< Revelation 9 >
1 And the fifth messenger sounded the trumpet, and I saw a star having fallen to the earth out of Heaven, and there was given to him the key of the pit of the abyss, (Abyssos )
Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la Kuzimu. (Abyssos )
2 and [he] opened the pit of the abyss, and there came up a smoke out of the pit as smoke of a great furnace, and the sun and the air were darkened from the smoke of the pit. (Abyssos )
Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la Kuzimu, kukatoka moshi wa tanuru kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa Kuzimu. (Abyssos )
3 And out of the smoke came forth locusts to the earth, and there was given to them authority, as scorpions of the earth have authority,
Nzige wakatoka katika moshi huo, wakaingia duniani wakapewa nguvu kama ya ng'e.
4 and it was said to them that they may not injure the grass of the earth, nor any green thing, nor any tree, but only the men who do not have the seal of God on their foreheads,
Wakaamrishwa wasiharibu nyasi za nchi wala majani wala miti yoyote, bali wawaharibu wale tu ambao hawakupigwa mhuri wa Mungu katika paji la uso.
5 and it was given to them that they may not kill them, but that they may be tormented five months, and their torment—as the torment of a scorpion—when it may strike a man;
Nzige hao hawakuruhusiwa kuwaua watu, ila kuwatesa tu kwa muda wa miezi mitano. Maumivu watakayosababisha ni kama maumivu yanayompata mtu wakati anapoumwa na ng'e.
6 and in those days men will seek death and they will not find it, and they will desire to die, and death will flee from them.
Muda huo watu watatafuta kifo lakini hawatakipata; watatamani kufa lakini kifo kitawakimbia.
7 And the likenesses of the locusts—like to horses made ready to battle, and on their heads [something] as garlands like gold, and their faces as faces of men,
Kwa kuonekana, nzige hao walikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita. Juu ya vichwa vyao walikuwa na taji zilizo kama za dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
8 and they had hair as hair of women, and their teeth were as [those] of lions,
Nywele zao zilikuwa kama nywele za wanawake, na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
9 and they had breastplates as breastplates of iron, and the noise of their wings—as the noise of chariots of many horses running to battle;
Vifua vyao vilikuwa vimefunikwa kitu kama ngao ya chuma. Sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya msafara wa magari ya farasi wengi wanaokimbilia vitani.
10 and they have tails like to scorpions, and stings were in their tails; and their authority [is] to injure men five months;
Walikuwa na mikia na miiba kama ng'e, na kwa mikia hiyo, walikuwa na nguvu ya kuwadhuru watu kwa muda wa miezi mitano.
11 and they have over them a king—the messenger of the abyss—a name [is] to him in Hebrew, Abaddon, and in the Greek he has a name, Apollyon. (Abyssos )
Tena wanaye mfalme anayewatawala, naye ndiye malaika wa kuzimu; jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki ni Apolioni, yaani mwangamizi. (Abyssos )
12 The first woe went forth, behold, there yet come two woes after these things.
Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanafuata.
13 And the sixth messenger sounded the trumpet, and I heard a voice out of the four horns of the altar of gold that is before God,
Kisha malaika wa sita akapiga tarumbeta yake. Nami nikasikia sauti moja kutoka katika pembe nne za madhabahu ya dhahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.
14 saying to the sixth messenger who had the trumpet, “Loose the four messengers who are bound at the great river Euphrates”;
Sauti hiyo ikamwambia huyo malaika wa sita mwenye tarumbeta, “Wafungulie malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Eufrate!”
15 and the four messengers were loosed, who have been made ready for the hour, and day, and month, and year, that they may kill the third of mankind;
Naye akawafungulia malaika hao wanne ambao walikuwa wametayarishwa kwa ajili ya saa hiyo ya siku ya mwezi huo, wa mwaka huohuo, kuua theluthi moja ya wanaadamu.
16 and the number of the forces of the horsemen—twice ten thousand ten thousands, and I heard the number of them.
Nilisikia idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa milioni mia mbili.
17 And thus I saw the horses in the vision, and those sitting on them, having breastplates of fire, and jacinth, and brimstone; and the heads of the horses [are] as heads of lions, and out of their mouths proceed fire, and smoke, and brimstone;
Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika hiyo njozi: Walikuwa na ngao vifuani zilizokuwa moto mtupu, zenye rangi ya samawati na njano kama kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vya simba; na moto, moshi, na kiberiti vilikuwa vinatoka kinywani mwao.
18 by these three plagues the third of mankind was killed, from the fire, and from the smoke, and from the brimstone, that is proceeding out of their mouths,
Theluthi moja ya wanaadamu waliuawa kwa mabaa hayo matatu yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliyokuwa yanatoka katika vinywa vyao;
19 for the power of the horses are in their mouth, and in their tails, for their tails [are] like serpents, having heads, and they injure with them.
maana nguvu ya farasi hao ilikuwa vinywani mwao na katika mikia yao. Mikia yao ilikuwa na vichwa kama nyoka, na waliitumia hiyo kuwadhuru watu.
20 And the rest of mankind, who were not killed in these plagues, neither converted from the works of their hands, that they may not worship the demons, and idols, those of gold, and those of silver, and those of brass, and those of stone, and those of wood, that are neither able to see, nor to hear, nor to walk,
Wanaadamu wengine waliobaki ambao hawakuuawa na mabaa hayo, hawakugeuka na kuviacha vitu walivyokuwa wametengeneza kwa mikono yao wenyewe; bali wakaendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti, vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia wala kutembea.
21 and they did not convert from their murders, nor from their sorceries, nor from their whoredoms, nor from their thefts.
Wala hawakutubu na kuacha kufanya mauaji, uchawi, uzinzi, na wizi.