< Revelation 8 >

1 And when He opens the seventh seal, there came silence in Heaven about half an hour,
Wakati Mwanakondoo alipofungua muhuri ya saba, kukawa na ukimya mbinguni takribani nusu saa.
2 and I saw the seven messengers who have stood before God, and there were given to them seven trumpets,
Kisha nikaona malaika saba wasimamao mbele za Mungu, na wakapewa tarumbeta saba.
3 and another messenger came, and he stood at the altar, having a golden censer, and there was given to him much incense, that he may give [it] to the prayers of all the holy ones on the golden altar that [is] before the throne,
Malaika mwingine akaja, ameshikilia bakuli ya dhahabu yenye uvumba, amesimama madhabahuni. Akapewa uvumba mwingi ili kwamba autoe pamoja na maombi ya waamini wote katika madhabahu ya dhahabu mbele ya kiti cha enzi.
4 and the smoke of the incenses, with the prayers of the holy ones, went up before God out of the hand of the messenger;
Moshi wa ule uvumba, pamoja na maombi ya waamini, ukapanda juu mbele za Mungu kutoka mkononi mwa malaika.
5 and the messenger took the censer, and filled it out of the fire of the altar, and cast [it] to the earth, and there came voices, and thunders, and lightnings, and an earthquake.
Malaika akatwaa bakuli la uvumba na akalijaza moto kutoka kwenye madhabahu. Kisha akalitupa chini juu ya nchi, na kukatokea sauti za radi, miale ya radi na tetemeko la nchi.
6 And the seven messengers who are having the seven trumpets prepared themselves that they may sound the trumpets;
Wale malaika saba ambao walikuwa na tarumbeta saba wakawa tayari kuzipiga.
7 and the first messenger sounded the trumpet, and there came hail and fire, mingled with blood, and it was cast to the earth, and the third of the trees were burned up, and all the green grass was burned up.
Malaika wa kwanza akaipiga tarumbeta yake, na kukatokea mvua ya mawe na moto uliochanganyikana na damu. Vikatupwa chini katika nchi ili kwamba theluthi yake iungue, theluthi ya miti ikaungua na nyasi zote za kijani zikaungua.
8 And the second messenger sounded the trumpet, and [something] like a great mountain burning with fire was cast into the sea, and the third of the sea became blood,
Malaika wa pili akaipiga tarumbeta yake, na kitu kama mlima mkubwa uliokuwa unaungua kwa moto ukatupwa baharini. Theluthi ya bahari ikawa damu,
9 and the third of the creatures that [are] in the sea died, those having life, and the third of the ships were destroyed.
theluthi ya viumbe hai katika bahari vikafa, na theluthi ya meli zikaharibiwa.
10 And the third messenger sounded the trumpet, and there fell out of the sky a great star, burning as a lamp, and it fell on the third of the rivers, and on the fountains of waters,
Malaika wa tatu akaipiga tarumbeta yake, na nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, ikimulika kama kurunzi, juu ya theluthi ya mito na chemichemi za maji.
11 and the name of the star is called Wormwood, and the third of the waters become wormwood, and many of the men died [because] of the waters, because they were made bitter.
Jina la nyota ni pakanga. Theluthi ya maji ikawa pakanga, na watu wengi wakafa kutokana na maji yaliyokuwa machungu.
12 And the fourth messenger sounded the trumpet, and the third of the sun was struck, and the third of the moon, and the third of the stars, that the third of them may be darkened, and that the day may not shine—the third of it, and the night in like manner.
Malaika wa nne alipiga tarumbeta yake, na theluthi ya jua ikapigwa, pamoja na theluthi ya mwezi na theluthi ya nyota. Kwa hiyo theluthi ya vyote ikageuka kuwa giza; theluthi ya mchana na theluthi ya usiku havikuwa na mwanga.
13 And I saw, and I heard one messenger, flying in midair, saying with a great voice, “Woe, woe, woe, to those dwelling on the earth because of the rest of the voices of the trumpet of the three messengers being about to sound trumpets.”
Nilitazama, na nikasikia tai aliye kuwa anaruka katikati ya anga, akiita kwa sauti kuu, “Ole, ole, ole, kwa wale wakaao katika nchi, kwa sababu ya mlipuko wa tarumbeta iliyosalia ambayo imekaribia kupigwa na malaika watatu.”

< Revelation 8 >