< Psalms 135 >

1 Praise YAH! Praise the Name of YHWH, Praise, you servants of YHWH,
Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
2 Who are standing in the house of YHWH, In the courts of the house of our God.
ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Praise YAH! For YHWH [is] good, Sing praise to His Name, for [it is] pleasant.
Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
4 For YAH has chosen Jacob for Himself, Israel for His peculiar treasure.
Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
5 For I have known that YHWH [is] great, Indeed, our Lord [is] above all gods.
Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
6 All that YHWH pleased He has done, In the heavens and in earth, In the seas and all deep places,
Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
7 Causing vapors to ascend from the end of the earth, He has made lightnings for the rain, Bringing forth wind from His treasures.
Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
8 Who struck the firstborn of Egypt, From man to beast.
Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
9 He sent tokens and wonders into your midst, O Egypt, On Pharaoh and on all his servants.
Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Who struck many nations, and slew strong kings,
Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
11 Even Sihon king of the Amorite, And Og king of Bashan, And all kingdoms of Canaan.
Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
12 And He gave their land an inheritance, An inheritance to His people Israel,
Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
13 O YHWH, Your Name [is] for all time, O YHWH, Your memorial from generation to generation.
Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
14 For YHWH judges His people, And comforts Himself for His servants.
Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
15 The idols of the nations [are] silver and gold, Work of the hands of man.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
16 They have a mouth, and they do not speak, They have eyes, and they do not see,
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
17 They have ears, and they do not give ear, Nose—there is no breath in their mouth!
zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
18 Their makers are like them, Everyone who is trusting in them.
Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
19 O house of Israel, bless YHWH, O house of Aaron, bless YHWH,
Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
20 O house of Levi, bless YHWH, Those fearing YHWH, bless YHWH.
Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
21 Blessed [is] YHWH from Zion, Inhabiting Jerusalem—praise YAH!
Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.

< Psalms 135 >