< Matthew 6 >

1 “Take heed not to do your kindness before men, to be seen by them, and if not—you have no reward from your Father who [is] in the heavens;
“Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo.
2 whenever, therefore, you may do kindness, you may not sound a trumpet before you as the hypocrites do, in the synagogues, and in the streets, that they may have glory from men; truly I say to you, they have their reward!
“Basi, unapomsaidia maskini, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masunagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
3 But you, doing kindness, do not let your left hand know what your right hand does,
Lakini wewe unapomsaidia maskini, fanya hivyo kwamba hata rafiki yako asijue ufanyalo.
4 that your kindness may be in secret, and your Father who is seeing in secret will reward you Himself.
Toa msaada wako kwa siri, na Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
5 And when you may pray, you will not be as the hypocrites, because they cherish to pray standing in the synagogues and in the corners of the broad places, that they may be seen of men; truly I say to you that they have their reward.
“Mnaposali, msifanye kama wanafiki. Wao hupenda kusimama na kusali katika masunagogi na katika pembe za njia ili watu wawaone. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
6 But you, when you may pray, go into your chamber, and having shut your door, pray to your Father who [is] in secret, and your Father who is seeing in secret will reward you.
Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango, kisha umwombe Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
7 And—praying—you may not use vain repetitions like the nations, for they think that in their speaking much they will be heard,
“Mnaposali, msipayuke maneno kama watu wasiomjua Mungu. Wao hudhani kwamba Mungu atawasikiliza ati kwa sababu ya maneno mengi.
8 therefore do not be like them, for your Father knows those things that you have need of before your asking Him;
Msiwe kama wao. Baba yenu anajua mnayoyahitaji hata kabla ya kumwomba.
9 therefore pray thus: Our Father who [is] in the heavens, hallowed be Your Name.
Basi, hivi ndivyo mnavyopaswa kusali: Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe.
10 Your kingdom come, Your will come to pass, as in Heaven also on the earth.
Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
11 Give us today our appointed bread.
Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.
12 And forgive us our debts, as we also forgive our debtors.
Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
13 And may You not lead us into temptation, but deliver us from the evil [one], because Yours is the kingdom, and the power, and the glory—for all ages. Amen.
Usitutie katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. is Baadhi ya makala za zamani zina; Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.
14 For if you may forgive men their trespasses He also will forgive you—your Father who [is] in the heavens;
“Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
15 but if you may not forgive men their trespasses, neither will your Father forgive your trespasses.
Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
16 And when you may fast, do not be as the hypocrites, of sour countenances, for they disfigure their faces, that they may appear to men fasting; truly I say to you that they have their reward.
“Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki. Wao hukunja nyuso zao wapate kuonekana na watu kuwa wanafunga. Nawaambieni hakika, hao wamekwisha pata tuzo lao.
17 But you, fasting, anoint your head, and wash your face,
Wewe lakini unapofunga, paka kichwa chako mafuta, nawa uso wako,
18 that you may not appear to men fasting, but to your Father who [is] in secret, and your Father, who is seeing in secret, will reward you.
ili mtu yeyote asijue kwamba unafunga, ila ujulikane tu kwa Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika atakutuza.
19 Do not treasure up to yourselves treasures on the earth, where moth and rust disfigure, and where thieves break through and steal,
“Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba.
20 but treasure up to yourselves treasures in Heaven, where neither moth nor rust disfigure, and where thieves do not break through nor steal,
Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba.
21 for where your treasure is, there will your heart be also.
Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
22 The lamp of the body is the eye, if, therefore, your eye may be perfect, all your body will be enlightened,
“Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni zima, mwili wako wote utakuwa katika mwanga.
23 but if your eye may be evil, all your body will be dark; if, therefore, the light that [is] in you is darkness—the darkness, how great!
Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote utakuwa katika giza. Basi, ikiwa mwanga ulioko ndani yako ni giza, basi, hilo ni giza la kutisha mno.
24 None is able to serve two lords, for either he will hate the one and love the other, or he will hold to the one, and despise the other; you are not able to serve God and wealth.
“Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.
25 Because of this I say to you, do not be anxious for your life, what you may eat, and what you may drink, nor for your body, what you may put on. Is not life more than nourishment, and the body than clothing?
“Ndiyo maana nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula na kinywaji mnavyohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu. Je, maisha ni chakula tu au zaidi? Na mwili, je, si zaidi ya mavazi?
26 Look to the birds of the sky, for they do not sow, nor reap, nor gather into storehouses, and your heavenly Father nourishes them; are you not much better than they?
Waangalieni ndege wa mwituni: hawapandi, hawavuni, wala hawana ghala yoyoye. Hata hivyo, Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani kuliko hao?
27 And who of you, being anxious, is able to add to his age one cubit?
Ni nani miongoni mwenu kwa kuwa na wasiwasi sana anaweza kuuongeza muda wa maisha yake?
28 And why are you anxious about clothing? Consider well the lilies of the field; how do they grow? They do not labor, nor do they spin;
“Na kuhusu mavazi, ya nini kuwa na wasiwasi? Tazameni maua ya porini jinsi yanavyostawi. Hayafanyi kazi wala hayasokoti.
29 and I say to you that not even Solomon in all his glory was clothed as one of these.
Lakini nawaambieni, hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
30 And if the herb of the field, that today is, and tomorrow is cast into the furnace, God so clothes—not much more you, O you of little faith?
Ikiwa basi Mungu hulivika hivyo jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatafanya zaidi kwenu ninyi? Enyi watu wenye imani haba!
31 Therefore you may not be anxious, saying, What may we eat? Or, What may we drink? Or, [With] what may we be clothed?
“Basi, msiwe na wasiwasi: Tutakula nini, tutakunywa nini, tutavaa nini!
32 For the nations seek for all these, for your heavenly Father knows that you have need of all these;
Maana hayo yote yanahangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote.
33 but seek first the Kingdom of God and His righteousness, and all these will be added to you.
Bali, zingatieni kwanza Ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo mengine yote mtapewa kwa ziada.
34 Therefore do not be anxious for tomorrow, for tomorrow will be anxious for its own things; sufficient for the day [is] the evil of it.”
Basi, msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho inayo yake. Matatizo ya siku moja yanawatosheni kwa siku hiyo.

< Matthew 6 >