< Revelation 15 >
1 And I saw another sign in the sky, great and wonderful: seven messengers having the seven last plagues, because in these the wrath of God was completed,
Ndipo nikaona ishara nyingine kubwa ya ajabu mbinguni: malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika.
2 and I saw as a sea of glass mingled with fire, and those who gain the victory over the beast, and his image, and his mark, [and] the number of his name, standing by the sea of the glass, having harps of God,
Nikaona kile kilichoonekana kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu.
3 and they sing the song of Moses, servant of God, and the song of the Lamb, saying, “Great and wonderful [are] Your works, O LORD God, the Almighty, righteous and true [are] Your ways, O King of holy ones!
Nao wakaimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, matendo yako ni makuu na ya ajabu. Njia zako wewe ni za haki na za kweli, Mfalme wa nyakati zote!
4 Who may not fear You, O LORD, and glorify Your Name? Because You alone [are] holy, because all the nations will come and worship before You, because Your righteous acts were revealed.”
Ni nani ambaye hatakuogopa wewe Bwana na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako ndiwe mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo yako ya haki yamedhihirishwa.”
5 And after these things I saw, and behold, the temple of the Dwelling Place of the Testimony was opened in Heaven;
Baada ya haya nikatazama, nalo hekalu, la hema la Ushuhuda, lilikuwa limefunguliwa mbinguni.
6 and the seven messengers having the seven plagues came forth out of the temple, clothed in linen, pure and radiant, and girded around the breasts with golden girdles:
Ndani ya lile hekalu wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za kitani ingʼaayo na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao.
7 and one of the four living creatures gave to the seven messengers seven golden bowls, full of the wrath of God, who is living through the ages of the ages; (aiōn )
Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele. (aiōn )
8 and the temple was filled with smoke from the glory of God, and from His power, and no one was able to enter into the temple until the seven plagues of the seven messengers may be completed.
Nalo lile hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake, wala hakuna yeyote aliyeweza kuingia mle hekaluni mpaka yale mapigo saba ya wale malaika saba yalipomalizika.