< Psalms 111 >

1 Praise YAH! [ALEPH-BET] I thank YHWH with the whole heart, In the secret meeting of the upright, And of the congregation.
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 Great [are] the works of YHWH, Sought out by all desiring them.
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 Splendid and majestic is His work, And His righteousness is standing forever.
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4 He has made a memorial of His wonders, YHWH [is] gracious and merciful.
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 He has given prey to those fearing Him, He remembers His covenant for all time.
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6 He has declared the power of His works to His people, To give to them the inheritance of nations.
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 The works of His hands [are] true and just, All His appointments [are] steadfast.
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 They are sustained forever and for all time. They are made in truth and uprightness.
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 He has sent redemption to His people, He has appointed His covenant for all time, His Name [is] holy and fearful.
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 The fear of YHWH [is] the beginning of wisdom, Good understanding have all doing them, His praise [is] standing forever!
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.

< Psalms 111 >