< Psalms 101 >
1 A PSALM OF DAVID. I sing kindness and judgment, To You, O YHWH, I sing praise.
Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
2 I act wisely in a perfect way, When do You come to me? I habitually walk in the integrity of my heart, In the midst of my house.
Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
3 I do not set a worthless thing before my eyes, I have hated the work of those turning aside, It does not adhere to me.
Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
4 A perverse heart turns aside from me, I do not know wickedness.
Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
5 Whoever slanders his neighbor in secret, Him I cut off, The high of eyes and proud of heart, Him I do not endure.
Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
6 My eyes are on the faithful of the land, To dwell with me, Whoever is walking in a perfect way, he serves me.
Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
7 He who is working deceit does not dwell in my house, Whoever is speaking lies is not established before my eyes.
Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
8 At morning I cut off all the wicked of the land, To cut off from the city of YHWH All the workers of iniquity!
Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.