< Zechariah 6 >
1 And I turn back, and lift up my eyes, and look, and behold, four chariots are coming forth from between two of the mountains, and the mountains [are] mountains of bronze.
Kisha nikageuka na kuinua macho na nikaona vibandawazi vinne vya farasi vikija kutoka kati ya milima miwili; na milima hiyo ilikuwa imetengenezwa kwa shaba.
2 In the first chariot [are] red horses, and in the second chariot brown horses,
Kibandawazi cha kwanza kilikuwa na farasi wekundu, kibandawazi cha pili kilikuwa na farasi weusi,
3 and in the third chariot white horses, and in the fourth chariot strong spotted horses.
kibandawazi cha tatu kilikuwa na farasi weupe, na kibandawazi cha nne kilikuwa na farasi wa kijivu.
4 And I answer and say to the messenger who is speaking with me, “What [are] these, my lord?”
Hivyo nikamwuliza malaika aliyesema nami, “Ni vitu gani hivi bwana wangu?”
5 And the messenger answers and says to me, “These [are] four spirits of the heavens coming forth from presenting themselves before the Lord of the whole earth.
Malaika akajibu na kuniambia, “Hizi ni pepo nne za mbinguni zisimamazo mbele ya Bwana wa dunia yote.
6 The brown horses that [are] therein, are coming forth to the land of the north; and the white have come forth to their back part; and the spotted have come forth to the land of the south;
Lenye farasi weusi linakwenda nchi ya kaskazini; farasi weupe wanakwenda nchi ya magharibi; na farasi wa kijivu wanakwenda nchi ya kusini.”
7 and the strong ones have come forth, and they seek to go to walk up and down in the earth”; and he says, “Go, walk up and down in the earth”; and they walk up and down in the earth.
Farasi hawa wenye nguvu walitoka na wanatafuta kwenda na kuzunguka juu ya nchi, hivyo malaika akasema, “Nendeni na mzunguke juu ya nchi!” nao wakaenda juu ya dunia yote.
8 And he calls me, and speaks to me, saying, “See, those coming forth to the land of the north have caused My Spirit to rest in the land of the north.”
Kisha akaniita na kuniambia, “Tazama wale wanaokwenda nchi ya kaskazini, wataituliza roho yangu juu nchi hiyo.”
9 And there is a word of YHWH to me, saying,
Hivyo neno la Yahwe likanijia kusema,
10 “Take of the captivity (who came from Babylon) from Heldai, from Tobijah, and from Jedaiah, and you have come in—you, in that day, indeed, you have come into the house of Josiah son of Zephaniah,
“Chukua sadaka kutoka kwa waliohamishwa - kutoka kwa Helidai, Tobiya na Yedaya - leo hii uende na kuipeleka katika nyumba ya Yosia mwana wa Zefania, aliyetoka Babeli.
11 and you have taken silver and gold, and have made a crown, and have placed [it] on the head of Joshua son of Josedech, the high priest,
Kisha uchukue fedha na dhahabu, ufanye taji na uivike katika kichwa cha Yoshua mwana wa Yehosadaki kuhani mkuu.
12 and have spoken to him, saying, Thus spoke YHWH of Hosts, saying, Behold, the Man! A Shoot—[is] His Name, And from His place He shoots up, And He has built the temple of YHWH.
Ongea naye na useme, Yahwe wa majeshi asema hivi: Mtu huyu, jina lake Tawi! Naye atakuwa alipo na kisha atajenga hekalu la Yahwe!
13 Indeed, He builds the temple of YHWH, And He carries away splendor, And He has sat and ruled on His throne, And has been a priest on His throne, And a counsel of peace is between both.
Ndiye atakayejenga hekalu la Yahwe naye atauinua utukufu wake; kisha ataketi na kutawala katika kiti chake cha enzi. Atakuwa kuhani juu ya kiti cha enzi na ufahamu wa amani utakuwa kati ya vyote viwili.
14 And the crown is to Helem, and to Tobijah, and to Jedaiah, and to Hen son of Zephaniah, for a memorial in the temple of YHWH.
Taji itawekwa hekaluni mwa Yahwe kwa heshima ya Heldai, Tobiya na Yedaya na kama kumbukumbu ya ukarimu wa mwana wa Zefania.
15 And the far-off come in, and they have built in the temple of YHWH, and you have known that YHWH of Hosts has sent me to you, indeed, it has come to pass, if you certainly listen to the voice of your God YHWH.”
Ndipo waliombali watakapokuja na kulijenga hekalu la Yahwe, hivyo mtajua kuwa Yahwe wa majeshi amenituma kwenu; kwani ikiwa kweli mnaisikiliza sauti ya Yahwe Mungu wenu hili litatendeka!”