< Psalms 88 >

1 A SONG. A PSALM OF THE SONS OF KORAH. TO THE OVERSEER. [SET] ON “SICKNESS TO AFFLICT.” AN INSTRUCTION OF HEMAN THE EZRAHITE. O YHWH, God of my salvation, Daily I have cried, nightly before You,
Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
2 My prayer comes in before You, Incline Your ear to my loud cry,
Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
3 For my soul has been full of evils, And my life has come to Sheol. (Sheol h7585)
Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
4 I have been reckoned with those going down [to] the pit, I have been as a man without strength.
Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5 Among the dead—free, As pierced ones lying in the grave, Whom You have not remembered anymore, Indeed, they have been cut off by Your hand.
Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6 You have put me in the lowest pit, In dark places, in depths.
Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
7 Your fury has lain on me, And You have afflicted [with] all Your breakers. (Selah)
Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
8 You have put my acquaintance far from me, You have made me an abomination to them, Shut up—I do not go forth.
Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9 My eye has grieved because of affliction, I called You, O YHWH, all the day, I have spread out my hands to You.
Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
10 Do You do wonders to the dead? Does Rephaim rise? Do they thank You? (Selah)
Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
11 Is Your kindness recounted in the grave? Your faithfulness in destruction?
Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
12 Are Your wonders known in the darkness? And Your righteousness in the land of forgetfulness?
Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
13 And I, to You, O YHWH, I have cried, And in the morning my prayer comes before You.
Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
14 Why, O YHWH, do You cast off my soul? You hide Your face from me.
Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
15 I [am] afflicted, and expiring from youth, I have borne Your terrors—I pine away.
Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
16 Your wrath has passed over me, Your terrors have cut me off,
Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
17 They have surrounded me as waters all the day, They have gone around against me together,
Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
18 You have put lover and friend far from me, My acquaintance [is] the place of darkness!
Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.

< Psalms 88 >