< Proverbs 7 >

1 My son! Keep my sayings, And lay up my commands with you.
Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
2 Keep my commands, and live, And my law as the pupil of your eye.
Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
3 Bind them on your fingers, Write them on the tablet of your heart.
Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
4 Say to wisdom, “You [are] my sister.” And cry to understanding, “Relative!”
Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
5 To preserve you from a strange woman, From a stranger who has made her sayings smooth.
ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
6 For at a window of my house, I have looked out through my casement,
Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
7 And I see among the simple ones, I discern among the sons, A young man lacking understanding,
Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
8 Passing on in the street, near her corner, And the way [to] her house he steps,
Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
9 In the twilight—in the evening of day, In the darkness of night and blackness.
Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
10 And behold, a woman to meet him—(A harlot’s dress, and watchful of heart,
Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
11 She [is] noisy, and stubborn, her feet do not rest in her house.
Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
12 Now in an out-place, now in broad places, And she lies in wait near every corner)—
Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
13 And she laid hold on him and kissed him, She has hardened her face and says to him,
Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
14 “Sacrifices of peace-offerings [are] by me, Today I have completed my vows.
leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
15 Therefore I have come forth to meet you, To earnestly seek your face, and I find you.
hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
16 I decked my bed [with] ornamental coverings, Carved works—cotton of Egypt.
Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
17 I sprinkled my bed [with] myrrh, aloes, and cinnamon.
Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
18 Come, we are filled [with] love until the morning, We delight ourselves in loves.
Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
19 For the man is not in his house, He has gone on a long journey.
Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
20 He has taken a bag of money in his hand, At the day of the new moon he comes to his house.”
Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
21 She turns him aside with the abundance of her speech, She forces him with the flattery of her lips.
katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
22 He is going after her straight away, he comes as an ox to the slaughter, And as a chain to the discipline of a fool,
Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
23 Until an arrow splits his liver, As a bird has hurried to a snare, And has not known that it [is] for its life.
mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
24 And now, you sons, listen to me, And give attention to sayings of my mouth.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
25 Do not let your heart turn to her ways, Do not wander in her paths,
Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
26 For many [are] the wounded she caused to fall, And mighty [are] all her slain ones.
Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
27 The ways of Sheol—her house, Going down to inner chambers of death! (Sheol h7585)
Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)

< Proverbs 7 >