< 1 Timothy 2 >
1 Now I exhort, first of all, that supplications, prayers, intercessions, and thanksgivings be made for all men;
Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
2 for kings, and all who are in authority, that we may lead a quiet and peaceable life in all godliness and honesty.
kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
3 For this is good and acceptable in the sight of God our Saviour,
Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
4 who wills all men to be saved, and to come to an acknowledgment of the truth.
anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
5 For there is one God, and one mediator between God and men, --the man Christ Jesus,
Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
6 who gave himself a ransom for all; --of which the testimony is in its proper season:
aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
7 for which I was appointed a herald and an Apostle, (I speak the truth, I do not falsify, ) a teacher to the Gentiles in faith and truth.
Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
8 I will, therefore, that the men pray everywhere, lifting up holy hands, without wrath and disputings.
Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
9 I like manner also, that the women adorn themselves in decent apparel, with modesty and sobriety, not with plaited hair, or gold, or pearls, or costly raiment:
Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10 but (which becomes women professing godliness, ) with good works.
bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
11 Let a woman learn in silence with all submission:
Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
12 for I do not allow a woman to teach, nor to usurp authority over a man, but to be silent;
Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
13 for Adam was first formed, then Eve.
Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
14 Besides, Adam was not deceived: but the woman, being deceived, was in transgression.
Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
15 However, she shall be saved through child-bearing, if they live in faith, and love, and holiness, with sobriety.
Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.