< Numbers 12 >
1 And Miriam speaks—Aaron also—against Moses concerning the circumstance of the Cushite woman whom he had taken, for he had taken a Cushite woman;
Miriamu na Aroni walianza kuzungumza dhidi ya Mose kwa sababu ya mke wake Mkushi, kwa kuwa alikuwa ameoa Mkushi.
2 and they say, “Has YHWH only spoken by Moses? Has he not also spoken by us?” And YHWH hears.
Waliuliza, “Je, Bwana amesema kupitia Mose peke yake? Je, hajasema kutupitia sisi pia?” Naye Bwana akasikia hili.
3 And the man Moses [is] very humble, more than any of the men who [are] on the face of the ground.
(Basi Mose alikuwa mtu mnyenyekevu sana, mnyenyekevu kuliko mtu mwingine yeyote katika uso wa dunia.)
4 And YHWH suddenly says to Moses, and to Aaron, and to Miriam, “Come out, you three, to the Tent of Meeting”; and those three come out.
Ghafula Bwana akawaambia Mose, Aroni na Miriamu, “Njooni katika Hema la Kukutania, ninyi nyote watatu.” Kwa hiyo wote watatu wakaenda.
5 And YHWH comes down in the pillar of the cloud, and stands at the opening of the tent, and calls Aaron and Miriam, and both of them come out.
Kisha Bwana akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye ingilio la Hema, akawaita Aroni na Miriamu. Wakati wote wawili waliposogea mbele,
6 And He says, “Now hear My words: If your prophet is of YHWH, I make Myself known to him in a vision; I speak with him in a dream.
Bwana akasema, “Sikilizeni maneno yangu: “Akiwapo nabii wa Bwana miongoni mwenu, nitajifunua kwake kwa maono, nitanena naye katika ndoto.
7 Not so My servant Moses; He [is] steadfast in all My house.
Lakini sivyo kwa mtumishi wangu Mose; yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote.
8 I speak with him mouth to mouth, Even [by] an appearance, and not in riddles; And he beholds the form of YHWH attentively. Now why have you not been afraid To speak against My servant—against Moses?”
Kwake nitanena naye uso kwa uso, waziwazi wala si kwa mafumbo; yeye ataona umbo la Bwana. Kwa nini basi ninyi hamkuogopa kuzungumza kinyume cha mtumishi wangu Mose?”
9 And the anger of YHWH burns against them, and He goes on,
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao, akawaacha.
10 and the cloud has turned aside from off the tent, and behold, Miriam [is] leprous as snow; and Aaron turns to Miriam, and behold, leprous!
Wakati hilo wingu liliinuka kutoka juu ya Hema, Miriamu akawa tayari ana ukoma, mweupe kama theluji. Aroni akamgeukia, akaona ana ukoma.
11 And Aaron says to Moses, “O my lord, please do not lay [this] sin on us [in] which we have been foolish, and [in] which we have sinned;
Kisha Aroni akamwambia Mose, “Tafadhali, bwana wangu, usituhesabie dhambi hii ambayo tumeifanya kwa upumbavu.
12 please do not let her be as [one] dead, when in his coming out from the womb of his mother—the half of his flesh is consumed.”
Usimwache awe kama mtoto mchanga aliyezaliwa akiwa mfu, ambaye nusu ya mwili wake imeharibika hapo atokapo katika tumbo la mama yake.”
13 And Moses cries to YHWH, saying, “O God, please give healing to her! Please!”
Hivyo Mose akamlilia Bwana akisema, “Ee Mungu, nakuomba umponye!”
14 And YHWH says to Moses, “But [if] her father had but spat in her face—is she not ashamed [for] seven days? She is shut out [for] seven days at the outside of the camp, and afterward she is gathered.”
Bwana akamjibu Mose, “Je, kama baba yake angemtemea usoni, asingeona aibu kwa siku saba? Mfungie nje ya kambi kwa siku saba; baada ya hapo anaweza kurudishwa kambini.”
15 And Miriam is shut out at the outside of the camp [for] seven days, and the people have not journeyed until Miriam is gathered;
Kwa hiyo Miriamu akafungiwa nje ya kambi kwa siku saba, nao watu hawakuendelea na safari mpaka aliporudishwa kambini.
16 and afterward the people have journeyed from Hazeroth, and they encamp in the wilderness of Paran.
Baada ya hayo, watu waliondoka Haserothi, wakapiga kambi katika Jangwa la Parani.