< Revelation 14 >

1 And I saw, and behold, a Lamb was standing on Mount Zion, and with Him one hundred forty-four thousand, having the Name of His Father written on their foreheads;
Kisha nikaona mlima Sioni, na Mwanakondoo amesimama juu yake; pamoja naye walikuwa watu mia moja arobaini na nne elfu ambao juu ya paji za nyuso zao walikuwa wameandikwa jina la Mwanakondoo na jina la Baba yake.
2 and I heard a voice out of Heaven, as a voice of many waters, and as a voice of great thunder, and I heard a voice of harpists harping with their harps,
Basi, nikasikia sauti kutoka mbinguni, sauti iliyokuwa kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo kubwa. Sauti niliyosikia ilikuwa kama sauti ya wachezaji muziki wakipiga vinubi vyao.
3 and they sing, as it were, a new song before the throne, and before the four living creatures, and the elders, and no one was able to learn the song except the one hundred forty-four thousand who have been bought from the earth;
Walikuwa wanaimba wimbo mpya mbele ya kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe hai wanne na wale wazee. Hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao watu mia moja arobaini na nne elfu waliokombolewa duniani.
4 these are they who were not defiled with women, for they are virgin; these are they who are following the Lamb wherever He may go; these were bought from among men—a first-fruit to God and to the Lamb—
Watu hao ndio wale waliojiweka safi kwa kutoonana kimwili na wanawake, nao ni mabikira. Wao humfuata Mwanakondoo kokote aendako. Wamekombolewa kutoka miongoni mwa binadamu wengine, wakawa wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwanakondoo.
5 and in their mouth there was not found guile, for they are unblemished before the throne of God.
Hawakupata kamwe kuwa waongo; hawana hatia yoyote.
6 And I saw another messenger flying in midair, having continuous good news to proclaim to those dwelling on the earth, and to every nation, and tribe, and tongue, and people, (aiōnios g166)
Kisha nikamwona malaika mwingine anaruka juu angani akiwa na Habari Njema ya milele ya Mungu, aitangaze kwa watu wote waishio duniani, kwa mataifa yote, makabila yote, watu wa lugha zote na rangi zote. (aiōnios g166)
7 saying in a great voice, “Fear God, and give to Him glory, because the hour of His judgment came, and worship Him who made the sky, and the land, and sea, and fountains of waters.”
Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumtukuza! Maana saa imefika ya kutoa hukumu yake. Mwabuduni yeye aliyeumba mbingu na nchi, bahari na chemchemi za maji.”
8 And another messenger followed, saying, “Fallen, fallen is Babylon the great, because of the wine of the wrath of her whoredom she has given to all nations to drink.”
Malaika wa pili alimfuata huyo wa kwanza akisema, “Ameanguka! Naam, Babuloni mkuu ameanguka! Babuloni ambaye aliwapa mataifa yote wainywe divai yake—divai kali ya uzinzi wake!”
9 And a third messenger followed them, saying in a great voice, “If anyone worships the beast and his image, and receives a mark on his forehead or on his hand,
Na malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Yeyote anayemwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake juu ya paji la uso wake au juu ya mkono wake,
10 he also will drink of the wine of the wrath of God that has been mingled unmixed in the cup of His anger, and he will be tormented in fire and brimstone before the holy messengers, and before the Lamb,
yeye mwenyewe atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu, ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchanganywa na maji. Mtu huyo atateseka ndani ya moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele ya Mwanakondoo.
11 and the smoke of their torment goes up through ages of ages; and they have no rest day and night, who are worshiping the beast and his image, also if any receive the mark of his name. (aiōn g165)
Moshi wa moto unaowatesa kupanda juu milele na milele. Watu hao waliomwabudu huyo mnyama na sanamu yake, na kutiwa alama ya jina lake, hawatakuwa na nafuu yoyote usiku na mchana.” (aiōn g165)
12 Here is endurance of the holy ones; here [are] those keeping the commands of God, and the faith of Jesus.”
Kutokana na hayo, ni lazima watu wa Mungu, yaani watu wanaotii amri ya Mungu na kumwamini Yesu, wawe na uvumilivu.
13 And I heard a voice out of Heaven saying to me, “Write: Blessed are the dead who are dying in the LORD from this time!” “Yes,” says the Spirit, “That they may rest from their labors—and their works follow them!”
Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika! Heri watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa wameungana na Bwana.” Naye Roho asema, “Naam! Watapumzika kutoka taabu zao; maana matunda ya jasho lao yatawafuata.”
14 And I saw, and behold, a white cloud, and on the cloud [One] sitting like [a] Son of Man, having on His head a golden garland, and in His hand a sharp sickle;
Kisha nikatazama, na kumbe palikuwapo wingu jeupe hapo. Na juu ya wingu hilo kulikuwa na kiumbe kama mtu. Alikuwa amevaa taji ya dhahabu kichwani, na kushika mundu mkononi mwake.
15 and another messenger came forth out of the temple crying in a great voice to Him who is sitting on the cloud, “Send forth Your sickle and reap, because the hour of reaping has come to You, because the harvest of the earth has been ripe”;
Kisha malaika mwingine akatoka Hekaluni, na kwa sauti kubwa akamwambia yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu, “Tafadhali, tumia mundu wako ukavune mavuno, maana wakati wa mavuno umefika; mavuno ya dunia yameiva.”
16 and He who is sitting on the cloud put forth His sickle on the earth, and the earth was reaped.
Basi, yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu akautupa mundu wake duniani, na mavuno ya dunia yakavunwa.
17 And another messenger came forth out of the temple that [is] in Heaven, having—he also—a sharp sickle,
Kisha malaika mwingine akatoka katika Hekalu mbinguni akiwa na mundu wenye makali.
18 and another messenger came forth out from the altar, having authority over the fire, and he called with a great cry to him having the sharp sickle, saying, “Send forth your sharp sickle, and gather the clusters of the vine of the earth, because her grapes have come to perfection”;
Kisha malaika mwingine msimamizi wa moto, akatoka madhabahuni akamwambia kwa sauti kubwa yule malaika mwenye mundu wenye makali, “Nawe tia huo mundu wako mkali, ukakate vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva!”
19 and the messenger put forth his sickle to the earth, and gathered the vine of the earth, and cast [it] into the great winepress of the wrath of God;
Basi, malaika huyo akautupa mundu wake duniani, akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya chombo kikubwa cha kukamulia zabibu, chombo cha ghadhabu ya Mungu.
20 and the winepress was trodden outside of the city, and blood came forth out of the winepress—to the bridles of the horses, one thousand six hundred stadia.
Zabibu zikakamuliwa ndani ya hilo shinikizo lililoko nje ya mji, na damu ikatoka katika shinikizo hilo mtiririko mrefu kiasi cha mita mia tatu na kina chake kiasi cha mita mia mbili.

< Revelation 14 >