< Matthew 14 >
1 At that time Herod the tetrarch heard the fame of Jesus,
Kwa wakati huo, Herode alisikia habari juu ya Yesu.
2 and said to his servants, “This is John the Immerser, he rose from the dead, and because of this the mighty energies are working in him.”
Akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji amefufuka kutoka katika wafu. Kwa hiyo nguvu hizi zipo juu yake.”
3 For Herod having laid hold on John, bound him, and put him in prison, because of Herodias, his brother Philip’s wife,
Kwa kuwa Herode alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumtupa gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo kaka yake.
4 for John was saying to him, “It is not lawful to you to have her,”
Kwa kuwa Yohana alimwambia, “Si halali kumchukua yeye kuwa mke wake.”
5 and willing to kill him, he feared the multitude, because as a prophet they were holding him.
Herode angemwua lakini aliwaogopa watu kwa sababu walimwona Yohana kuwa nabii.
6 But the birthday of Herod being kept, the daughter of Herodias danced in the midst, and pleased Herod,
Lakini wakati siku ya kuzaliwa Herode ilipofika binti wa Herodia alicheza katikati ya watu na kumpendeza Herode.
7 after which with an oath he professed to give her whatever she might ask.
Katika kujibu kili aliahidi kwa kiapo kwamba atampa chochote atakachoomba.
8 And she, having been instigated by her mother, says, “Give me here on a plate the head of John the Immerser”;
Baada ya kushauriwa na mama yake, alisema, “Nipe mimi hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
9 and the king was grieved, but because of the oaths and of those dining with him, he commanded [it] to be given;
Mfalme alikuwa na sikitiko kwa maombi ya binti, lakini kwa ajili ya kiapo chake, kwa sababu ya wote waliokuwa chakulani pamoja naye aliamuru kwamba inapaswa ifanyike.
10 and having sent, he beheaded John in the prison,
Alituma Yohana aletwe kutoka gerezani
11 and his head was brought on a plate, and was given to the girl, and she brought [it] near to her mother.
ili akatwe kichwa chake na kikaletwa juu ya sinia na akapewa binti na akakipeleka kwa mama yake.
12 And his disciples having come, took up the body, and buried it, and having come, they told Jesus,
Kisha wanafunzi wake wakaja kuuchukua ule mwili na kuuzika, baada ya hili walienda kumwambia Yesu.
13 and Jesus having heard, withdrew from there in a boat to a desolate place by Himself, and the multitudes having heard followed Him on land from the cities.
Naye Yesu aliposika haya, akijatenga kutoka mahali pale akapanda ndani ya mashuka akaenda sehemu iliyotengwa. Wakati umati ulipo fahamu alikokuwa, walimfuata kwa miguu kutoka mijini.
14 And Jesus having come forth, saw a great multitude, and was moved with compassion on them, and healed their sick;
Kisha Yesu alikuja mbele yao akauona umati mkubwa. Akawaonea huruma na kuponya magonjwa yao.
15 and evening having come, His disciples came to Him, saying, “The place is desolate, and the hour has now past, let away the multitudes that, having gone into the villages, they may buy food for themselves.”
Jioni ilipotimia, wanafunzi wakaja kwake na kusema, “Hii ni sehemu ya jangwa, na siku tayari imepita. Watawanyishe makutano ili waende vijijini wakanunue chakula kwa ajili yao.
16 And Jesus said to them, “They have no need to go away—you give them to eat.”
Lakini Yesu akawaambia, ''Hawana haja ya kwenda zao. Wapeni ninyi chakula”
17 And they say to Him, “We have nothing here except five loaves and two fishes.”
Wakamwambia, ''Hapa tunayo mikate mitano na samaki wawili tu.”''
18 And He said, “Bring them to Me here.”
Yesu akasema, “Ileteni kwangu.”
19 And having commanded the multitudes to recline on the grass, and having taken the five loaves and the two fishes, having looked up to the sky, He blessed, and having broken, He gave the loaves to the disciples, and the disciples [gave] to the multitudes,
Kisha Yesu akauamuru umati kukaa chini ya nyasi. Akachukuwa mikate mitano na samaki wawili. Akatazama juu mbinguni, akabariki na kumega mikate akawapa wanafunzi. Wanafunzi wakaupatia umati.
20 and they all ate, and were filled, and they took up what was over of the broken pieces twelve hand-baskets full;
Wakala wote na kushiba. Kisha wakavikusanya vipande vyote vya chakula na kujaza vikapu kumi na mbili.
21 and those eating were about five thousand men, apart from women and children.
Wale waliokula walikadiriwa kuwa wanaume elfu tano bila ya kusehabu wanawake na watoto.
22 And immediately Jesus constrained His disciples to go into the boat, and to go before Him to the other side, until He might let away the multitudes;
Mara moja aliwaamuru wanafunzi waingie ndani ya mashua, wakati huo yeye akawaaga umati waende zao.
23 and having let away the multitudes, He went up to the mountain by Himself to pray, and evening having come, He was there alone,
Baada ya kuwaaga umati kwenda zao, akapanda juu mlimani kuomba pekee yake. Wakati ilipokuwa jioni alikuwa huko pekee yake.
24 and the boat was now in the midst of the sea, distressed by the waves, for the wind was contrary.
Lakini sasa mashua ilipokuwa katikati ya bahari ukiyumbayumba kwa sababu ya mawimbi, kwani upepo ulikuwa wa mpisho.
25 And in the fourth watch of the night Jesus went away to them, walking on the sea,
Katika usiku wa zamu ya nne Yesu aliwakaribia, akitembea juu ya maji.
26 and the disciples having seen Him walking on the sea, were troubled, saying, “It is an apparition,” and from the fear they cried out;
Wakati wanafunzi wake walipomwona akiitembea juu ya bahari, walihofu na kusema, “Ni mzuka,'' na kupaaza sauti katika hali ya uoga.
27 and immediately Jesus spoke to them, saying, “Take courage! I AM; do not be afraid.”
Yesu akawaambia mara moja, akisema, “Jipeni moyo! ni mimi! msiogope.”
28 And Peter answering Him said, “Lord, if it is You, command me to come to You on the waters”;
Petro alimjibu kwa kusema, “Bwana, kama ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.''
29 and He said, “Come”; and having gone down from the boat, Peter walked on the waters to come to Jesus,
Yesu akasema, “Njoo.'' Hivyo Petro akatoka ndani ya mashua na akatembea juu ya maji kwenda kwa Yesu.
30 but seeing the vehement wind, he was afraid, and having begun to sink, he cried out, saying, “Lord, save me!”
Lakini Petro alipoona mawimbi, aliogopa, na kuanza kuzama, chini, akaita sauti na kusema, “Bwana, niokoe!''
31 And immediately Jesus, having stretched forth the hand, laid hold of him and says to him, “Little faith! For why did you waver?”
Haraka Yesu akanyoosha mkono wake akamnyanyua Petro, na kumwambia, “Wewe mwenye imani ndogo, kwa nini ulikuwa na mashaka?”
32 And they having gone into the boat, the wind stilled,
Ndipo Yesu na Petro walipoingia katika mashua, upepo ulikoma kuvuma.
33 and those in the boat having come, worshiped Him, saying, “You are truly God’s Son.”
Wanafunzi mashuani wakamwabudu Yesu na kusema, “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu.”
34 And having passed over, they came into the land of Gennesaret,
Na walipokwisha kuvuka, walifika katika nchi ya Genesareti.
35 and having recognized Him, the men of that place sent forth to all that surrounding region, and they brought to Him all who were ill,
Na watu katika eneo lile walipomtambua Yesu, walituma ujumbe kila sehemu za kando, na kuleta kila aliyekuwa mgonjwa.
36 and were calling on Him that they might only touch the fringe of His garment, and as many as touched were saved.
Walimsihi kwamba waweze kugusha pindo la vazi lake, na wengi walioligusa waliponywa.