< Acts 11 >

1 Now the Apostles and brethren who were in Jerusalem, heard, that the Gentiles also had received the word of God.
Mitume na ndugu walioamini waliokuwa huko Uyahudi wakasikia kuwa watu wa Mataifa nao wamepokea neno la Mungu.
2 And when Peter was come up to Jerusalem, they who were of the circumcision contended with him,
Hivyo Petro alipopanda Yerusalemu, wale wa tohara waliokuwa wameamini wakamshutumu,
3 saying, You did go in to men who were uncircumcised, and did eat with them.
wakisema, “Ulikwenda kwa watu wasiotahiriwa na kula pamoja nao.”
4 And Peter beginning, opened to them the matter in order, saying,
Ndipo Petro akaanza kuwaeleza kuhusu mambo yote yalivyotokea hatua kwa hatua akisema,
5 I was praying in the city of Joppa; and, in a trance, I saw a vision, something like a great sheet descending from heaven, let down by the four corners, and it came close to me:
“Nilikuwa katika mji wa Yafa nikiomba, nami nikapitiwa na usingizi wa ghafula, nikaona maono. Kulikuwa na kitu kama nguo kubwa ikishuka kutoka mbinguni, ikishushwa kwa ncha zake nne, nayo ikanikaribia.
6 and looking attentively upon it, I observed, and saw four-footed creatures of the earth, and wild beasts, and reptiles, and fowls of the air:
Nilipoangalia ndani yake kwa karibu niliona wanyama wenye miguu minne wa nchini, wanyama wa mwitu, watambaao na ndege wa angani.
7 and I heard a voice saying to me, Arise, Peter, kill, and eat:
Ndipo nikasikia sauti ikiniambia, ‘Petro, ondoka uchinje na ule.’
8 but I said, By no means, Lord; for nothing common or unclean has ever entered into my mouth.
“Nikajibu, ‘La hasha Bwana! Kitu chochote kilicho najisi hakijaingia kinywani mwangu.’
9 And the voice answered me the second time from heaven, Those things which God has cleansed, do not you call common.
“Sauti ikasema kutoka mbinguni mara ya pili, ‘Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.’
10 And this was done three times. And all the things were drawn up again into heaven.
Jambo hili lilitokea mara tatu, ndipo kile kitu kikavutwa tena mbinguni.
11 And behold, at that instant, three men were come to the house in which I was, sent from Cesarea to me.
“Wakati ule ule watu watatu, waliokuwa wametumwa kutoka Kaisaria waliwasili katika nyumba niliyokuwa nikikaa.
12 And the Spirit commanded me to go with them, without any scruple: and these six brethren also went along with me. And we entered into the man's house:
Roho Mtakatifu akaniambia niende nao bila kuwa na ubaguzi kati yao na sisi. Hawa ndugu sita pia walifuatana nami, nasi tukaingia nyumbani mwa huyo Kornelio.
13 and he told us how he had seen a messenger standing in his house, and saying to him, Send to Joppa, and bring hither Simon, whose surname is Peter;
Akatuambia jinsi alivyoona malaika aliyekuwa amesimama katika nyumba yake na kusema, ‘Tuma watu waende Yafa wakamlete Simoni aitwaye Petro.
14 who shall speak words to you, by which you and all your family shall be saved.
Yeye atakupa ujumbe ambao kwa huo wewe na wa nyumbani mwako wote mtaokoka.’
15 And as I began to speak, the Holy Spirit fell upon them, as as on us at the beginning.
“Nami nilipoanza kusema, Roho Mtakatifu akashuka juu yao kama vile alivyotushukia sisi hapo mwanzo.
16 And I remembered the word of the Lord, how he said, John immersed in water; but you shall be immersed in the Holy Spirit.
Nami nikakumbuka neno la Bwana alivyosema, ‘Yohana alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu.’
17 Since, therefore, God gave to them the same gift as he did to us, who had believed on the Lord Jesus Christ, what was I, that I should be able to obstruct God?
Basi ikiwa Mungu aliwapa hawa watu kipawa kile kile alichotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani hata nifikirie kuwa ningeweza kumpinga Mungu?”
18 And when they heard these things, they acquiesced, and glorified God; saying, God has, then, given to the Gentile also reformation to life.
Waliposikia haya hawakuwa na la kupinga zaidi. Nao wakamwadhimisha Mungu wakisema, “Basi, Mungu amewapa hata watu wa Mataifa toba iletayo uzima wa milele.”
19 Now, indeed, those who had been dispersed, on account of the distress which arose about Stephen, had traveled as far as Phenicia, and Cyprus, and Antioch, speaking the word to none but Jews only.
Basi wale waliotawanyika kwa ajili ya mateso yaliyotokana na kifo cha Stefano, wakasafiri hadi Foinike na Kipro na Antiokia. Nao hawakuhubiri lile Neno kwa mtu yeyote isipokuwa Wayahudi.
20 Yet some of the, being men of Cyprus, and Cyrene; when they came to Antioch, spoke to the Greeks, announcing the glad tidings concerning the Lord Jesus.
Lakini baadhi yao walikuwepo watu wa Kipro na Kirene, ambao walipokuja Antiokia walinena na Wayunani pia wakiwahubiria habari njema za Bwana Yesu.
21 And the hand of the Lord was with them, and a great number believed, and turned to the Lord.
Mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao, nayo idadi kubwa ya watu wakaamini na kumgeukia Bwana.
22 And the report concerning them came to the ears of the congregation that was at Jerusalem; and they sent Barnabas, to go as far as Antioch.
Habari hizi zilipofika masikioni mwa kanisa huko Yerusalemu, wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23 Who, when he was come, and beheld the favor of God, rejoiced, and exhorted them all to adhere to the Lord, with full determination of heart;
Alipofika na kuona madhihirisho ya neema ya Mungu, akafurahi na kuwatia moyo waendelee kuwa waaminifu kwa Bwana kwa mioyo yao yote.
24 for he was a good man, and full of the Holy Spirit, and of faith: and a considerable number were added to the Lord.
Barnaba alikuwa mtu mwema, aliyejaa Roho Mtakatifu, mwenye imani, nayo idadi kubwa ya watu wakaongezeka kwa Bwana.
25 Then Barnabas went to Tarsus, to seek Saul;
Kisha Barnaba akaenda Tarso kumtafuta Sauli,
26 and finding him, he brought him to Antioch. And it came to pass, that they assembled with the congregation, for a whole year, and taught considerable numbers; and the disciples were first named Christians at Antioch.
naye alipompata akamleta Antiokia. Hivyo kwa mwaka mzima Barnaba na Sauli wakakutana na kanisa na kufundisha idadi kubwa ya watu. Ilikuwa ni katika kanisa la Antiokia kwa mara ya kwanza wanafunzi waliitwa Wakristo.
27 And in these days prophets came from Jerusalem to Antioch.
Wakati huo manabii walishuka toka Yerusalemu hadi Antiokia.
28 And one of them, whose name was Agabus, stood up, and signified by the Spirit, that there should be a great famine over all the land: which came to pass in the days of Claudius.
Mmoja wao, jina lake Agabo, akasimama akatabiri kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itaenea ulimwengu mzima. Njaa hiyo ilitokea wakati wa utawala wa Klaudio.
29 And the disciples determined, that, according to the respective abilities of each, they should send to the assistance of the brethren who dwelt in Judea.
Mitume wakaamua kwamba kila mtu, kulingana na uwezo alio nao, atoe msaada kwa ajili ya ndugu wanaoishi Uyahudi.
30 And this they did, sending it to the elders, by the hands of Barnabas and Saul.
Wakafanya hivyo, misaada yao ikapelekwa kwa wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.

< Acts 11 >