< Romans 3 >

1 What, then, [is] the superiority of the Jew? Or what the profit of the circumcision?
Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Au kuna thamani gani katika tohara?
2 Much in every way; for first, indeed, that they were entrusted with the oracles of God;
Kuna faida kubwa kwa kila namna! Kwanza kabisa, Wayahudi wamekabidhiwa lile Neno halisi la Mungu.
3 for what, if certain were faithless? Will their faithlessness make the faithfulness of God useless?
Ingekuwaje kama wengine hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kungebatilisha uaminifu wa Mungu?
4 Let it not be! And let God become true, and every man false, according as it has been written: “That You may be declared righteous in Your words, and may overcome in Your being judged.”
La hasha! Mungu na aonekane mwenye haki, na kila mwanadamu kuwa mwongo, kama ilivyoandikwa: “Ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena, na ukashinde utoapo hukumu.”
5 And if our unrighteousness establishes God’s righteousness, what will we say? Is God unrighteous who is inflicting the wrath? (I speak after the manner of a man.)
Ikiwa uovu wetu unathibitisha haki ya Mungu waziwazi, tuseme nini basi? Je, Mungu kuileta ghadhabu yake juu yetu ni kwamba yeye si mwenye haki? (Nanena kibinadamu.)
6 Let it not be! Since how will God judge the world?
La hasha! Kama hivyo ndivyo ilivyo, Mungu angehukumuje ulimwengu?
7 For if the truth of God in my falsehood abounded more to His glory, why am I also yet judged as a sinner?
Mtu aweza kuuliza, “Kama uongo wangu unasaidia kuonyesha kweli ya Mungu na kuzidisha utukufu wake, kwa nini basi mimi nahukumiwa kuwa mwenye dhambi?”
8 And not, as we are spoken evil of, and as certain affirm us to say, “We may do the evil things, that the good ones may come?” Whose judgment is righteous.
Nasi kwa nini tusiseme, kama wengine wanavyotusingizia kuwa tunasema, “Tutende maovu ili mema yapate kuja?” Wao wanastahili hukumu yao.
9 What, then? Are we better? Not at all! For we charged before both Jews and Greeks with being all under sin,
Tusemeje basi? Je, sisi ni bora kuwaliko wao? La hasha! Kwa maana tumekwisha kuhakikisha kwa vyovyote kwamba Wayahudi na watu wa Mataifa wote wako chini ya nguvu ya dhambi.
10 according as it has been written: “There is none righteous, not even one;
Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.
11 there is none who is understanding, there is none who is seeking after God.
Hakuna hata mmoja mwenye ufahamu, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu.
12 All went out of the way, together they became unprofitable, there is none doing good, there is not even one.
Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja.”
13 Their throat [is] an opened grave; with their tongues they used deceit; poison of cobras [is] under their lips—
“Makoo yao ni makaburi wazi; kwa ndimi zao wao hufanya udanganyifu.” “Sumu ya nyoka iko midomoni mwao.”
14 whose mouth is full of cursing and bitterness.
“Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.”
15 Their feet [are] swift to shed blood.
“Miguu yao ina haraka kumwaga damu;
16 Ruin and misery [are] in their ways.
maangamizi na taabu viko katika njia zao,
17 And a way of peace they did not know.
wala njia ya amani hawaijui.”
18 There is no fear of God before their eyes.”
“Hakuna hofu ya Mungu machoni pao.”
19 And we have known that as many things as the Law says, to those in the Law it speaks, that every mouth may be stopped, and all the world may come under judgment to God;
Basi tunajua ya kwamba chochote sheria inachosema, inawaambia wale walio chini ya sheria ili kila kinywa kinyamazishwe na ulimwengu wote uwajibike kwa Mungu.
20 for this reason by works of law will no flesh be declared righteous before Him, for through law is a knowledge of sin.
Kwa hiyo hakuna binadamu hata mmoja atakayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya sheria, kwa maana sheria hutufanya tuitambue dhambi.
21 And now apart from law the righteousness of God has been revealed, testified to by the Law and the Prophets,
Lakini sasa, haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa pasipo sheria, ambayo Sheria na Manabii wanaishuhudia.
22 and the righteousness of God [is] through the faith of Jesus Christ to all, and on all those believing—for there is no difference,
Haki hii itokayo kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wamwaminio. Kwa maana hapo hakuna tofauti,
23 for all have sinned and fall short of the glory of God—
kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,
24 being declared righteous freely by His grace through the redemption that [is] in Christ Jesus,
wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
25 whom God set forth [as] a propitiatory covering, through faith in His blood, for the showing forth of His righteousness, because of the passing over of the former sins in the forbearance of God—
Yeye ambaye Mungu alimtoa awe dhabihu ya upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alifanya hivi ili kuonyesha haki yake, kwa sababu kwa ustahimili wake aliziachilia zile dhambi zilizotangulia kufanywa.
26 for the showing forth of His righteousness in the present time, for His being righteous, and declaring him righteous who [is] of the faith of Jesus.
Alifanya hivyo ili kuonyesha haki yake wakati huu, ili yeye awe mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yule anayemwamini Yesu.
27 Where then [is] the boasting? It was excluded; by what law? Of works? No, but by a law of faith:
Basi, kujivuna kuko wapi? Kumewekwa mbali. Kwa sheria gani? Je, ni kwa ile ya matendo? La hasha, bali kwa ile sheria ya imani.
28 therefore we reckon a man to be declared righteous by faith, apart from works of law.
Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
29 [Is He] only the God of Jews, and not also of nations?
Je, Mungu ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Naam, yeye ni Mungu wa watu wa Mataifa pia.
30 Yes, also of nations; since [there is] one God who will declare righteous circumcision by faith, and uncircumcision through faith.
Basi kwa kuwa tuna Mungu mmoja tu, atawahesabia haki wale waliotahiriwa kwa imani na wale wasiotahiriwa kwa imani iyo hiyo.
31 Do we then make law useless through faith? Let it not be! Indeed, we establish law.
Je, basi ni kwamba tunaibatilisha sheria kwa imani hii? La, hasha! Badala yake tunaithibitisha sheria.

< Romans 3 >