< 1 Corinthians 12 >
1 Now, concerning spiritual gifts, brethren, I would not have you ignorant.
Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
2 You know that you were Gentiles, led away to dumb idols, even as you happened to be led.
Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
3 Wherefore, I inform you, that no one, speaking by the Spirit of God, pronounces Jesus accursed; and, that no one can declare Jesus Lord, except by the Holy Spirit.
Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
4 Now, there are diversities of gifts, but the same spirit.
Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
5 And there are diversities of ministries, but the same Lord.
Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
6 And there are diversities of operations, but the same God, who works all in all.
Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
7 And to each is given this manifestation of the Spirit, for the advantage of all.
Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
8 For to one, indeed, is given, by the Spirit, the word of wisdom: and to another, the word of knowledge, according to the same Spirit.
Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
9 And to another, faith, by the same Spirit: and to another, healing, by the same Spirit:
Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
10 and to another, the operations of powers: and to another, prophecy: and to another, diverse kinds of foreign tongues: and to another, the interpretation of foreign tongues.
Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
11 Now, all these does the one and the same Spirit effectively work; distributing to each, respectively, as he pleases.
Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
12 For, as the body is one, although it have many members; and all the members of that one body, being many, are one body, so also is Christ.
Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
13 For, indeed, by one Spirit, we all have been immersed into one body; whether Jews or Greeks, whether slaves or freemen; and all have been made to drink of one Spirit.
Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
14 Since, then, the body is not one member, but many;
Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
15 if the foot shall say, Because I am not the hand, I am not of the body; is it, for this, not of the body?
Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
16 And if the ear shall say, Because I am not the eye, I am not of the body; is it, for this, not of the body?
Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
17 If the whole body were an eye, where were the hearing? If the whole were hearing, where were the smelling?
Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
18 But, now, God has placed the members, every one of them, in the body, as he has pleased.
Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
19 Besides, if all were one member, where were the body?
Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 But now, indeed, there are many members, but one body.
Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
21 Therefore, the eye can not say to the hand, I have no need of you: nor, again, the head to the feet, I have no need of you.
Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
22 Nay, those members of the body which seem to be more feeble, are necessary.
Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
23 And those which we think are less honorable members of the body, around them we throw more abundant honor; and so our uncomely members have more abundant comeliness.
Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
24 But, our comely members have no need. However, God has tempered the body together; having given to the member which wants it, more abundant honor.
wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
25 That there may be no schism in the body; but, that the members may have the very same anxious care, one for another.
ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
26 So, whether one member suffer, all the members sympathize; or, one member be honored, all the members rejoice together.
Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
27 Now, you are Christ's body, and members in particular.
Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
28 And these, indeed, God has placed in the congregation: first, Apostles; secondly, prophets; thirdly, teachers; next, powers; then, gifts of healing; helpers, directors, kinds of foreign languages.
Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
29 Are all Apostles? are all prophets? are all teachers? have all powers?
Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
30 have all the gift of healing? do all speak in foreign languages? do all interpret?
Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
31 Now, ardently desire the best gifts; and yet I show you a more excellent way.
Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.