< Nehemiah 7 >

1 And it comes to pass, when the wall has been built, that I set up the doors, and the gatekeepers are appointed, and the singers, and the Levites,
Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
2 and I charge my brother Hanani, and Hananiah head of the palace, concerning Jerusalem—for he [is] as a man of truth, and fearing God above many—
Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
3 and I say to them, “Do not let the gates of Jerusalem be opened until the heat of the sun, and while they are standing by let them shut the doors, and fasten, and appoint guards of the inhabitants of Jerusalem, each at his watch, and each in front of his house.”
Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
4 And the city [is] broad on both sides, and great, and the people [are] few in its midst, and there are no houses built;
Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
5 and my God puts it to my heart, and I gather the nobles, and the prefects, and the people, for the genealogy, and I find a scroll of the genealogy of those coming up at the beginning, and I find written in it:
Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
6 These [are] sons of the province, those coming up of the captives of the expulsion that Nebuchadnezzar king of Babylon removed—and they return to Jerusalem and to Judah, each to his city—
Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
7 who are coming in with Zerubbabel, Jeshua, Nehemiah, Azariah, Raamiah, Nahamani, Mordecai, Bilshan, Mispereth, Bigvai, Nehum, Baanah. The number of the men of the people of Israel:
wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
8 sons of Parosh, two thousand one hundred and seventy-two;
wazao wa Paroshi 2,172
9 sons of Shephatiah, three hundred seventy-two;
wazao wa Shefatia 372
10 sons of Arah, six hundred fifty-two;
wazao wa Ara 652
11 sons of Pahath-Moab, of the sons of Jeshua and Joab, two thousand and eight hundred [and] eighteen;
wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
12 sons of Elam, one thousand two hundred fifty-four;
wazao wa Elamu 1,254
13 sons of Zattu, eight hundred forty-five;
wazao wa Zatu 845
14 sons of Zaccai, seven hundred and sixty;
wazao wa Zakai 760
15 sons of Binnui, six hundred forty-eight;
wazao wa Binui 648
16 sons of Bebai, six hundred twenty-eight;
wazao wa Bebai 628
17 sons of Azgad, two thousand three hundred twenty-two;
wazao wa Azgadi 2,322
18 sons of Adonikam, six hundred sixty-seven;
wazao wa Adonikamu 667
19 sons of Bigvai, two thousand sixty-seven;
wazao wa Bigwai 2,067
20 sons of Adin, six hundred fifty-five;
wazao wa Adini 655
21 sons of Ater of Hezekiah, ninety-eight;
wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
22 sons of Hashum, three hundred twenty-eight;
wazao wa Hashumu 328
23 sons of Bezai, three hundred twenty-four;
wazao wa Besai 324
24 sons of Hariph, one hundred [and] twelve;
wazao wa Harifu 112
25 sons of Gibeon, ninety-five;
wazao wa Gibeoni 95
26 men of Beth-Lehem and Netophah, one hundred eighty-eight;
watu wa Bethlehemu na Netofa 188
27 men of Anathoth, one hundred twenty-eight;
watu wa Anathothi 128
28 men of Beth-Azmaveth, forty-two;
watu wa Beth-Azmawethi 42
29 men of Kirjath-Jearim, Chephirah, and Beeroth, seven hundred forty-three;
watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
30 men of Ramah and Gaba, six hundred twenty-one;
watu wa Rama na Geba 621
31 men of Michmas, one hundred and twenty-two;
watu wa Mikmashi 122
32 men of Bethel and Ai, one hundred twenty-three;
watu wa Betheli na Ai 123
33 men of the other Nebo, fifty-two;
watu wa Nebo 52
34 sons of the other Elam, one thousand two hundred fifty-four;
wazao wa Elamu 1,254
35 sons of Harim, three hundred and twenty;
wazao wa Harimu 320
36 sons of Jericho, three hundred forty-five;
wazao wa Yeriko 345
37 sons of Lod, Hadid, and Ono, seven hundred and twenty-one;
wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
38 sons of Senaah, three thousand nine hundred and thirty.
wazao wa Senaa 3,930
39 The priests: sons of Jedaiah, of the house of Jeshua, nine hundred seventy-three;
Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
40 sons of Immer, one thousand fifty-two;
wazao wa Imeri 1,052
41 sons of Pashur, one thousand two hundred forty-seven;
wazao wa Pashuri 1,247
42 sons of Harim, one thousand and seventeen.
wazao wa Harimu 1,017
43 The Levites: sons of Jeshua, of Kadmiel, of sons of Hodevah, seventy-four.
Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
44 The singers: sons of Asaph, one hundred forty-eight.
Waimbaji: wazao wa Asafu 148
45 The gatekeepers: sons of Shallum, sons of Ater, sons of Talmon, sons of Akkub, sons of Hatita, sons of Shobai: one hundred thirty-eight.
Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
46 The Nethinim: sons of Ziha, sons of Hasupha, sons of Tabbaoth,
Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
47 sons of Keros, sons of Sia, sons of Padon,
wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
48 sons of Lebanah, sons of Hagaba, sons of Shalmai,
wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
49 sons of Hanan, sons of Giddel, sons of Gahar,
wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
50 sons of Reaiah, sons of Rezin, sons of Nekoda,
wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
51 sons of Gazzam, sons of Uzza, sons of Phaseah,
wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
52 sons of Bezai, sons of Meunim, sons of Nephishesim,
wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
53 sons of Bakbuk, sons of Hakupha, sons of Harhur,
wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
54 sons of Bazlith, sons of Mehida, sons of Harsha,
wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
55 sons of Barkos, sons of Sisera, sons of Tamah,
wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
56 sons of Neziah, sons of Hatipha.
wazao wa Nesia na Hatifa.
57 Sons of the servants of Solomon: sons of Sotai, sons of Sophereth, sons of Perida,
Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
58 sons of Jaala, sons of Darkon, sons of Giddel,
wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
59 sons of Shephatiah, sons of Hattil, sons of Pochereth of Zebaim, sons of Amon.
wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
60 All the Nethinim and the sons of the servants of Solomon [are] three hundred ninety-two.
Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
61 And these [are] those coming up from Tel-Melah, Tel-Harsha, Cherub, Addon, and Immer—and they have not been able to declare the house of their fathers, and their seed, whether they [are] of Israel—
Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
62 sons of Delaiah, sons of Tobiah, sons of Nekoda, six hundred forty-two.
wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
63 And of the priests: sons of Habaiah, sons of Koz, sons of Barzillai (who has taken a wife from the daughters of Barzillai the Gileadite, and is called by their name).
Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
64 These have sought their register among those reckoning themselves by genealogy, and it has not been found, and they are redeemed from the priesthood,
Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
65 and the Tirshatha says to them that they do not eat of the most holy things until the standing up of the priest with [the] Lights and Perfections.
Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
66 All the assembly together [is] forty-two thousand three hundred and sixty,
Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
67 apart from their servants and their handmaids—these [are] seven thousand three hundred thirty-seven; and of them [are] male and female singers, two hundred forty-five.
tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
68 Their horses [are] seven hundred thirty-six; their mules, two hundred [and] forty-five;
Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
69 camels, four hundred thirty-five; donkeys, six thousand seven hundred and twenty.
ngamia 435 na punda 6,720.
70 And from the extremity of the heads of the fathers they have given to the work; the Tirshatha has given to the treasure, one thousand drams of gold, fifty bowls, five hundred and thirty priests’ coats.
Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
71 And of the heads of the fathers they have given to the treasure of the work, twenty thousand drams of gold, and two thousand and two hundred pounds of silver.
Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
72 And that which the rest of the people have given [is] twenty thousand drams of gold, and two thousand pounds of silver, and sixty-seven priests’ coats.
Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
73 And they dwell—the priests, and the Levites, and the gatekeepers, and the singers, and [some] of the people, and the Nethinim, and all Israel—in their cities, and the seventh month comes, and the sons of Israel [are] in their cities.
Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,

< Nehemiah 7 >