< Matthew 25 >
1 “Then will the kingdom of the heavens be likened to ten virgins, who, having taken their lamps, went forth to meet the bridegroom;
Ndipo ufalme wa mbinguni utafananishwa na wanawali kumi waliochukua taa zao na kuondoka kwenda kumpokea bwana harusi.
2 and five of them were prudent, and five foolish;
Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano wengine walikuwa werevu.
3 they who were foolish having taken their lamps, did not take with themselves oil;
Wanawali wapumbavu walipochukua taa zao, hawakuchukua mafuta yoyote.
4 and the prudent took oil in their vessels, with their lamps.
Bali wanawali welevu walichukua vyombo vyenye mafuta pamoja na taa zao.
5 And the bridegroom lingering, they all nodded and were sleeping,
Sasa wakati bwana harusi amechelewa kufika, wote walishikwa usingizi na wakalala.
6 and in the middle of the night a cry was made, Behold, the bridegroom comes; go forth to meet him!
Lakini wakati wa usiku wa manane kulikuwa na yowe, 'Tazama, bwana harusi! Tokeni nje mkampokee.'
7 Then all those virgins rose, and trimmed their lamps,
Ndipo hao wanawali waliamka wote na kuwasha taa zao.
8 and the foolish said to the prudent, Give us of your oil, because our lamps are going out;
Wale wapumbavu waliwaambia wale welevu, 'Mtupatie sehemu ya mafuta yenu kwa sababu taa zetu zinazimika.'
9 and the prudent answered, saying, Lest there may not be sufficient for us and you, go rather to those selling, and buy for yourselves.
Lakini wale welevu waliwajibu na kuwaambia, 'Kwa kuwa hayatatutosha sisi na ninyi, badala yake nendeni kwa wanaouza mjinunulie kiasi kwa ajili yenu.'
10 And while they are going away to buy, the bridegroom came, and those ready went in with him to the wedding feasts, and the door was shut;
Wakati wameenda huko kununua, Bwana harusi alifika, na wote waliokuwa tayari walienda naye kwenye sherehe ya harusi, na mlango ulifungwa.
11 and afterward come also the rest of the virgins, saying, Lord, lord, open to us;
Baadaye wale wanawali wengine pia walifika na kusema, 'Bwana, bwana, tufungulie.'
12 and he answering said, Truly I say to you, I have not known you.
Lakini alijibu na kusema, 'Kweli nawaambia, Mimi siwajui.'
13 Watch therefore, for you have not known the day nor the hour in which the Son of Man comes.
Kwa hiyo angalieni, kwa kuwa hamjui siku au saa.
14 For—as a man going abroad called his own servants, and delivered to them his substance,
Kwa kuwa ni sawa na mtu alipotaka kusafiri kwenda nchi nyingine. Aliwaita watumwa wake na kuwakabidhi utajiri wake.
15 and to one he gave five talents, and to another two, and to another one, to each according to his several ability, went abroad immediately.
Mmoja wao alimpatia talanta tano, mwingine alimpa mbili, na yule mwingine alimpa talanta moja. Kila mmoja alipokea kiasi kulingana na uwezo wake, na yule mtu alisafari kwenda zake.
16 And he who received the five talents, having gone, worked with them, and made five other talents;
Mapema yule aliyepokea talanta tano alienda kuziwekeza, na kuzalisha talanta zingine tano.
17 in like manner also he who [received] the two, he gained, also he, other two;
Vilevile yule aliyepokea talanta mbili, alizalisha zingine mbili.
18 and he who received the one, having gone away, dug in the earth, and hid his lord’s money.
Lakini mtumwa aliyepokea talanta moja, alienda zake, akachimba shimo ardhini, na kuificha fedha ya bwana wake.
19 And after a long time comes the lord of those servants, and takes reckoning with them;
Na baada ya muda mrefu, bwana wa watumwa hao alirudi na kutengeneza mahesabu nao.
20 and he who received the five talents, having come, brought five other talents, saying, Lord, you delivered five talents to me; behold, I gained five other talents besides them.
Yule mtumwa aliyepokea talanta tano alikuja na kuleta talanta zingine tano, akasema, 'Bwana, ulinipa talanta tano. Tazama, nimepata faida ya talanta zingine tano.'
21 And his lord said to him, Well done, good and faithful servant, you were faithful over a few things, I will set you over many things; enter into the joy of your lord.
Bwana wake alimwambia, 'Hongera, mtumwa mzuri na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vidogo. Nitakupa madaraka juu ya vitu vingi. Ingia katika furaha ya bwana wako.'
22 And he also, who received the two talents, having come, said, Lord, you delivered to me two talents; behold, I gained two other talents besides them.
Mtumwa aliyepokea talanta mbili alikuja na kusema, 'Bwana, ulinipa talanta mbili. Tazama, nimepata faida ya talanta zingine mbili,'
23 His lord said to him, Well done, good and faithful servant, you were faithful over a few things, I will set you over many things; enter into the joy of your lord.
Bwana wake alimwambia, 'Hongera, mtumwa mzuri na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache. Nitakupa madaraka juu ya vitu vingi. Ingia katika furaha ya bwana wako.'
24 And he also who has received the one talent, having come, said, Lord, I knew you, that you are a hard man, reaping where you did not sow, and gathering from where you did not scatter;
Baadaye mtumwa aliyepokea talanta moja alikuja na kusema, 'Bwana, najua kuwa wewe ni mtu mkali. Unachuma mahali ambapo hukupanda, na unavuna mahali ambapo hukusia.
25 and having been afraid, having gone away, I hid your talent in the earth; behold, you have your own!
Mimi niliogopa, nikaenda zangu na kuificha talanta yako katika udongo. Tazama, unayo hapa ile iliyo yako.'
26 And his lord answering said to him, Evil servant, and slothful, you had known that I reap where I did not sow, and I gather from where I did not scatter!
Lakini bwana wake alijibu na kusema, 'Wewe mtumwa mwovu na mzembe, ulijua kwamba ninachuma mahali ambapo sijapanda na kuvuna mahali ambapo sikusia.
27 It was necessary [for] you then to put my money to the money-lenders, and having come I had received my own with increase.
Kwahiyo ulipaswa kuwapa fedha yangu watu wa benki, na wakati wa kurudi kwangu ningeipokea ile yangu pamoja na faida.
28 Take therefore from him the talent, and give to him having the ten talents,
Kwa hiyo mnyang'anyeni hiyo talanta na mpeni yule mtumwa aliye na talanta kumi.
29 for to everyone having will be given, and he will have overabundance, and from him who is not having, even that which he has will be taken from him;
Kila mtu aliye nacho, ataongezewa zaidi-hata kwa kuzidishiwa sana. Lakini kwa yeyote asiye na kitu, hata alicho nacho atanyang'anywa.
30 and cast forth the unprofitable servant into the outer darkness; there will be the weeping and the gnashing of the teeth.
Mtupeni nje gizani huyo mtumwa asiyefaa, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.'
31 And whenever the Son of Man may come in His glory, and all the holy messengers with Him, then He will sit on a throne of His glory;
Wakati Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapokaa juu ya kiti chake cha utukufu.
32 and all the nations will be gathered together before Him, and He will separate them from one another, as the shepherd separates the sheep from the goats,
Mataifa yote yatakusanyika mbele zake, naye atawatenganisha watu, kama vile mchungaji anavyowatenganisha kondoo na mbuzi.
33 and He will set the sheep indeed on His right hand, and the goats on the left.
Atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, bali mbuzi atawaweka mkono wa kushoto.
34 Then the King will say to those on His right hand, Come, the blessed of My Father, inherit the kingdom that has been prepared for you from the foundation of the world;
Kisha mfalme atawaambia wale walio mkono wake wa kulia, 'Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.
35 for I hungered, and you gave Me to eat; I thirsted, and you gave Me to drink; I was a stranger, and you received Me;
Kwa kuwa nilikuwa na njaa na mlinipa chakula; Nilikuwa mgeni na mlinikaribisha;
36 naked, and you clothed Me; I was sick, and you looked after Me; I was in prison, and you came to Me.
Nilikuwa uchi, na mlinivika nguo; Nilikuwa mgonjwa na mkanitunza; Nilikuwa kifungoni na mkaniijia.'
37 Then will the righteous answer Him, saying, Lord, when did we see You hungering, and we nourished? Or thirsting, and we gave to drink?
Ndipo wenye haki watamjibu na kumwambia, 'Bwana, lini tulikuona ukiwa na njaa, na kukulisha? Au una kiu na tukakupa maji?
38 And when did we see You a stranger, and we received? Or naked, and we clothed?
Na lini tulikuona ukiwa mgeni, na tukakukaribisha? Au ukiwa uchi na tukakuvisha nguo?
39 And when did we see You ailing or in prison, and we came to You?
Na lini tulikuona ukiwa mgonjwa, au katika kifungo, na tukakujia?
40 And the King answering, will say to them, Truly I say to you, inasmuch as you did [it] to one of these My brothers—the least—you did [it] to Me.
Na mfalme atawajibu na kuwaambia, 'Kweli nawaambia, mlichotenda hapa kwa mmoja wa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.'
41 Then will He say also to those on the left hand, Go from Me, the cursed, into the continuous fire that has been prepared for the Devil and his messengers; (aiōnios )
Ndipo atawaambia hao walio mkono wake wa kushoto, 'Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, nendeni katika moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya shetani na malaika zake, (aiōnios )
42 for I hungered, and you gave Me nothing to eat; I thirsted, and you gave Me nothing to drink;
kwa sababu nilikuwa na njaa lakini hamkunipa chakula; Nilikuwa na kiu lakini hamkunipa maji;
43 I was a stranger, and you did not receive Me; naked, and you did not clothe Me; sick and in prison, and you did not look after Me.
Nilikuwa mgeni lakini hamkunikaribisha; nikiwa uchi lakini hamkunipa mavazi; nikiwa mgonjwa na nikiwa kifungoni, lakini hamkunitunza.'
44 Then they will answer, they also, saying, Lord, when did we see You hungering, or thirsting, or a stranger, or naked, or sick, or in prison, and we did not minister to You?
Ndipo wao pia watamjibu na kusema, 'Bwana, lini tulikuona ukiwa na njaa, au una kiu, au u mgeni, au ukiwa uchi, au ukiwa mgonjwa, au ukiwa mfungwa, na hatukukuhudumia?
45 Then will He answer them, saying, Truly I say to you, inasmuch as you did [it] not to one of these, the least, you did [it] not to Me.
Kisha atawajibu na kusema, 'Kweli nawaambia, kile ambacho hamkutenda kwa mmoja wa hawa wadogo, hamkunitendea mimi.'
46 And these will go away into continuous punishment, but the righteous into continuous life.” (aiōnios )
Hawa watakwenda katika adhabu ya milele bali wenye haki katika uzima wa milele.” (aiōnios )