< Numbers 3 >
1 And these [are] the generations of Aaron and Moses, in the day of YHWH’s speaking with Moses in Mount Sinai.
Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
2 And these [are] the names of the sons of Aaron: the firstborn Nadab, and Abihu, Eleazar, and Ithamar;
Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
3 these [are] the names of the sons of Aaron, the anointed priests, whose hand he has consecrated for acting as priest.
Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
4 And Nadab dies—Abihu also—before YHWH, in their bringing strange fire near before YHWH, in the wilderness of Sinai, and they did not have sons; and Eleazar—Ithamar also—acts as priest in the presence of their father Aaron.
Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
5 And YHWH speaks to Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
6 “Bring the tribe of Levi near, and you have caused it to stand before Aaron the priest, and they have served him,
“Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
7 and kept his charge, and the charge of all the congregation before the Tent of Meeting, to do the service of the Dwelling Place;
Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
8 and they have kept all the vessels of the Tent of Meeting, and the charge of the sons of Israel, to do the service of the Dwelling Place;
Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
9 and you have given the Levites to Aaron and to his sons; they are surely given to him out of the sons of Israel.
Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
10 And you appoint Aaron and his sons, and they have kept their priesthood, and the stranger who comes near is put to death.”
Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
11 And YHWH speaks to Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
12 “And I, behold, have taken the Levites from the midst of the sons of Israel instead of every firstborn opening a womb among the sons of Israel, and the Levites have been Mine;
“Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
13 for every firstborn [is] Mine, in the day of My striking every firstborn in the land of Egypt I have sanctified to Myself every firstborn in Israel, from man to beast; they are Mine; I [am] YHWH.”
kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
14 And YHWH speaks to Moses in the wilderness of Sinai, saying,
Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
15 “Number the sons of Levi by the house of their fathers, by their families; every male from a son of a month and upward—you number them.”
“Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
16 And Moses numbers them according to the command of YHWH, as he has been commanded.
Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
17 And these are the sons of Levi by their names: Gershon, and Kohath, and Merari.
Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
18 And these [are] the names of the sons of Gershon by their families: Libni and Shimei.
Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
19 And the sons of Kohath by their families: Amram, and Izhar, Hebron, and Uzziel.
Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
20 And the sons of Merari by their families: Mahli and Mushi; these are the families of the Levites, by the house of their fathers.
Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
21 Of Gershon—the family of the Libnite and the family of the Shimite; these are the families of the Gershonite.
Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
22 Their numbered ones, in number, every male from a son of a month and upward, their numbered ones [are] seven thousand and five hundred.
Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
23 The families of the Gershonite encamp westward behind the Dwelling Place.
Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
24 And the prince of a father’s house for the Gershonite [is] Eliasaph son of Lael.
Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
25 And the charge of the sons of Gershon in the Tent of Meeting [is] the Dwelling Place, and the tent, its covering, and the veil at the opening of the Tent of Meeting,
Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
26 and the hangings of the court, and the veil at the opening of the court, which [is] by the Dwelling Place and by the altar all around, and its cords, to all its service.
mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
27 And of Kohath—the family of the Amramite, and the family of the Izharite, and the family of the Hebronite, and the family of the Uzzielite; these are families of the Kohathite.
Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
28 In number, all the males, from a son of a month and upward, [are] eight thousand and six hundred, keeping the charge of the holy place.
Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
29 The families of the sons of Kohath encamp southward by the side of the Dwelling Place.
Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
30 And the prince of a father’s house for the families of the Kohathite [is] Elizaphan son of Uzziel.
Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
31 And their charge [is] the Ark, and the table, and the lampstand, and the altars, and the vessels of the holy place with which they serve, and the veil, and all its service.
Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
32 And Eleazar son of Aaron the priest [is] the prince of the princes of the Levites, [with] the oversight of the keepers of the charge of the holy place.
Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
33 Of Merari—the family of the Mahlite and the family of the Mushite; these [are] the families of Merari.
Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
34 And their numbered ones, in number, all the males from a son of a month and upward, [are] six thousand and two hundred.
Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
35 And the prince of a father’s house for the families of Merari [is] Zuriel son of Abihail; they encamp northward by the side of the Dwelling Place.
Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
36 And the oversight [and] charge of the sons of Merari [are] the boards of the Dwelling Place, and its bars, and its pillars, and its sockets, and all its vessels, and all its service,
Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
37 and the pillars of the court all around, and their sockets, and their pins, and their cords.
na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
38 And those encamping before the Dwelling Place eastward, before the Tent of Meeting, at the east, [are] Moses and Aaron, and his sons, keeping the charge of the sanctuary for the charge of the sons of Israel, and the stranger who comes near is put to death.
Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
39 All those numbered of the Levites whom Moses numbered—Aaron also—by the command of YHWH, by their families, every male from a son of a month and upward, [are] twenty-two thousand.
Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
40 And YHWH says to Moses, “Number every firstborn male of the sons of Israel from a son of a month and upward, and take up the number of their names;
Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
41 and you have taken the Levites for Me (I [am] YHWH), instead of every firstborn among the sons of Israel, and the livestock of the Levites instead of every firstling among the livestock of the sons of Israel.”
Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
42 And Moses numbers, as YHWH has commanded him, all the firstborn among the sons of Israel.
Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
43 And every firstborn male, by the number of names, from a son of a month and upward, of their numbered ones, are twenty-two thousand two hundred and seventy-three.
Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
44 And YHWH speaks to Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
45 “Take the Levites instead of every firstborn among the sons of Israel, and the livestock of the Levites instead of their livestock; and the Levites have been Mine; I [am] YHWH.
“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
46 And [from] those ransomed of the two hundred and seventy-three of the firstborn of the sons of Israel, who are more than the Levites,
Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
47 you have even taken five shekels apiece by the counted head—you take by the shekel of the holy place; the shekel [is] twenty gerahs;
kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
48 and you have given the money to Aaron and to his sons, whereby those over and above are ransomed.”
Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
49 And Moses takes the ransom money from those over and above those ransomed by the Levites;
Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
50 he has taken the money from the firstborn of the sons of Israel—one thousand and three hundred and sixty-five, by the shekel of the holy place;
Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
51 and Moses gives the money of those ransomed to Aaron and to his sons, according to the command of YHWH, as YHWH has commanded Moses.
Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.