< Psalms 92 >
1 A PSALM. A SONG FOR THE SABBATH DAY. [It is] good to give thanks to YHWH, And to sing praises to Your Name, O Most High,
Zaburi. Wimbo wa siku ya Sabato. Ni vyema kumshukuru Bwana na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,
2 To declare Your kindness in the morning, And Your faithfulness in the nights.
kuutangaza upendo wako asubuhi, na uaminifu wako wakati wa usiku,
3 On ten strings and on stringed instrument, On (higgaion) with harp.
kwa zeze yenye nyuzi kumi na kwa sauti ya kinubi.
4 For You have caused me to rejoice, O YHWH, in Your work, I sing concerning the works of Your hands.
Ee Bwana, kwa kuwa matendo yako yamenifurahisha, nitaziimba kwa shangwe kazi za mikono yako.
5 How great Your works have been, O YHWH, Your thoughts have been very deep.
Ee Bwana, tazama jinsi yalivyo makuu matendo yako, tazama jinsi yalivyo ya kina mawazo yako!
6 A brutish man does not know, And a fool does not understand this—
Mjinga hafahamu, mpumbavu haelewi,
7 When the wicked flourish as an herb, And all workers of iniquity blossom—For their being destroyed forever and ever!
ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao mabaya wanastawi, wataangamizwa milele.
8 And You [are] high for all time, O YHWH.
Bali wewe, Ee Bwana, utatukuzwa milele.
9 For behold, Your enemies, O YHWH, For behold, Your enemies perish, All workers of iniquity separate themselves.
Ee Bwana, hakika adui zako, hakika adui zako wataangamia. Wote watendao mabaya watatawanyika.
10 And You exalt my horn as a wild ox, I have been anointed with fresh oil.
Umeitukuza pembe yangu kama ile ya nyati dume, mafuta mazuri yamemiminwa juu yangu.
11 And my eye looks on my enemies, Of those rising up against me, The evildoers, my ears hear.
Macho yangu yamewaona adui zangu wakishindwa, masikio yangu yamesikia maangamizi ya adui zangu waovu.
12 The righteous flourish as a palm-tree, He grows as a cedar in Lebanon.
Wenye haki watastawi kama mtende, watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni,
13 Those planted in the house of YHWH, In the courts of our God, flourish.
waliopandwa katika nyumba ya Bwana, watastawi katika nyua za Mungu wetu.
14 Still they bring forth in old age, They are fat and flourishing,
Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda, watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu,
15 To declare that YHWH my Rock [is] upright, And there is no perverseness in Him!
wakitangaza, “Bwana ni mkamilifu; yeye ni Mwamba wangu, na ndani yake hamna uovu.”