< Numbers 28 >

1 And YHWH speaks to Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 “Command the sons of Israel, and you have said to them: My offering, My bread for My fire-offerings, My refreshing fragrance, you take heed to bring near to Me in its appointed time.
“Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
3 And you have said to them: This [is] the fire-offering which you bring near to YHWH: two lambs, sons of a year, perfect ones, daily, [for] a continual burnt-offering;
Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
4 you prepare the first lamb in the morning, and you prepare the second lamb between the evenings;
Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
5 and a tenth of the ephah of flour for a present mixed with a fourth of the hin of beaten oil;
kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
6 [it is] a continual burnt-offering, which was made in Mount Sinai for refreshing fragrance, [for] a fire-offering to YHWH.
Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
7 And its drink-offering [is] a fourth of the hin for one lamb; pour out a drink-offering of strong drink to YHWH in the holy place.
Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
8 And you prepare the second lamb between the evenings; as the present of the morning and as its drink-offering, you prepare [it as] a fire-offering of refreshing fragrance to YHWH.
Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
9 And on the Sabbath day, two lambs, sons of a year, perfect ones, and two-tenth parts of flour, a present mixed with oil, and its drink-offering—
“‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
10 the burnt-offering of the Sabbath in its Sabbath, besides the continual burnt-offering and its drink-offering.
Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
11 And in the beginnings of your months you bring a burnt-offering near to YHWH: two bullocks, sons of the herd, and one ram, seven lambs, sons of a year, perfect ones;
“‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
12 and three-tenth parts of flour, a present mixed with oil, for one bullock, and two-tenth parts of flour, a present mixed with oil, for one ram;
Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
13 and a tenth—a tenth part of flour, a present mixed with oil, for one lamb, [for] a burnt-offering, a refreshing fragrance, a fire-offering to YHWH;
pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
14 and their drink-offerings are a half of the hin for a bullock, and a third of the hin for a ram, and a fourth of the hin for a lamb, of wine; this [is] the burnt-offering of every month for the months of the year.
Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
15 And one kid of the goats is prepared for a sin-offering to YHWH, besides the continual burnt-offering and its drink-offering.
Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
16 And in the first month, on the fourteenth day of the month, [is] the Passover to YHWH;
“‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
17 and in the fifteenth day of this month [is] a festival; [for] seven days unleavened bread is eaten.
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
18 In the first day [is] a holy convocation; you do no servile work;
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
19 and you have brought a fire-offering near, a burnt-offering to YHWH: two bullocks, sons of the herd, and one ram, and seven lambs, sons of a year, they are perfect ones for you;
Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
20 and their present of flour mixed with oil—you prepare three-tenth parts for a bullock and two-tenth parts for a ram;
Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
21 you prepare a tenth—a tenth part for one lamb, for the seven lambs,
pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
22 and one goat [for] a sin-offering, to make atonement for you.
Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
23 Apart from the burnt-offering of the morning, which [is] for the continual burnt-offering, you prepare these;
Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
24 like these you prepare bread of a fire-offering daily [for] seven days, a refreshing fragrance to YHWH; it is prepared besides the continual burnt-offering and its drink-offering.
Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
25 And on the seventh day you have a holy convocation; you do no servile work.
Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
26 And on the day of the first-fruits, in your bringing a new present near to YHWH, in your weeks, you have a holy convocation; you do no servile work.
“‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
27 And you have brought a burnt-offering near for refreshing fragrance to YHWH: two bullocks, sons of the herd, one ram, seven lambs, sons of a year,
Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
28 and their present, flour mixed with oil, three-tenth parts for one bullock, two-tenth parts for one ram,
Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
29 a tenth—a tenth part for one lamb, for the seven lambs;
na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
30 one kid of the goats to make atonement for you;
Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
31 apart from the continual burnt-offering and its present, you prepare [them] and their drink-offerings; they are perfect ones for you.”
Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.

< Numbers 28 >