< Psalms 115 >

1 Not to us, O YHWH, not to us, But to Your Name give glory, For Your kindness, for Your truth.
Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
2 Why do the nations say, “Where, pray, [is] their God?”
Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
3 And our God [is] in the heavens, All that He has pleased He has done.
Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
4 Their idols [are] silver and gold, work of man’s hands,
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
5 They have a mouth, and they do not speak, They have eyes, and they do not see,
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
6 They have ears, and they do not hear, They have a nose, and they do not smell,
zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
7 Their hands, but they do not handle, Their feet, and they do not walk;
Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
8 Nor do they mutter through their throat, Their makers are like them, Everyone who is trusting in them.
Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
9 O Israel, trust in YHWH, “He [is] their help and their shield.”
Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
10 O house of Aaron, trust in YHWH, “He [is] their help and their shield.”
Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
11 You fearing YHWH, trust in YHWH, “He [is] their help and their shield.”
Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
12 YHWH has remembered us, He blesses, He blesses the house of Israel, He blesses the house of Aaron,
Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
13 He blesses those fearing YHWH, The small with the great.
Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
14 YHWH adds to you—to you and to your sons.
Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
15 Blessed [are] you of YHWH, Maker of the heavens and earth,
Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
16 The heavens—the heavens [are] YHWH’s, And He has given the earth to sons of men;
Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
17 The dead do not praise YAH, Nor any going down to silence.
Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
18 And we, we bless YAH, From now on, and for all time. Praise YAH!
bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.

< Psalms 115 >