< Psalms 99 >

1 YHWH has reigned, peoples tremble, The Inhabitant of the cherubim, the earth shakes.
Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
2 YHWH [is] great in Zion, And He [is] high over all the peoples.
Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
3 They praise Your Name, “Great, and fearful, [it] is holy!”
Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
4 And the strength of the king Has loved judgment, You have established uprightness; Judgment and righteousness in Jacob, You have done.
Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
5 Exalt our God YHWH, And bow yourselves at His footstool, He [is] holy.
Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
6 Moses and Aaron among His priests, And Samuel among those proclaiming His Name. They are calling to YHWH, And He answers them.
Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
7 He speaks to them in a pillar of cloud, They have kept His testimonies, And He has given the statute to them.
Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
8 O YHWH, our God, You have afflicted them, You have been a forgiving God to them, And taking vengeance on their actions.
Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
9 Exalt our God YHWH, And bow yourselves at His holy hill, For our God YHWH [is] holy!
Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.

< Psalms 99 >