< Psalms 44 >

1 TO THE OVERSEER. AN INSTRUCTION OF THE SONS OF KORAH. O God, we have heard with our ears, Our fathers have recounted to us, The work You worked in their days, In the days of old.
Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
2 You, [with] Your hand, have dispossessed nations. And You plant them. You afflict peoples, and send them away.
Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
3 For they did not possess the land by their sword, And their arm did not give salvation to them, But Your right hand, and Your arm, And the light of Your countenance, Because You had accepted them.
Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
4 You [are] He, my King, O God, Command the deliverances of Jacob.
Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
5 By You we push our adversaries, By Your Name we tread down our withstanders,
Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
6 For I do not trust in my bow, And my sword does not save me.
Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
7 For You have saved us from our adversaries, And You have put to shame those hating us.
Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
8 In God we have boasted all the day, And we thank Your Name for all time. (Selah)
Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
9 In anger You have cast off and cause us to blush, And do not go forth with our hosts.
Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10 You cause us to turn backward from an adversary, And those hating us, Have spoiled for themselves.
Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11 You make us food like sheep, And You have scattered us among nations.
Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12 You sell Your people—without wealth, And have not become great by their price.
Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13 You make us a reproach to our neighbors, A scorn and a reproach to our surrounders.
Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14 You make us an allegory among nations, A shaking of the head among peoples.
Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
15 All the day my confusion [is] before me, And the shame of my face has covered me.
Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16 Because of the voice of a reproacher and reviler, Because of an enemy and a self-avenger.
kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17 All this met us, and we did not forget You, Nor have we dealt falsely in Your covenant.
Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18 We do not turn our heart backward, Nor turn aside our step from Your path.
Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 But You have struck us in a place of dragons, And cover us over with death-shade.
Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20 If we have forgotten the Name of our God, And spread our hands to a strange God,
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21 Does God not search this out? For He knows the secrets of the heart.
Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
22 Surely, for Your sake we have been slain all the day, Reckoned as sheep of the slaughter.
Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
23 Stir up—why do You sleep, O Lord? Awake, do not cast us off forever.
Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
24 Why do You hide Your face? You forget our afflictions and our oppression,
Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25 For our soul has bowed to the dust, Our belly has cleaved to the earth.
Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
26 Arise, a help to us, And ransom us for your kindness’ sake.
Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.

< Psalms 44 >