< Micah 5 >
1 Now gather yourself together, O daughter of troops, He has laid a siege against us, They strike [the] judge of Israel on the cheek with a rod.
Sasa njoni pamoja katika safu ya kupigana, binti wa maaskari; maaskari wameuzingira mji, kwa ufito watampiga mwamuzi wa Israeli kwenye shavu.
2 “And you, Beth-Lehem Ephratah, Little to be among the chiefs of Judah! From you He comes forth to Me—to be ruler in Israel, And His comings forth [are] of old, From the days of antiquity.”
Lakini wewe, Bethlehemu Efrata, hata kama uko mdogo miongoni mwa koo za Yuda, kutoka kweko mmoja atakuja kwangu kutawala Israeli, ambaye mwanzo wake ni kutoka nyakati za kale, toka milele.
3 Therefore He gives them up until the time she who brings forth has brought forth, And the remnant of His brothers return to the sons of Israel.
Kwa hiyo Mungu atawapa, hata mda wa yeye aliye katika uchungu kuzaa mtoto, na mabaki ya ndugu zake yatawarudia wana wa Israeli.
4 And He has stood and delighted in the strength of YHWH, In the excellence of the Name of His God YHWH, And they have remained, For now He is great to the ends of the earth.
Atasimama na kuchunga kundi lake kwa nguvu za Yahwe, kwa ukuu wa enzi ya jina la Yahwe Mungu wake. Watabaki, kwa kuwa atakuwa mashuhuri hata mwisho wa dunia.
5 And this [One] has been peace. Asshur, when he comes into our land, And when he treads in our palaces, We have raised against him seven shepherds, And eight anointed of man.
Atakuwa amani yetu. Wakati Waashuru watakapokuja kwenye nchi yetu, wakati wakitembea dhidi ya boma yetu, kisha kisha tutainuka juu yao wachungaji saba na viongozi nane juu ya watu.
6 And they have afflicted the land of Asshur with the sword, And the land of Nimrod at its openings, And He has delivered from Asshur when he comes into our land, And when he treads in our borders.
Watachunga nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake. Atatuokoa kutoka kwa Waashuru, watakapokuja kwenye nchi yetu, watakapoingia kwenye mipaka yetu.
7 And the remnant of Jacob has been in the midst of many peoples, As dew from YHWH—as showers on the herb, That does not wait for man, nor stays for the sons of men.
Mabaki ya Yakobo yatakuwa katika kabila za watu wengi, kama umande utokao kwa Yahwe, kama manyunyu kwenye majani, ambayo hayamsubiri mtu, na hayawasubiri watoto wa mwanadamu.
8 Indeed, the remnant of Jacob has been among nations, In the midst of many peoples, As a lion among beasts of a forest, As a young lion among ranks of a flock, Which if it has passed through, Has both trodden down and has torn, And there is no deliverer.
Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa, miongoni mwa watu wengi, kama simba katikati ya kundi la kondoo. wakati akipita katikati yao, atawakanyaga juu yao na kuwachachana kuwa vipande vipande, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
9 High is your hand above your adversaries, And all your enemies are cut off.
Mkono wako utainuliwa dhidi ya maadui zako, na utawaharibu.
10 “And it has come to pass in that day,” A declaration of YHWH, “I have cut off your horses from your midst, And I have destroyed your chariots,
“Itatokea siku hiyo,” asema Yahwe, “kwamba nitawaharibu farasi wako kutoka miongoni mwenu na nitayavunja magari yako ya farasi.
11 And I have cut off the cities of your land, And I have thrown down all your fortresses,
Nitaiharibu miji katika nchi yako na kuzingusha ngome zako zote.
12 And have cut off sorcerers out of your hand, And observers of clouds—you have none.
Nitauharibu uchawi kwenye mkono wako, na hakutakuwa na waaguzi tena.
13 And I have cut off your carved images, And your standing-pillars out of your midst, And you do not bow yourself anymore To the work of your hands.
Nitaziaharibu sanamu zako za pango na nguzo za mawe kutoka miongoni mwako. Hautaabudu tena ustadi wa mikono yako.
14 And I have plucked up your Asherim out of your midst, And I have destroyed your enemies.
Nitazin'goa nguzo zako za Ashera kutoka miongoni mwenu, na nitaiharibu miji yenu.
15 And I have done vengeance in anger and in fury, With the nations who have not listened!”
Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu juu ya mataifa ambayo hayakusikiliza.”