< Psalms 146 >

1 Praise YAH! Praise, O my soul, YHWH.
Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
2 I praise YHWH during my life, I sing praise to my God while I exist.
Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
3 Do not trust in princes—in a son of man, For he has no deliverance.
Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
4 His spirit goes forth, he returns to his earth, In that day his thoughts have perished.
Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
5 O the blessedness of him Who has the God of Jacob for his help, His hope [is] on his God YHWH,
Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
6 Making the heavens and earth, The sea and all that [is] in them, Who is keeping truth for all time,
Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
7 Doing judgment for the oppressed, Giving bread to the hungry.
Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
8 YHWH is loosing the prisoners, YHWH is opening (the eyes of) the blind, YHWH is raising the bowed down, YHWH is loving the righteous,
Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
9 YHWH is preserving the strangers, He causes the fatherless and widow to stand, And He turns the way of the wicked upside down.
Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
10 YHWH reigns for all time, Your God, O Zion, to generation and generation, Praise YAH!
Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.

< Psalms 146 >