< Psalms 106 >
1 Praise YAH, give thanks to YHWH, for [He is] good, for His kindness [is] for all time!
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Who utters the mighty acts of YHWH? Sounds all His praise?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 O the blessedness of those keeping judgment, Doing righteousness at all times.
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Remember me, O YHWH, With the favor of Your people, Look after me in Your salvation.
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 To look on the good of Your chosen ones, To rejoice in the joy of Your nation, To boast myself with Your inheritance.
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 We have sinned with our fathers, We have done perversely, we have done wickedly.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Our fathers in Egypt, Have not considered wisely Your wonders, They have not remembered The abundance of Your kind acts, And provoke by the sea, at the Sea of Suph.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 And He saves them for His Name’s sake, To make His might known,
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 And rebukes the Sea of Suph, and it is dried up, And causes them to go Through depths as a wilderness.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 And He saves them from the hand Of him who is hating, And redeems them from the hand of the enemy.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 And waters cover their adversaries, One of them has not been left.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 And they believe in His words, they sing His praise,
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 They have hurried—forgotten His works, They have not waited for His counsel.
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 And they lust greatly in a wilderness, And try God in a desert.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 And He gives to them their request, And sends leanness into their soul.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 And they are envious of Moses in the camp, Of Aaron, YHWH’s holy one.
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 Earth opens, and swallows up Dathan, And covers over the company of Abiram.
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 And fire burns among their company, A flame sets the wicked on fire.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 They make a calf in Horeb, And bow themselves to a molten image,
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 And change their glory Into the form of an ox eating herbs.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 They have forgotten God their Savior, The doer of great things in Egypt,
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 Of wonderful things in the land of Ham, Of fearful things by the Sea of Suph.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 And He commands to destroy them, Unless Moses, His chosen one, Had stood in the breach before Him, To turn back His wrath from destroying.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 And they kick against the desirable land, They have not given credence to His word.
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 And they murmur in their tents, They have not listened to the voice of YHWH.
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 And He lifts up His hand to them, To cause them to fall in a wilderness,
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 And to cause their seed to fall among nations, And to scatter them through lands.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 And they are coupled to Ba‘al-Peor, And eat the sacrifices of the dead,
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 And they provoke to anger by their actions, And a plague breaks forth on them,
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 And Phinehas stands, and executes judgment, And the plague is restrained,
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 And it is reckoned to him for righteousness, From generation to generation—for all time.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 And they cause wrath by the waters of Meribah, And it is evil to Moses for their sakes,
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 For they have provoked his spirit, And he speaks wrongfully with his lips.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 They have not destroyed the peoples, As YHWH had commanded to them,
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 And mix themselves among nations, and learn their works,
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 And serve their idols, And they are for a snare to them.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 And they sacrifice their sons and their daughters to the demons,
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 And they shed innocent blood—Blood of their sons and of their daughters, Whom they have sacrificed to idols of Canaan, And the land is profaned with blood.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 And they are defiled with their works, And commit whoredom in their habitual doings.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 And the anger of YHWH Is kindled against His people, And He detests His inheritance.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 And gives them into the hand of nations, And those hating them rule over them,
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 And their enemies oppress them, And they are humbled under their hand.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 He delivers them many times, And they rebel in their counsel, And they are brought low in their iniquity.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 And He looks on their distress When He hears their cry,
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 And remembers His covenant for them, And is comforted, According to the abundance of His kindness.
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 And He appoints them for mercies Before all their captors.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Save us, O our God YHWH, and gather us from the nations, To give thanks to Your Holy Name, To glory in Your praise.
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Blessed [is] YHWH, God of Israel, From age until age. And all the people said, “Amen, praise YAH!”
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.