< Ruth 3 >
1 And her mother-in-law Naomi says to her, “My daughter, do I not seek rest for you, that it may be well with you?
Naomi, mama mkwe wake, alimwambia, “Mwanangu, hainilazimu kutafuta mahali pa wewe kupumzika, ili kwamba mambo yako yaende vizuri?
2 And now, is not Boaz of our acquaintance, with whose young women you have been? Behold, he is winnowing the threshing-floor of barley tonight,
Naye Boazi, mtu ambaye umekuwa pamoja na wasichana wake wa kazi, yeye si jamaa yetu? Tazama, jioni hii atakuwa akikung'uta shairi katika sakafu ya kupuria.
3 and you have bathed, and anointed yourself, and put your garments on you, and gone down to the threshing-floor; do not let yourself be known to the man until he completes to eat and to drink;
Kwa hiyo, oga, jipake mafuta, uvae nguo zako nzuri, na ushuke kwenda kwenye sakafu ya kupuria. Lakini usijulikane kwa mtu huyu mpaka atakapo maliza kula na kunywa.
4 and it comes to pass, when he lies down, that you have known the place where he lies down, and have gone in, and uncovered his feet, and lain down—and he declares to you that which you do.”
Na uhakikishe kuwa, atakapo lala chini, ukumbuke mahali alipo lala ili kwamba baadaye uende kwake, ufunue miguu yake, na ulale hapo. Kisha atakuambia cha kufanya.”
5 And she says to her, “All that you say—I do.”
Ruth alimwambia Naomi, “Nitafanya kila kitu ulicho sema.”
6 And she goes down [to] the threshing-floor, and does according to all that her mother-in-law commanded her
Alishuka kwenda kwenye sakafu ya kupuria, na alifuata maelekezo aliyopewa na mama mkwe wake.
7 And Boaz eats and drinks, and his heart is glad; and he goes in to lie down at the end of the heap; and she comes in gently, and uncovers his feet, and lies down.
Boazi alipomaliza kula na kunywa na moyo wake ulikuwa na furaha, alienda kulala chini mwisho wa sehemu ya kuhifadhia nafaka. Kisha Ruth akaenda taratibu, akaaifunua miguu ya Boazi, na kulala hapo chini.
8 And it comes to pass, at the middle of the night, that the man trembles, and turns himself, and behold, a woman is lying at his feet.
Panapo usiku wa manane Boazi alisituka. Akajigeuza, na hapo mwanamke alikuwa amelala katika miguu yake!
9 And he says, “Who [are] you?” And she says, “I [am] Ruth your handmaid, and you have spread your skirt over your handmaid, for you [are] a redeemer.”
Akamwambia, “Wewe ni nani?” Akajibu, “Mimi ni Ruth, mtumishi wako wa kike. Nifunike shuka lako mimi mtumishi wako wa kike, kwa kuwa wewe ni jamaa wa karibu.”
10 And he says, “Blessed [are] you of YHWH, my daughter; you have dealt more kindly at the latter end than at the beginning—not to go after the young men, either poor or rich.
Boazi akamwambia, “Mwanangu, Yahweh akubariki. Umeonyesha wema mwishoni kuliko mwazoni, kwa sababu hukwenda kwa wanaume vijana, awe tajiri au masikini.
11 And now, my daughter, do not fear, all that you say I do to you, for all the gate of my people knows that you [are] a virtuous woman.
Na sasa, mwanangu, usiogope! Nitakufanyia yote unayosema, kwa sababu mji wa watu wangu wote wanajua kuwa wewe ni mwanamke unayestahili.
12 And now, surely, true, that I [am] a redeemer, but also there is a redeemer nearer than I.
Nikweli kuwa mimi ni jamaa wa karibu; hata hivyo, kuna jamaa wa karibu kuliko mimi.
13 Lodge tonight, and it has been in the morning, if he redeems you, well: he redeems; and if he does not delight to redeem you, then I have redeemed you—I; YHWH lives! Lie down until the morning.”
Baki hapa usiku huu, na asubuhi, ikiwa atafanya jukumu lake la jamaa wa karibu, vizuri, muache afanye jukumu lake la kindugu. lakini kama hata fanya jukumu la kindugu kwako, ndipo mimi nitafanya, kama Yahweh aishivyo. Lala mpaka asubuhi.”
14 And she lies down at his feet until the morning, and rises before one discerns another; and he says, “Let it not be known that the woman has come into the floor.”
Kwa hiyo Ruth alilala kwenye miguu ya Boazi hadi asubuhi. Lakini aliamka mapema kabla ya yeyote kuweza kumtambua mtu mwingine. Kwa kuwa alikwisha mwambia, “Isijulikane kuwa mwanamke alikuja kwenye sakafu ya kupuria.”
15 And he says, “Give the covering which [is] on you, and keep hold on it”; and she keeps hold on it, and he measures six [measures] of barley, and lays [it] on her; and he goes into the city.
Kisha Boazi akamwambia, lete mtandio wako na uushikilie.” Alipo fanya hivyo, alipima vipimo vikubwa sita vya shairi katika mtandio na kumtwisha Ruth. Kisha Boazi akaenda mjini.
16 And she comes to her mother-in-law, and she says, “Who [are] you, my daughter?” And she declares to her all that the man has done to her.
Ruth aliporudi kwa mama mkwe wake, alisema, “Ulifanyaje, mwanangu?” Ndipo Ruth akamwambia mambo yote aliyotendewa na mtu huyo.
17 And she says, “These six [measures] of barley he has given to me, for he said, You do not go in empty to your mother-in-law.”
Alimwambia, “Hivi vipimo sita vya shairi ni vile alivyonipa yeye, kwa kuwa alisema, 'Usiende mikono mitupu kwa mama mkwe wako.'”
18 And she says, “Sit still, my daughter, until you know how the matter falls, for the man does not rest except he has completed the matter today.”
Kisha Naomi akasema, “Baki hapa, mwanangu, mpaka utakapojua yatakavyo kuwa, kwa kuwa Boazi hata pumzika mpaka atakapolimaliza jambo hili leo.”