< Psalms 45 >
1 TO THE OVERSEER. [SET] ON “LILIES.” AN INSTRUCTION OF THE SONS OF KORAH. A SONG OF LOVES. My heart has stirred a good word, I am telling my works to the King, My tongue [is] the pen of a speedy writer.
Moyo wangu unafurika kwa neno zuri; nitasoma kwa sauti maneno niliyo yaandika kuhusu mfalme; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mwenye ustadi.
2 You have been beautified above the sons of men, Grace has been poured into Your lips, Therefore God has blessed You for all time.
Wewe u mzuri sana kuliko mwanadamu yeyote; neema imemiminwa midomoni mwako; Kwa hiyo tunajua ya kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Gird Your sword on the thigh, O Mighty [One], Your splendor and Your majesty!
Weka upanga wako upande wako, wewe uliye mwenye nguvu, katika utukufu wako na enzi yako.
4 As for Your majesty—prosper [and] ride! Because of truth, meekness, [and] righteousness, And Your right hand shows You fearful things.
Katika enzi yako enenda katika ushindi kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki; mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.
5 Your arrows [are] sharp—Peoples fall under You—In the heart of the enemies of the King.
Mishale yako ni mkali; watu huanguka chini yako; mishale yako imo ndani ya mioyo ya adui za mfalme.
6 Your throne, O God, [is for] all time and forever, A scepter of uprightness [Is] the scepter of Your kingdom.
Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
7 You have loved righteousness and hate wickedness, Therefore God, Your God, has anointed You With oil of joy above Your companions.
Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
8 Myrrh, and aloes, [and] cassia [Cover] all Your garments; Out of palaces of ivory, Stringed instruments have made You glad.
Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
9 Daughters of kings [are] among Your precious ones, A queen has stood at Your right hand, In pure gold of Ophir.
Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
10 Listen, O daughter, and see, incline your ear, And forget your people, and your father’s house,
Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
11 And the King desires your beauty, Because He [is] your Lord—bow yourself to Him,
Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.
12 And the daughter of Tyre with a present, The rich of the people appease your face.
Binti wa Tiro atakuwepo akiwa na zawadi; matajiri kati wa watu watajipendekeza kwako.
13 All glory [is] the daughter of the king within, Her clothing [is] with filigrees of gold.
Binti mfalme katika jumba la kifahari ana utukufu wote; mavazi yake yametengenezwa kwa dhahabu.
14 In various colors she is brought to the King; Afterward, virgins, her companions, Are brought to You.
Naye ataongozwa kwa mfalme akiwa katika mavazi ya dhahabu; mabikra, wenzake wanoumfuata, wataletwa kwako mafalme.
15 They are brought with joy and gladness, They come into the palace of the King.
Wao wataongozwa kwa furaha na shangwe; wataingia mahali pa mfalme.
16 Instead of Your fathers are Your sons, You appoint them for princes in all the earth.
Katika mahali pa baba zako watoto wako watakuwepo, ambao wewe utawafanya kuwa wakuu katika nchi yote.
17 I make mention of Your Name in all generations, Therefore peoples praise You, For all time and forever!
Nami nitalifanya jina lako kukumbukwa katika uzao wote; kwa hiyo watu watakushukuru milele na milele.