< Acts 27 >

1 And as it was determined that we should set sail into Italy, they delivered Paul, and some other prisoners, to a centurions of the Augustan Band, whose name was Julius.
Ilipoamuliwa kwamba tungesafiri kwa njia ya bahari kwenda Italia, Paulo na wafungwa wengine wakakabidhiwa kwa kiongozi mmoja wa askari aliyeitwa Juliasi, aliyekuwa wa Kikosi cha Walinzi wa Kaisari.
2 And going on board a ship of Adramyttis, we weighed anchor, intending to sail by the coasts of Asia; Aristarchus, a Macedonian, of Thessalonica, being with us.
Tulipanda meli iliyotoka Adramitio, iliyokuwa inakaribia kusafiri kwenda kwenye bandari zilizopo pwani ya Asia, tukaanza safari yetu tukiwa pamoja na Aristarko, Mmakedonia kutoka Thesalonike.
3 And the next day we reached Sidon: and Julius, treating Paul with great humanity, permitted him to go to his friends, and to enjoy the benefit of their care.
Kesho yake tukatia nanga Sidoni, naye Juliasi akamfanyia wema Paulo, akamruhusu aende kwa rafiki zake ili wamtimizie mahitaji yake.
4 And weighing anchor thence, we sailed under Cyprus, because the winds were contrary.
Kutoka huko tukaingia baharini tena na tukapita upande wa chini wa kisiwa cha Kipro kwa sababu upepo ulikuwa wa mbisho.
5 And sailing through the sea over against Cilicia and Pamphylia, we came to Myra, a city of Lycia.
Baada ya sisi kuvuka bahari iliyoko upande wa Kilikia na Pamfilia, tukafika Mira huko Likia.
6 And there, the centurion, finding a ship of Alexandria, bound for italy, put us on board of it.
Huko yule kiongozi wa askari akapata meli ya Iskanderia ikielekea Italia, akatupandisha humo.
7 And when we had sailed slowly for several days, and were hardly got over against Cnidus, the wind now permitting us; we sailed under Crete, over against Salmone:
Tukasafiri polepole kwa siku nyingi na kwa shida, hatimaye tukafika karibu na Nido. Kwa kuwa upepo wa mbisho ulituzuia tusiweze kushika mwelekeo tuliokusudia, tukapita chini ya Krete mkabala na Salmone.
8 and passing it with difficulty, we came to a certain place called the Fair Havens, in the neighborhood of which, was the city of Lasea.
Tukaambaa na pwani kwa shida, tukafika sehemu iitwayo Bandari Nzuri, karibu na mji wa Lasea.
9 And, as much time was spent, and sailing was now hazardous, because the fast was already over, Paul exhorted them,
Muda mwingi ulikuwa umepotea na kusafiri baharini kulikuwa hatari kwa sababu wakati huu ulikuwa baada ya siku za kufunga. Hivyo Paulo akawaonya akasema,
10 saying to them, Sirs, I perceive that this voyage will be attended with injury and great damage, not only to the lading and to the ship, but also to our lives.
“Mabwana, naona kuwa hii safari ni yenye maafa na ya kuleta hasara kubwa kwa meli na shehena, pia kwa maisha yetu.”
11 But the centurion paid greater regard to the pilot, and the master of the vessel, than to those things which were spoken by Paul.
Lakini badala ya yule kiongozi wa askari kusikiliza yale Paulo aliyosema, akafuata zaidi ushauri wa nahodha na mwenye meli.
12 And as the haven was not commodious to winter in, the greater part advised to set sail from thence, if they might possibly reach Phenice, to winter there;
Kwa kuwa ile bandari ilikuwa haifai kukaa wakati wa majira ya baridi, wengi wakashauri kwamba tuendelee na safari wakitarajia kufika Foinike na kukaa huko kwa majira ya baridi. Hii ilikuwa bandari iliyoko katika kisiwa cha Krete ikikabili upande wa kusini-magharibi na kaskazini-magharibi.
13 which is a haven of Crete, looking to the southwest and northwest: and as the south win blew gently, supposing they were secure of their purpose, they weighed anchor, and sailed on close to Crete.
Upepo mtulivu ulipoanza kuvuma toka kusini, wakadhani kuwa wangeweza kufikia lengo lao, hivyo wakangʼoa nanga na kusafiri wakipita kandokando ya pwani ya kisiwa cha Krete.
14 But not long after, there arose against her a tempestuous wind, which is called Euroclydon.
Lakini baada ya muda mfupi ikavuma tufani kubwa iitwayo “Eurakilo” toka kisiwa cha Krete.
15 And as the ship was violently hurried away, and was not able to bear up against the wind, we gave her up, and were driven.
Meli ikapigwa na dhoruba na haikuweza kushindana na ule upepo, tukarudishwa baharini upepo ulikokuwa unaelekea.
16 An running under a certain island, called Clauda, we were hardly able to get masters of the boat:
Hatimaye tukisafiri kupita chini ya kisiwa kidogo kiitwacho Kauda, ambapo kwa kuwa tulikuwa tumekingiwa upepo na hicho kisiwa, tuliweza kwa shida kuifunga mashua ya kuokolea watu.
17 which, when they had hoisted up, they used helps, undergirding the ship: and fearing, lest they should fall upon the quicksands, they struck sail, and so were driven.
Watu walipokwisha kuivuta mashua hiyo na kuiingiza katika meli, waliifunga kwa kamba chini ya meli yenyewe ili kuzishikanisha pamoja. Wakiogopa kupelekwa kwenye mchanga karibu na pwani ya Sirti, wakashusha matanga wakaiacha meli isukumwe na huo upepo.
18 And we were exceedingly tossed by the storm, the next day they lightened the ship:
Tulikuwa tunapigwa na dhoruba kwa nguvu, kiasi kwamba kesho yake walianza kutupa shehena toka melini.
19 and the third day we cast out, with our own hands, the tackling of the ship.
Siku ya tatu, wakatupa vyombo vya meli baharini kwa mikono yao wenyewe.
20 Now, as neither sun nor stars appeared for several days, and no small tempest pressed upon us, all remainder of hope that we might be delivered, was taken away.
Kulipokuwa hakuna kuonekana kwa jua wala nyota kwa siku nyingi, nayo dhoruba ikiwa inaendelea kuwa kali, hatimaye tulikata kabisa tamaa ya kuokoka.
21 And when there was great want of food, then Paul, standing in the midst of them, said, Sirs, you ought to have hearkened to me, and not to have loosed from Crete, and incurred this injury and loss.
Baada ya watu kukaa siku nyingi bila kula chakula, Paulo akasimama katikati yao akasema, “Enyi watu, iliwapasa kunisikiliza na kuacha kusafiri baharini kutoka Krete, ndipo ninyi mngekuwa mmejinusuru na uharibifu huu na hasara hii.
22 Nevertheless, even now I exhort you to be of good courage: for there shall be no loss of any life among you; but only of the ship.
Sasa ninawasihi sana, jipeni moyo mkuu kwa kuwa hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake, ila meli itaangamia.
23 For there appeared to me this night, an angel of the God whose I am, and whom I worship,
Jana usiku, malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake na ambaye ninamwabudu alisimama karibu nami,
24 saying, Fear not, Paul; you must be presented before Cesar; and, behold, God has given you all them that sail with you.
naye akasema, ‘Paulo usiogope, kwa kuwa ni lazima usimame mbele ya Kaisari, naye Mungu amekupa kwa neema uhai wa wote wanaosafiri pamoja nawe.
25 Wherefore, take courage, men; for I trust in God that it shall be so, even as it was told me.
Hivyo jipeni moyo, enyi watu, kwa kuwa ninamwamini Mungu kwamba yatakuwa kama vile alivyoniambia.’
26 But we must be cast upon a certain island.
Lakini hata hivyo meli yetu itakwama kwenye kisiwa fulani.”
27 And when the fourteenth night was come, as we were tossed up and down in the Adriatic sea, the mariners suspected, about midnight that they drew near to some land;
Usiku wa kumi na nne ulipofika, tulikuwa bado tunasukumwa na upepo katika Bahari ya Adria. Ilipokuwa yapata usiku wa manane, mabaharia wakahisi kwamba walikuwa wanakaribia nchi kavu.
28 and sounding, they found it twenty fathoms: and having gone a little way from thence, and sounding again, they found it fifteen fathoms.
Kwa hiyo wakapima kina cha maji na kukuta kilikuwa pima ishirini, baada ya kuendelea mbele kidogo wakapima tena wakapata kina cha pima kumi na tano.
29 And fearing lest they should fall upon some rocky shore, they cast four anchors out of the stern, and wished that the day would break.
Wakiogopa kwamba meli yetu ingegonga kwenye miamba, wakashusha nanga nne za nyuma ya meli, wakawa wanaomba kupambazuke.
30 But when the mariners endeavored to flee out of the ship, and had let down the boat into the sea, under pretense that they were about to carry out anchors from the ship-head;
Katika jaribio la kutoroka kutoka kwenye meli, mabaharia wakashusha mashua ya kuokolea watu baharini, wakijifanya kwamba wanakwenda kushusha nanga za omo.
31 Paul said to the centurion and the soldiers, Unless these continue in the ship, you can not be saved.
Ndipo Paulo akamwambia yule jemadari na askari, “Hawa watu wasipobaki katika meli, hamtaweza kuokoka.”
32 Then the soldiers cut off the cords of the boat, and let it fall off.
Hivyo basi wale askari wakakata kamba zilizoshikilia ile mashua ya kuokolea watu kwenye meli, wakaiacha ianguke humo baharini.
33 And while the day was coming on, Paul exhorted them all to take some food, saying, To-day, whilst waiting for this fourteenth day, you continue fasting, having taken nothing.
Kabla ya mapambazuko, Paulo akawasihi watu wote wale chakula akisema, “Leo ni siku ya kumi na nne mmekuwa katika wasiwasi mkiwa mmefunga na bila kula chochote.
34 I exhort you, therefore, to take a refreshment; for this is conducive to your safety: for not a hair shall fall from the head of any of you.
Kwa hiyo nawasihi mle chakula, kwa maana itawasaidia ili mweze kuishi. Kwa kuwa hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza unywele hata mmoja kutoka kichwani mwake.”
35 And when he had spoke thus, and had taken bread, he gave thanks to God, before them all; and having broken it, he began to eat.
Baada ya kusema maneno haya, Paulo akachukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega akaanza kula.
36 And being all encouraged, they also took some food.
Ndipo wote wakatiwa moyo, wakaanza kula chakula.
37 And we were in the ship, in all two hundred and seventy-six souls.
Ndani ya meli tulikuwa jumla ya watu 276.
38 And being satisfied with food, they lightened the ship; and cast the corn into the sea.
Baada ya watu wote kula chakula cha kutosha, wakapunguza uzito wa meli kwa kutupa ngano baharini.
39 And when it was day, they did not know the land: but they perceived a certain creek, with a shore, into which they determined, if they were able, to force the ship.
Kulipopambazuka, mabaharia hawakuitambua ile nchi, lakini waliona ghuba yenye ufuko wa mchanga, ambako waliamua kuipweleza meli kama ingewezekana.
40 And having cut off the anchors, leaving them in the sea, they, at the same time, loosing the rudder bands, and hoisting up the mainsail to the wind, pressed toward the shore.
Kwa hiyo wakatupa nanga zote na kuziacha baharini, na wakati huo huo wakalegeza kamba zilizokuwa zikishikilia usukani wa meli. Kisha wakatweka tanga la mbele lishike upepo na kuisukuma meli kuelekea pwani.
41 But falling on a place where two seas met, they ran the ship aground, and the fore part stuck fast, and remained immovable, while the hinder part was broken by the force of the waves.
Lakini wakafika mahali ambapo bahari mbili zinakutana, wakaipweleza meli ufuoni, omo ikakwama sana, ikawa haiwezi kuondolewa, lakini sehemu ya shetri ikavunjika vipande vipande kwa kule kupiga kwa mawimbi yenye nguvu.
42 And the counsel of the soldiers was, that they should kill the prisoners, lest any one should swim away, and escape.
Wale askari wakapanga kuwaua wale wafungwa ili kuzuia hata mmoja wao asiogelee na kutoroka.
43 But the centurion, being desirous to save Paul, hindered them from their purpose, and commanded those that could swim, to throw themselves out first, into the sea, and get away to land:
Lakini yule jemadari alitaka kuokoa maisha ya Paulo, basi akawazuia askari wasitekeleze mpango wao. Akaamuru wale wanaoweza kuogelea wajitupe baharini kwanza, waogelee mpaka nchi kavu.
44 and the remainder, some upon planks, and others upon some of the things of the ship. And so it happened that they all got safe to land.
Waliosalia wangefika nchi kavu kwa kutumia mbao au vipande vya meli iliyovunjika, hivyo ikatimia kwamba wote wakaokoka na kufika nchi kavu salama.

< Acts 27 >