< Psalms 130 >
1 A SONG OF THE ASCENTS. I have called You from the depths, YHWH.
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 Lord, listen to my voice, Your ears are attentive to the voice of my supplications.
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
3 If You observe iniquities, Lord YAH, who stands?
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 But forgiveness [is] with You, that You may be feared.
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 I hoped [for] YHWH—my soul has hoped, And I have waited for His word.
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6 My soul [is] for the Lord, More than those watching for morning, Watching for morning!
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
7 Israel waits on YHWH, For kindness [is] with YHWH, And redemption [is] abundant with Him.
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8 And He redeems Israel from all his iniquities!
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.