< Matthew 26 >
1 And it came to pass, when Jesus finished all these words, He said to His disciples,
Yesu alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,
2 “You have known that after two days the Passover comes, and the Son of Man is delivered up to be crucified.”
“Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”
3 Then were gathered together the chief priests, and the scribes, and the elders of the people, into the court of the chief priest who was called Caiaphas;
Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.
4 and they consulted together that they might take Jesus by guile, and kill [Him],
Wakafanya shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
5 and they said, “Not in the celebration, that there may not be a tumult among the people.”
Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”
6 And Jesus having been in Bethany, in the house of Simon the leper,
Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
7 there came to Him a woman having an alabaster box of ointment, very precious, and she poured on His head as He is reclining.
naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
8 And having seen [it], His disciples were much displeased, saying, “To what purpose [is] this waste?
Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
9 For this ointment could have been sold for much, and given to the poor.”
Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
10 And Jesus having known, said to them, “Why do you give trouble to the woman? For a good work she worked for Me;
Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
11 for you always have the poor with you, and you do not always have Me;
Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
12 for she having put this ointment on My body—for My burial she did [it].
Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
13 Truly I say to you, wherever this good news may be proclaimed in the whole world, what this [one] did will also be spoken of—for a memorial of her.”
Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
14 Then one of the Twelve, who is called Judas Iscariot, having gone to the chief priests, said,
Kisha mmojawapo wa wale kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa viongozi wa makuhani
15 “What are you willing to give me, and I will deliver Him up to you?” And they weighed out to him thirty pieces of silver,
na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.
16 and from that time he was seeking a convenient season to deliver Him up.
Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu.
17 And on the first [day] of the Unleavened [Bread] the disciples came near to Jesus, saying to Him, “Where will You [that] we may prepare for You to eat the Passover?”
Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimjia Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
18 And He said, “Go away into the city, to such a one, and say to him, The Teacher says, My time is near; near you I keep the Passover with My disciples”;
Akajibu, “Nendeni kwa mtu fulani huko mjini, mkamwambie, ‘Mwalimu asema hivi: Saa yangu imekaribia. Nitaiadhimisha Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.’”
19 and the disciples did as Jesus appointed them, and prepared the Passover.
Hivyo wanafunzi wakafanya kama vile Yesu alivyokuwa amewaelekeza, nao wakaandaa Pasaka.
20 And evening having come, He was reclining with the Twelve,
Ilipofika jioni, Yesu alikuwa ameketi mezani pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
21 and while they are eating, He said, “Truly I say to you that one of you will deliver Me up.”
Nao walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
22 And being grieved exceedingly, they began to say to Him, each of them, “Is it I, Lord?”
Wakahuzunika sana, wakaanza kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
23 And He answering said, “He who dipped with Me the hand in the dish, he will deliver Me up;
Yesu akawaambia, “Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami ndiye atakayenisaliti.
24 the Son of Man indeed goes, as it has been written concerning Him, but woe to that man through whom the Son of Man is delivered up! It were good for him if that man had not been born.”
Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu. Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa!”
25 And Judas—he who delivered Him up—answering said, “Is it I, Rabbi?” He says to him, “You have said.”
Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, akasema, “Je, ni mimi Rabi?” Yesu akajibu, “Naam, wewe mwenyewe umesema.”
26 And while they were eating, Jesus having taken the bread, and having blessed, broke, and was giving [it] to the disciples, and said, “Take, eat, this is My body”;
Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
27 and having taken the cup, and having given thanks, He gave to them, saying, “Drink of it—all;
Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, “Nyweni nyote katika kikombe hiki.
28 for this is My blood of the New Covenant, that is being poured out for many, for forgiveness of sins;
Hii ndiyo damu yangu ya Agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
29 and I say to you that I may not drink from now on this produce of the vine, until that day when I may drink it with you new in the kingdom of My Father.”
Lakini ninawaambia, tangu sasa sitakunywa tena katika uzao huu wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
30 And having sung a hymn, they went forth to the Mount of Olives;
Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
31 then Jesus says to them, “All you will be stumbled at Me this night; for it has been written: I will strike the Shepherd, and the sheep of the flock will be scattered abroad;
Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu, ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo wa hilo kundi watatawanyika.’
32 but after My having risen, I will go before you to Galilee.”
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
33 And Peter answering said to Him, “Even if all will be stumbled at You, I will never be stumbled.”
Petro akajibu, “Hata kama wote watakuacha, kamwe mimi sitakuacha.”
34 Jesus said to him, “Truly I say to you that this night, before rooster-crowing, three times you will deny Me.”
Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
35 Peter says to Him, “Even if it may be necessary for me to die with You, I will not deny You”; in like manner also said all the disciples.
Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wanafunzi wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36 Then Jesus comes with them to a place called Gethsemane, and He says to the disciples, “Sit here, until having gone away, I will pray over there.”
Kisha Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake mpaka kwenye bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia, “Kaeni hapa, nami niende kule nikaombe.”
37 And having taken Peter and the two sons of Zebedee, He began to be sorrowful, and to be very heavy;
Akamchukua Petro pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kufadhaika.
38 then He says to them, “Exceedingly sorrowful is My soul—to death; abide here, and watch with Me.”
Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe pamoja nami.”
39 And having gone forward a little, He fell on His face, praying, and saying, “My Father, if it be possible, let this cup pass from Me; nevertheless, not as I will, but as You.”
Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba akisema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe.”
40 And He comes to the disciples, and finds them sleeping, and He says to Peter, “So! You were not able to watch with Me one hour!
Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
41 Watch, and pray, that you may not enter into temptation: the spirit indeed is forward, but the flesh weak.”
Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
42 Again, a second time, having gone away, He prayed, saying, “My Father, if this cup cannot pass away from Me except I drink it, Your will be done”;
Akaenda tena mara ya pili na kuomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisikinywe, basi mapenzi yako yafanyike.”
43 and having come, He finds them again sleeping, for their eyes were heavy.
Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito.
44 And having left them, having gone away again, He prayed a third time, saying the same word;
Hivyo akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na kuomba akisema maneno yale yale.
45 then He comes to His disciples and says to them, “Sleep on from now on, and rest! Behold, the hour has come near, and the Son of Man is delivered up into the hands of sinners.
Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Tazameni, saa imefika ambapo Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
46 Rise, let us go; behold, he who is delivering Me up has come near.”
Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
47 And while He is yet speaking, behold, Judas, one of the Twelve came, and with him a great multitude, with swords and sticks, from the chief priests and elders of the people.
Alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Alikuwa amefuatana na umati mkubwa wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
48 And he who delivered Him up gave them a sign, saying, “Whomsoever I will kiss, it is He, lay hold on Him”;
Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni.”
49 and immediately, having come to Jesus, he said, “Greetings, Rabbi,” and kissed Him;
Mara Yuda akamjia Yesu na kumsalimu, “Salamu, Rabi!” Akambusu.
50 and Jesus said to him, “Friend, for what are you present?” Then having come near, they laid hands on Jesus, and took hold on Him.
Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.” Kisha wale watu wakasogea mbele, wakamkamata Yesu.
51 And behold, one of those with Jesus, having stretched forth the hand, drew his sword, and having struck the servant of the chief priest, he took off his ear.
Ghafula mmoja wa wale waliokuwa na Yesu alipoona hivyo, akaushika upanga wake, akauchomoa na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
52 Then Jesus says to him, “Turn back your sword to its place; for all who took the sword will perish by the sword;
Ndipo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote watumiao upanga watakufa kwa upanga.
53 do you think that I am not able now to call on My Father, and He will place beside Me more than twelve legions of messengers?
Je, unadhani siwezi kumwomba Baba yangu naye mara moja akaniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54 How then may the Writings be fulfilled, that thus it must happen?”
Lakini je, yale Maandiko yanayotabiri kwamba ni lazima itendeke hivi yatatimiaje?”
55 In that hour Jesus said to the multitudes, “Did you come forth as against a robber, with swords and sticks, to take Me? Daily I was with you sitting, teaching in the temple, and you did not lay hold on Me;
Wakati huo, Yesu akawaambia ule umati wa watu, “Je, mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? Siku kwa siku niliketi Hekaluni nikifundisha, mbona hamkunikamata?
56 but all this has come to pass, that the Writings of the prophets may be fulfilled”; then all the disciples, having left Him, fled.
Lakini haya yote yametukia ili maandiko ya manabii yapate kutimia.” Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
57 And those laying hold on Jesus led [Him] away to Caiaphas the chief priest, where the scribes and the elders were gathered together,
Wale waliokuwa wamemkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu, mahali ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee walikuwa wamekusanyika.
58 and Peter was following Him far off, to the court of the chief priest, and having gone in within, he was sitting with the officers, to see the end.
Lakini Petro akamfuata kwa mbali hadi uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akaketi pamoja na walinzi ili aone litakalotukia.
59 And the chief priests, and the elders, and all the council, were seeking false witness against Jesus, that they might put Him to death,
Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu ili wapate kumuua.
60 and they did not find; and many false witnesses having come near, they did not find; and at last two false witnesses having come near,
Lakini hawakupata jambo lolote, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa uongo
61 said, “This One said, I am able to throw down the temple of God, and after three days to build it.”
na kusema, “Huyu mtu alisema, ‘Ninaweza kulivunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’”
62 And the chief priest having stood up, said to Him, “Nothing You answer? What do these witness against You?”
Kisha kuhani mkuu akasimama na kumwambia Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
63 And Jesus was silent. And the chief priest answering said to Him, “I adjure You, by the living God, that You may say to us if You are the Christ—the Son of God.”
Lakini Yesu akakaa kimya. Ndipo kuhani mkuu akamwambia, “Nakuapisha mbele za Mungu aliye hai. Tuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”
64 Jesus says to him, “You have said; nevertheless I say to you, hereafter you will see the Son of Man sitting on the right hand of the Power and coming on the clouds of Heaven.”
Yesu akajibu, “Wewe umenena. Lakini ninawaambia nyote: Siku za baadaye, mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
65 Then the chief priest tore his garments, saying, “He has slandered; what need have we yet of witnesses? Behold, now you heard His slander;
Ndipo kuhani mkuu akararua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? Tazama, sasa ninyi mmesikia hayo makufuru.
66 what do you think?” And they answering said, “He is worthy of death.”
Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”
67 Then they spit in His face and punched Him, and others slapped,
Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi
68 saying, “Declare to us, O Christ, who he is that struck You?”
na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni nani aliyekupiga?”
69 And Peter was sitting in the court outside, and there came near to him a certain maid, saying, “And you were with Jesus of Galilee!”
Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
70 And he denied before all, saying, “I have not known what you say.”
Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”
71 And he having gone forth to the porch, another female saw him, and says to those there, “And this one was with Jesus of Nazareth”;
Alipotoka nje kufika kwenye lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwepo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
72 and again he denied with an oath, “I have not known the Man.”
Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”
73 And after a while those standing near having come, said to Peter, “Truly you also are of them, for even your speech makes you evident.”
Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”
74 Then he began to curse, and to swear, “I have not known the Man”; and immediately a rooster crowed,
Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.
75 and Peter remembered the saying of Jesus, He having said to him, “Before rooster-crowing, you will deny Me three times”; and having gone outside, he wept bitterly.
Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.