< Matthew 12 >
1 At that time Jesus went on the Sabbaths through the grainfields, and His disciples were hungry, and they began to pluck ears, and to eat,
Wakati huo Yesu alienda siku ya sabato kupitia mashambani. Wanafunzi wake walikuwa na njaa na wakaanza kuyavunja masuke na kuyala.
2 and the Pharisees having seen, said to Him, “Behold, Your disciples do that which it is not lawful to do on a Sabbath.”
Lakini Mafarisayo walipoona hayo, wakamwambia Yesu “Angalia wanafunzi wako wanavunja sheria wanatenda siku yasiyo yuhusiwa siku ya Sabato''
3 And He said to them, “Did you not read what David did when he was hungry, himself and those with him—
Lakini Yesu akawaambia, “Hamjasoma jinsi Daudi aliyoyafanya, wakati alipokuwa na njaa, pamoja na watu aliokuwa nao?
4 how he went into the house of God, and ate the Bread of the Presentation, which it is not lawful to him to eat, nor to those with him, except to the priests alone?
Namna alivyoingia ndani ya nyumba ya Mungu na kula mikate ya wonyesho, ambayo ilikuwa siyo halali kwake kuila na wale aliokuwa nao, ila halali kwa Makuhani?
5 Or did you not read in the Law that on the Sabbaths the priests in the temple profane the Sabbath and are blameless?
Bado hamjasoma katika sheria, kwamba katika siku ya Sabato Makuhani ndani ya hekalu huinajisi Sabato, lakini hawana hatia?
6 And I say to you that [One] greater than the temple is here;
Lakini nasema kwenu kuwa aliye mkuu kuliko hekalu yuko hapa.
7 and if you had known what [this] is: Kindness I will, and not sacrifice—you had not condemned the blameless,
Kama mngalijua hii ina maanisha nini; nataka rehema na siyo dhabihu; msingaliwahukumu wasio na hatia,
8 for the Son of Man is Lord even of the Sabbath.”
Kwa kuwa Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
9 And having departed from there, He went to their synagogue,
Kisha Yesu akatoka pale akaenda katika sinagogi lao.
10 and behold, there was a man having the hand withered, and they questioned Him, saying, “Is it lawful to heal on the Sabbaths?” That they might accuse Him.
Tazama kulikuwa na mtu aliyepooza mkono. Mafarisayo wakamuuliza Yesu, wakisema. “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?” ili kwamba waweze kumshitaki kwa kutenda dhambi.
11 And He said to them, “What man will be of you who will have one sheep, and if this may fall on the Sabbaths into a ditch, will not lay hold on it and raise [it]?
Yesu akawaambia, “Nani kati yenu, ambaye ikiwa ana kondoo mmoja, na huyu kondoo akaanguka ndani ya shimo siku ya sabato, hatamshika na kumtoa kwa nguvu ndani ya shimo?
12 How much better, therefore, is a man than a sheep? So that it is lawful on the Sabbaths to do good.”
Je, ni kipi chenye thamani, zaidi kwani, si zaidi ya kondoo! Kwa hivyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.''
13 Then He says to the man, “Stretch forth your hand,” and he stretched [it] forth, and it was restored whole as the other.
Kisha Yesu akamwambia yule mtu,” Nyoosha mkono wako” Akaunyoosha, na ukapata afya, kama ule mwingine.
14 And the Pharisees having gone forth, held a consultation against Him, how they might destroy Him,
Lakini Mafarisayo wakatoka njena wakapanga jinsi ya kumwangamiza walienda nje kupanga kinyume chake. Walikuwa wakitafuta jinsi ya kumuua.
15 and Jesus having known, withdrew from there, and there followed Him great multitudes, and He healed them all,
Yesu alipoelewa hili aliondoka hapo. Watu wengi walimfuata, na akawaaponya wote.
16 and charged them that they might not make Him apparent,
Aliwaagiza wasije wakamfanya afahamike kwa wengine,
17 that it might be fulfilled that was spoken through Isaiah the prophet, saying,
kwamba itimie ile kweli, iliyokuwa imesemwa na nabii Isaya, akisema,
18 “Behold, My Servant, whom I chose, My Beloved, in whom My soul delighted, I will put My Spirit on Him, And He will declare judgment to the nations;
Tazama, mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu, katika yeye nafsi yangu imependezwa. Nitaweka Roho yangu juu yake, na atatangaza hukumu kwa Mataifa.
19 He will not strive nor cry, Nor will any hear His voice in the broad places;
Hatahangaika wala kulia kwa nguvu; wala awaye yote kusikia sauti yake mitaani.
20 A bruised reed He will not break, And smoking flax He will not quench, Until He may put forth judgment to victory,
Hatalivunja tete lililochubuliwa; hatazima utambi wowote utoao moshi, mpaka atakapoleta hukumu ikashinda.
21 And in His Name will nations hope.”
Na Mataifa watakuwa na ujasiri katika jina lake.
22 Then was brought to Him a demoniac, blind and mute, and He healed him, so that the blind and mute both spoke and saw.
Mtu fulani kipofu na bubu, aliyepagawa na pepo aliletwa mbele ya Yesu. Akamponya, pamoja na matokeo ya kwamba mtu bubu alisema na kuona.
23 And all the multitudes were amazed and said, “Is this the Son of David?”
Makutano wote walishangaa na kusema,”Yaweza mtu huyu kuwa mwana wa Daudi?”
24 But the Pharisees having heard, said, “This One does not cast out demons, except by Beelzebul, ruler of the demons.”
Lakini pindi Mafarisayo waliposikia muujiza huu, walisema, “Huyu mtu hatoi pepo kwa nguvu zake mwenyewe isipokuwa kwa nguvu za Belzebuli, mkuu wa pepo.
25 And Jesus, knowing their thoughts, said to them, “Every kingdom having been divided against itself is desolated, and no city or house having been divided against itself stands,
“Lakini Yesu alifahamu fikra zao na kuwaambia, “Kila ufalme uliogawanyika wenyewe huharibika, na kila mji au nyumba inayogawanyika yenyewe haitasimama.
26 and if Satan casts out Satan, against himself he was divided, how then does his kingdom stand?
Ikiwa Shetani, atamwondoa Shetani, basi anajipinga katika nafsi yake mwenyewe.
27 And if I, by Beelzebul, cast out the demons, your sons—by whom do they cast out? Because of this they will be your judges.
Ni namna gani ufalme wake utasimama? Na kama natoa pepo kwa nguvu za Belizabuli, wafuasi wenu huwatatoa kwa nija ya nani? Kwa ajili ya hili watakuwa mahakimu wenu.
28 But if I, by the Spirit of God, cast out the demons, then the Kingdom of God has already come to you.
Na kama natoa pepo kwa nguvu za Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekjua kwenu.
29 Or how is one able to go into the house of the strong man, and to snatch his goods, if first he may not bind the strong man? And then his house he will plunder.
Na mtu atawezaje kuingia ndani ya nyumba ya mwenye nguvu na kuiba, bila kumfunga mwenye nguvu kwanza? Ndiyo atakapoiba mali yake kutoka ndani ya nyumba.
30 He who is not with Me is against Me, and he who is not gathering with Me, scatters.
Yeyote asiye kuwa pamoja nami yuko kinyume changu, naye asiye kusanya pamoja nami huyo hutawanya.
31 Because of this I say to you, all sin and slander will be forgiven to men, but the slander of the Spirit will not be forgiven to men.
Kwa hiyo nasema kwenu, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, ila kumkufuru Roho Mtakatifu hawatasamehewa.
32 And whoever may speak a word against the Son of Man it will be forgiven to him, but whoever may speak against the Holy Spirit, it will not be forgiven him, neither in this age, nor in that which is coming. (aiōn )
Na yeyote asemaye neno kinyume cha Mwana wa Adamu, hilo atasamehewa. Lakini yeyote asemaye kinyume na Roho Mtakatifu, huyo hatasamehewa, katika ulimwengu huu, na wala ule ujao (aiōn )
33 Either make the tree good, and its fruit good, or make the tree bad, and its fruit bad, for from the fruit is the tree known.
Ama ufanye mti kuwa mzuri na tunda lake zuri, au uuharibu mti na tunda lake, kwa kuwa mti hutambulika kwa tunda lake.
34 Brood of vipers! How are you able to speak good things—being evil? For out of the abundance of the heart the mouth speaks.
Nyinyi kizazi cha nyoka, nyie ni waovu, mnawezaje kusema mambo mazuri? Kwa kuwa kinywa hunena kutoka katika akiba ya yaliyomo moyoni.
35 The good man out of the good treasure of the heart puts forth the good things, and the evil man out of the evil treasure puts forth evil things.
Mtu mwema katika akiba njema ya moyo wake hutoka mema, na mtu mwovu katika akiba ovu ya moyo wake, hutoa kilicho kiovu.
36 And I say to you that every idle word that men may speak, they will give for it a reckoning in [the] day of judgment;
Nawaambia kuwa katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu ya kila neno lisilo na maana walilosema.
37 for from your words you will be declared righteous, and from your words you will be declared unrighteous.”
Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki na kwa maneno yako utahukumiwa.”
38 Then certain of the scribes and Pharisees answered, saying, “Teacher, we will to see a sign from You.”
Kisha baadhi ya waandishi na Mafarisayo walimjibu Yesu wakisema” Mwalimu, tungependa kuona ishara kutoka kwako.”
39 And He answering said to them, “A generation, evil and adulterous, seeks a sign, and a sign will not be given to it, except the sign of Jonah the prophet;
Lakini Yesu alijibu na kuwaambia, “Kizazi kiovu na cha zinaa kinatafuta ishara. Lakini hakuna ishara itakayotolewa kwao isipokuwa ile ishara ya Yona nabii.
40 for as Jonah was in the belly of the fish three days and three nights, so will the Son of Man be in the heart of the earth three days and three nights.
Kama vile nabii Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la samaki mkubwa kwa siku tatu mchana na usiku, hivyo ndivyo Mwana wa Adam atakavyo kuwa ndani ya moyo wa nchi kwa siku tatu mchana na usiku.
41 Men of Nineveh will stand up in the judgment with this generation, and will condemn it, for they converted at the proclamation of Jonah, and behold, [One] greater than Jonah [is] here!
Watu wa Ninawi watasimama mbele ya hukumu pamoja na kizazi cha watu hawa na watakihukumu. Kwa kuwa walitubu kwa mahubiri ya Yona, na tazama, mtu fulani mkuu kuliko Yona yuko hapa.
42 A queen of the south will rise up in the judgment with this generation, and will condemn it, for she came from the ends of the earth to hear the wisdom of Solomon, and behold, [One] greater than Solomon [is] here!
Malkia wa kusini atainuka kwenye hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki na kukihukumu. Alikuja toka miisho ya dunia kuja kusikia hekima ya Selemani, na tazama, mtu fulani mkuu kuliko Selemani yupo hapa.
43 And when the unclean spirit may go forth from the man, it walks through dry places seeking rest and does not find;
Wakati pepo mchafu amtokapo mtu, hupita mahali pasipo na maji akitafuta kupumzika, lakini hapaoni
44 then it says, I will return to my house from where I came forth; and having come, it finds [it] unoccupied, swept, and adorned:
Kisha husema, 'nitarudi kwenye nyumba yangu niliyotoka.' Arudipo hukuta ile nyumba imesafishwa na iko tayari.
45 then it goes, and takes with itself seven other spirits more evil than itself, and having gone in they dwell there, and the last of that man becomes worse than the first; so will it also be to this evil generation.”
Kisha huenda na kuwaleta wengine roho wachafu saba walio wabaya zaidi kuliko yeye, huja kuishi wote pale. Na hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Hivyo ndivyo itakavyo kuwa kwa kizazi hiki kiovu.
46 And while He was yet speaking to the multitudes, behold, His mother and brothers had stood outside, seeking to speak to Him,
Wakati Yesu alipokuwa akizungumza na umati tazama, mama yake na ndugu zake walisimama nje, wakitafuta kuongea naye.
47 and one said to Him, “Behold, Your mother and Your brothers stand outside, seeking to speak to You.”
Mtu mmoja akamwambia, “Tazama mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanatafuta kuongea nawe”.
48 And He answering said to him who spoke to Him, “Who is My mother? And who are My brothers?”
Lakini Yesu alijibu na kumwambia aliyemjulisha, “Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina nani?”
49 And having stretched forth His hand toward His disciples, He said, “Behold, My mother and My brothers!
Naye alinyoosha mkono wake kwa wanafunzi na kusema, “Tazama, hawa ni mama na ndugu zangu!
50 For whoever may do the will of My Father who is in the heavens, He is My brother, and sister, and mother.”
Kwa kuwa yeyote afanyae mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, mtu huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu”.