, to his disciples, A certain rich man had a steward, who was accused to him of wasting his estate.
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Palikuwa na tajiri mmoja na msimamizi wake. Ilisemekana kwamba huyo msimamizi alikuwa anatumia vibaya mali ya tajiri yake.
2 Having, therefore, called him, he said, What is this that I hear of you? Render an account of your management, for you shall be steward no longer.
Hivyo huyo tajiri akamwita na kumuuliza, ‘Ni mambo gani haya ninayoyasikia kukuhusu? Toa taarifa ya usimamizi wako, kwa sababu huwezi kuendelea kuwa msimamizi.’
3 And the steward said within himself, What shall I do? My master takes from me the stewardship; I can not dig, and am ashamed to beg.
“Yule msimamizi akawaza moyoni mwake, ‘Nitafanya nini sasa? Bwana wangu ananiondoa katika kazi yangu. Sina nguvu za kulima, nami ninaona aibu kuombaomba.
4 I am resolved what to do, that when I am discarded, there may be some who will receive me into their houses.
Najua nitakalofanya ili nikiachishwa kazi yangu hapa, watu wanikaribishe nyumbani kwao.’
5 Having, therefore, sent severally for all his master's debtors, he asked one, How much do you owe my master?
“Kwa hiyo akawaita wadeni wote wa bwana wake, mmoja mmoja. Akamuuliza wa kwanza, ‘Deni lako kwa bwana wangu ni kiasi gani?’
6 He answered, A hundred baths of oil. Take back your bill, said the steward, sit down directly, and write fifty.
“Akajibu, ‘Galoni 800za mafuta ya mizeituni.’ “Msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati ya deni lako, ibadilishe upesi, uandike galoni 400.’
7 Then he asked another, How much do you owe? He answered, A hundred homers of wheat. Take back your bill, said he, and write eighty.
“Kisha akamuuliza wa pili, ‘Wewe deni lako ni kiasi gani?’ “Akajibu, ‘Vipimo 1,000vya ngano.’ “Yule msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati yako, andika vipimo 800!’
8 The master commended the prudence of the unjust steward; for the children of this world are more prudent in conducting their affairs, than the children of light. (aiōn g165)
“Yule bwana akamsifu yule msimamizi dhalimu kwa jinsi alivyotumia ujanja. Kwa maana watu wa dunia hii wana ujanja zaidi wanapojishughulisha na mambo ya dunia kuliko watu wa nuru. (aiōn g165)
9 Therefore, I say to you, with the deceitful riches procure to yourself friends, who, after your discharge, may receive you into the eternal mansion. (aiōnios g166)
Nawaambia, tumieni mali ya kidunia kujipatia marafiki, ili itakapokwisha, mkaribishwe katika makao ya milele. (aiōnios g166)
10 Whoso is faithful in little is faithful also in much: and whoso is unjust in little, is unjust also in much.
“Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, pia ni mwaminifu hata katika mambo makubwa, naye mtu ambaye si mwaminifu katika mambo madogo pia si mwaminifu katika mambo makubwa.
11 If, therefore, you have not been honest in the deceitful, who will intrust you with the true riches?
Ikiwa hamkuwa waaminifu katika mali ya kidunia, ni nani atakayewaaminia mali ya kweli?
12 And if you have been unfaithful managers for another, who will give you anything to manage for yourselves?
Nanyi kama hamkuwa waaminifu na mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
13 A servant can not serve two masters: for either he will hate one, and love the other; or, at least, will attend one, and neglect the other. You can not serve God and mammon.
“Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.”
14 When the Pharisees, who loved money, heard all these things, they ridiculed him.
Mafarisayo, waliokuwa wapenda fedha, waliyasikia hayo yote na wakamcheka kwa dharau.
15 But he said to them, As for you, you make yourselves pass upon men for righteous, but God knows your hearts; for that which is admired of men is abhorred of God.
Yesu akawaambia, “Ninyi mnajionyesha kuwa wenye haki mbele za wanadamu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana vile vitu ambavyo wanadamu wanavithamini sana, kwa Mungu ni machukizo.
16 You had the law and the prophets till the coming of John, since whose time, the kingdom of God is announced, and every occupant enters it by force.
“Sheria na Manabii vilihubiriwa mpaka kuja kwa Yohana Mbatizaji. Tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu zinahubiriwa, na kila mmoja hujiingiza kwa nguvu.
17 But sooner shall heaven and earth perish, than one tittle of the law shall fail.
Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita kuliko hata herufi moja kuondoka katika Sheria.
18 Whoever divorces his wife, and takes another, commits adultery; and whoever marries the divorced woman, commits adultery.
“Mtu yeyote amwachaye mkewe na kumwoa mwanamke mwingine anazini, naye mwanaume amwoaye mwanamke aliyetalikiwa anazini.
19 There was a certain rich man, that wore purple and fine linen, and feasted splendidly every day.
“Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, ambaye aliishi kwa anasa kila siku.
20 There was also a poor man named Lazarus, covered with sores, that was laid at his gate,
Hapo penye mlango wake aliishi maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima.
21 and who was desirous to feed on the crumbs which fell from the rich man's table: yes, even the dogs came and licked his sores.
Huyo Lazaro alitamani kujishibisha kwa makombo yaliyoanguka kutoka mezani kwa yule tajiri. Hata mbwa walikuwa wakija na kuramba vidonda vyake.
22 It happened that the poor man died, and was conveyed by angels to Abraham's bosom: the rich man also died, and was buried.
“Wakati ukafika yule maskini akafa, nao malaika wakamchukua akae pamoja na Abrahamu. Yule tajiri naye akafa na akazikwa.
23 And in hades, being in torments, he looked up, and saw Abraham afar off, and Lazarus in his bosom, (Hadēs g86)
Kule kuzimu alipokuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Abrahamu kwa mbali, naye Lazaro alikuwa karibu yake. (Hadēs g86)
24 and cried, saying, Have pity on me, father Abraham, and send Lazarus to dip the tip of his finger in water, and cool my tongue; for I am tortured in this flame.
Hivyo yule tajiri akamwita, ‘Baba Abrahamu, nihurumie na umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake ndani ya maji aupoze ulimi wangu, kwa sababu nina maumivu makuu kwenye moto huu.’
25 Abraham answered, Son, remember that you, in your lifetime, received good things, and Lazarus received evil things; but now he is in joy, and you are in torments.
“Lakini Abrahamu akamjibu, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba wakati wa uhai wako ulipata mambo mazuri, lakini Lazaro alipata mambo mabaya. Lakini sasa anafarijiwa hapa na wewe uko katika maumivu makuu.
26 Besides, there lies a huge gulf between us and you, so that they who would pass hence to you, can not: neither can they pass to us, who would come thence.
Zaidi ya hayo, kati yetu na ninyi huko kumewekwa shimo kubwa, ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko wasiweze, wala mtu yeyote asiweze kuvuka kutoka huko kuja kwetu.’
27 The other replied, I entreat you, then, father, to send him to my father's house;
“Akasema, ‘Basi, nakuomba, umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu,
28 for I have five brothers, that he may admonish them, lest they also come into this place of torment.
maana ninao ndugu watano. Awaonye, ili wasije nao wakafika mahali hapa pa mateso.’
29 Abraham answered, They have Moses and the prophets, let them hear them.
“Abrahamu akamjibu, ‘Ndugu zako wana Maandiko ya Mose na Manabii, wawasikilize hao.’
30 Nay, said he, father Abraham, but if one went to them from the dead, they would reform.
“Yule tajiri akasema, ‘Hapana, baba Abrahamu, lakini mtu kutoka kwa wafu akiwaendea, watatubu.’
31 Abraham replied, if they hear not Moses and the prophets, neither will they be persuaded though one should arise from the dead.
“Abrahamu akamwambia, ‘Kama wasipowasikiliza Mose na Manabii, hawataweza kushawishika hata kama mtu akifufuka kutoka kwa wafu.’”

< Luke 16 >