< Matthew 19 >

1 And it came to pass, when Jesus finished these words, He removed from Galilee, and came to the borders of Judea, beyond the Jordan,
Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, alitoka Galilaya, akaenda katika mkoa wa Yudea, ng'ambo ya mto Yordani.
2 and great multitudes followed Him, and He healed them there.
Watu wengi walimfuata huko, naye akawaponya.
3 And the Pharisees came near to Him, tempting Him, and saying to Him, “Is it lawful for a man to put away his wife for every cause?”
Mafarisayo kadhaa walimjia, wakamwuliza kwa kumtega, “Je, ni halali mume kumpa talaka mkewe kwa kisa chochote?”
4 And He answering said to them, “Did you not read that He who made [them] from the beginning, made them a male and a female,
Yesu akawajibu, “Je, hamkusoma katika Maandiko Matakatifu kwamba Mungu aliyemuumba mtu tangu mwanzo alimfanya mwanamume na mwanamke,
5 and said, For this cause will a man leave father and mother, and cleave to his wife, and they will be—the two—for one flesh?
na akasema: Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataungana na mke wake, nao wawili watakuwa mwili mmoja?
6 So that they are no longer two, but one flesh; what therefore God joined together, let no man separate.”
Kwa hiyo wao si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asikitenganishe.”
7 They say to Him, “Why then did Moses command to give a roll of divorce, and to put her away?”
Lakini wao wakamwuliza, “Kwa nini basi, Mose alituagiza mwanamke apewe hati ya talaka na kuachwa?”
8 He says to them, “Moses for your stiffness of heart permitted you to put away your wives, but from the beginning it has not been so.
Yesu akawajibu, “Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
9 And I say to you that whoever may put away his wife, if not for whoredom, and may marry another, commits adultery; and he who married her that has been put away, commits adultery.”
Lakini haikuwa hivyo tangu mwanzo. Basi nawaambieni, yeyote atakayemwacha mke wake isipokuwa kwa sababu ya uzinzi, akaoa mke mwingine, anazini.”
10 His disciples say to Him, “If the case of the man with the woman is so, it is not good to marry.”
Wanafunzi wake wakamwambia, “Ikiwa mambo ya mume na mkewe ni hivyo, ni afadhali kutooa kabisa.”
11 And He said to them, “All do not receive this word, but those to whom it has been given;
Yesu akawaambia, “Si wote wanaoweza kulipokea fundisho hili, isipokuwa tu wale waliojaliwa na Mungu.
12 for there are eunuchs who from the mother’s womb were so born; and there are eunuchs who were made eunuchs by men; and there are eunuchs who kept themselves eunuchs because of the kingdom of the heavens: he who is able to receive [it]—let him receive.”
Maana kuna sababu kadhaa za kutoweza kuoa: wengine ni kwa sababu wamezaliwa hivyo, wengine kwa sababu wamefanywa hivyo na watu, na wengine wameamua kutooa kwa ajili ya Ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea fundisho hili na alipokee.”
13 Then were brought near to Him children that He might put hands on them and pray, and the disciples rebuked them.
Kisha watu wakamletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono na kuwaombea. Lakini wanafunzi wakawakemea.
14 But Jesus said, “Permit the children, and do not forbid them to come to Me, for of such is the kingdom of the heavens”;
Yesu akasema, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie; maana Ufalme wa mbinguni ni wa watu walio kama watoto hawa.”
15 and having laid [His] hands on them, He departed from there.
Basi, akawawekea mikono, kisha akaondoka mahali hapo.
16 And behold, one having come near, said to Him, “Good Teacher, what good thing will I do that I may have continuous life?” (aiōnios g166)
Mtu mmoja alimjia Yesu, akamwuliza, “Mwalimu, nifanye kitu gani chema ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
17 And He said to him, “Why do you call Me good? No one [is] good except one—God; but if you will to enter into life, keep the commands.”
Yesu akamwambia, “Mbona unaniuliza kuhusu jambo jema? Kuna mmoja tu aliye mwema. Ukitaka kuingia katika uzima, shika amri.”
18 He says to Him, “What kind?” And Jesus said, “You will not murder, You will not commit adultery, You will not steal, You will not bear false witness,
Yule mtu akamwuliza, “Amri zipi?” Yesu akasema, “Usiue, usizini, usiibe, usitoe ushahidi wa uongo,
19 Honor your father and mother, and, You will love your neighbor as yourself.”
waheshimu baba yako na mama yako; na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
20 The young man says to Him, “All these I kept from my youth; what yet do I lack?”
Huyo kijana akamwambia, “Hayo yote nimeyazingatia tangu utoto wangu; sasa nifanye nini zaidi?”
21 Jesus said to him, “If you will to be perfect, go away, sell what you have, and give to the poor, and you will have treasure in Heaven, and come, follow Me.”
Yesu akamwambia, “Kama unapenda kuwa mkamilifu, nenda ukauze mali yako uwape maskini hiyo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni, kisha njoo unifuate.”
22 And the young man, having heard the word, went away sorrowful, for he had many possessions;
Huyo kijana aliposikia hayo, alienda zake akiwa mwenye huzuni, maana alikuwa na mali nyingi.
23 and Jesus said to His disciples, “Truly I say to you that hardly will a rich man enter into the kingdom of the heavens;
Hapo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kweli nawaambieni, itakuwa vigumu sana kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.
24 and again I say to you, it is easier for a camel to go through the eye of a needle, than for a rich man to enter into the Kingdom of God.”
Tena nawaambieni, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.”
25 And His disciples having heard, were exceedingly amazed, saying, “Who, then, is able to be saved?”
Wale wanafunzi waliposikia hivyo walishangaa, wakamwuliza, “Ni nani basi, awezaye kuokoka?”
26 And Jesus having earnestly beheld, said to them, “With men this is impossible, but with God all things are possible.”
Yesu akawatazama, akasema, “Kwa binadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu mambo yote huwezekana.”
27 Then Peter answering said to Him, “Behold, we left all, and followed You, what then will we have?”
Kisha Petro akasema, “Na sisi je? Tumeacha yote tukakufuata; tutapata nini basi?”
28 And Jesus said to them, “Truly I say to you that you who followed Me, in the regeneration, when the Son of Man may sit on a throne of His glory, will sit—you also—on twelve thrones, judging the twelve tribes of Israel;
Yesu akawaambia, “Nawaambieni kweli, Mwana wa Mtu atakapoketi katika kiti cha enzi cha utukufu wake katika ulimwengu mpya, ninyi mlionifuata mtaketi katika viti kumi na viwili mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
29 and everyone who left houses, or brothers, or sisters, or father, or mother, or wife, or children, or fields, for My Name’s sake, will receive a hundredfold, and will inherit continuous life; (aiōnios g166)
Na kila aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi, na kupata uzima wa milele. (aiōnios g166)
30 and many first will be last, and last first.”
Lakini walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.

< Matthew 19 >