< Proverbs 6 >

1 My son! If you have been guarantor for your friend, Have struck your hand for a stranger,
Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
2 Have been snared with sayings of your mouth, Have been captured with sayings of your mouth,
basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
3 Do this now, my son, and be delivered, For you have come into the hand of your friend. Go, trample on yourself, and strengthen your friend,
Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
4 Do not give sleep to your eyes, And slumber to your eyelids,
Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
5 Be delivered as a roe from the hand, And as a bird from the hand of a fowler.
Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
6 Go to the ant, O slothful one, See her ways and be wise;
Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
7 Which has no captain, overseer, and ruler,
Hana akida, afisa au mtawala,
8 She prepares her bread in summer, She has gathered her food in harvest.
lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
9 Until when, O slothful one, do you lie? When do you arise from your sleep?
Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
10 A little sleep, a little slumber, A little clasping of the hands to rest,
Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
11 And your poverty has come as a traveler, And your want as an armed man.
ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
12 A man of worthlessness, a man of iniquity, Walking [with] perverseness of mouth,
Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
13 Winking with his eyes, speaking with his feet, Directing with his fingers,
akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
14 Contrariness [is] in his heart, devising evil at all times, He sends forth contentions.
Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
15 Therefore his calamity comes suddenly, He is broken instantly—and no healing.
Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
16 These six has YHWH hated, Indeed, seven [are] abominations to His soul:
Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
17 High eyes, False tongues, And hands shedding innocent blood,
Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
18 A heart devising thoughts of vanity, Feet hastening to run to evil,
moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
19 A false witness [who] breathes out lies, And one sending forth contentions between brothers.
shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
20 Keep, my son, the command of your father, And do not leave the law of your mother.
Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 Bind them on your heart continually, Tie them on your neck.
Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
22 In your going up and down, it leads you, In your lying down, it watches over you, And you have awoken—it talks [with] you.
utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
23 For the command [is] a lamp, And the Law a light, And a way of life [are] reproofs of instruction,
Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
24 To preserve you from an evil woman, From the flattery of the tongue of a strange woman.
Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
25 Do not desire her beauty in your heart, And do not let her take you with her eyelids.
Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
26 For a harlot consumes to a cake of bread, And an adulteress hunts the precious soul.
Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
27 Does a man take fire into his bosom, And are his garments not burned?
Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28 Does a man walk on the hot coals, And are his feet not scorched?
Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29 So [is] he who has gone in to the wife of his neighbor, None who touches her is innocent.
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30 They do not despise the thief, When he steals to fill his soul when he is hungry,
Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31 And being found he repays sevenfold, He gives all the substance of his house.
Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32 He who commits adultery [with] a woman lacks heart, He who does it is destroying his soul.
Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33 He finds a stroke and shame, And his reproach is not wiped away,
Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
34 For jealousy [is] the fury of a man, And he does not spare in a day of vengeance.
Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
35 He does not accept the appearance of any atonement, Indeed, he does not consent, Though you multiply bribes!
Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.

< Proverbs 6 >