< Matthew 11 >

1 And it came to pass, when Jesus finished directing His twelve disciples, He departed from there to teach and to preach in their cities.
Ikawa baada ya Yesu kumaliza kuwaelekeza wanafunzi wake kumi na wawili aliondoka plae kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao,
2 And John having heard in the prison the works of the Christ, having sent two of his disciples,
na Yohana akiwa gereszani aliposikia akiwa juu ya matendo ya Kristo, alituma ujumbe kupitia wanafunzi wake,
3 said to Him, “Are You He who is coming, or do we look for another?”
na wakamuuliza, “Wewe ni yule ajaye, au kuna mwingine tunapaswa kumtazamia?”
4 And Jesus answering said to them, “Having gone, declare to John the things that you hear and see,
Yesu akajibu na kusema kwao “Nendeni mkamtaarifu Yohana yale mnayoyaona na yale mnayoyasikia.
5 blind receive sight, and lame walk, lepers are cleansed, and deaf hear, dead are raised, and poor have good news proclaimed,
Watu wasioona wanapata kuona, viwete wanatembea, wakoma wanatakaswa, watu wasiosikia wanasikia tena, watu waliokufa wanafufuliwa kupata uhai, na watu wahitaji wanahubiriwa habari njema.
6 and blessed is he who may not be stumbled in Me.”
Na amebarikiwa yule asiyeona shaka juu yangu.
7 And as they are going, Jesus began to say to the multitudes concerning John, “What did you go out to the wilderness to view? A reed shaken by the wind?
Pindi watu hawa walipoondoka, Yesu alianza kusema na umati juu ya Yohana, “Ni nini mlikwenda kuona katika jangwa tete likitikiswa na upepo?
8 But what did you go out to see? A man clothed in soft garments? Behold, those wearing the soft things are in the kings’ houses.
Lakini nini mlikwenda kuona mtu aliyevaa mavazi mololo? Hakika, wale wavaao mavazi mololo hukaa katika nyumba za wafalme.
9 But what did you go out to see? A prophet? Yes, I say to you, and more than a prophet,
Lakini mliondoka kuona nini-Nabii? Ndiyo, nawaambia, na zaidi ya Nabii.
10 for this is he of whom it has been written: Behold, I send My messenger before Your face, who will prepare Your way before You.
Huyu ndiye aliyeandikiwa, 'Tazama, namtuma mjumbe wangu mbele ya uso wako, ambaye ataandaa njia yako mbele yako.
11 Truly I say to you, there has not risen, among those born of women, [one] greater than John the Immerser, but he who is least in the kingdom of the heavens is greater than he.
Mimi nawaambia kweli, kati ya waliozaliwa na wanawake hakuna aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkubwa kuliko yeye.
12 And from the days of John the Immerser until now, the kingdom of the heavens suffers violence, and violent men seize it by force,
Toka siku za Yohana Mbatizaji mpaka sasa, ufalme wa Mbinguni ni wa nguvu, na watu wenye nguvu, huuchukua kwa nguvu.
13 for all the Prophets and the Law prophesied until John,
Kwa kuwa manabii na sheria, ikamelcuwa wakitabiri mpaka kwa Yohana.
14 and if you are willing to receive [it], he is Elijah who was about to come;
Na kamamko tayari kukubali, huyu ni Eliya, yule ajaye.
15 he who is having ears to hear—let him hear.
Aliye na masikio ya kusikia na asikie.
16 And to what will I liken this generation? It is like little children in marketplaces, sitting and calling to others,
Nikilinganishe na nini kizazi hiki? Ni mfano wa watoto wanaocheza maeneo ya sokoni, wanaokaa na kuitana
17 and saying, We piped to you, and you did not dance, we lamented to you, and you did not strike the breast.
na kusema, 'Tuliwapigia zomari na hamkucheza. Tuliomboleza, na hamukulia.'
18 For John came neither eating nor drinking, and they say, He has a demon;
Kwa kuwa Yohana alikuja bila kula mkate au kunywa mvinyo, na wakawa wanasema, 'Ana pepo.'
19 the Son of Man came eating and drinking, and they say, Behold, a man, a glutton, and a wine-drinker, a friend of tax collectors and sinners; and wisdom was justified of her children.”
Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa na wakasema 'Angalia, ni mtu mlaji na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi!' Lakini hekima inadhihirishwa kwa matendo yake.''
20 Then He began to reproach the cities in which were done most of His mighty works, because they did not convert.
Yesu alianza kuikemea miji ambamo baadhi ya matendo yake ya ajabu yalitendeka, kwa sababu walikuwa hawajatubu,
21 “Woe to you, Chorazin! Woe to you, Bethsaida! Because, if in Tyre and Sidon had been done the mighty works that were done in you, long ago in sackcloth and ashes they had converted;
Ole wako, Kolazini, Ole wako Bethsaida! Kama matendo makuu yangetendeka Tiro na Sidoni yale yaliyotendeka hapa, wangekuwa wametubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
22 but I say to you, to Tyre and Sidon it will be more tolerable in [the] day of judgment than for you.
Lakini itakuwa uvumilivu kwa Tiro na Sidoni siku ya hukumu kuliko kwako.
23 And you, Capernaum, which were exalted to Heaven, will be brought down to Hades, because if the mighty works that were done in you had been done in Sodom, it had remained to this day; (Hadēs g86)
Wewe, Kapernaum, unadhani utainuliwa hadi mbinguni? Hapana utashushwa hadi chini kuzimu. Kama kwa Sodoma kungefanyika matendo makuu, kama yalifanyika kwako, ingekuwepo hadi leo. (Hadēs g86)
24 but I say to you, to the land of Sodom it will be more tolerable in [the] day of judgment than to you.”
Bali nasema kwako kwamba itakuwa rahisi kwa nchi ya Sodoma kusimama siku ya hukumu kuliko wewe.
25 At that time Jesus answering said, “I confess to You, Father, Lord of the heavens and of the earth, that You hid these things from wise and understanding ones, and revealed them to babies.
Katika muda huo Yesu alisema, “Nakusifu wewe, Baba, Bwana wa Mbingu na Nchi, kwa sababu uliwaficha mambo haya wenye hekima na ufahamu, na kuyafunua kwa wasio na elimu, kama watoto wadogo.
26 Yes, Father, because so it was good pleasure before You.
Baba kwa kuwa ilikupendeza hivyo machoni pako.
27 All things were delivered to Me by My Father, and none know the Son, except the Father, nor does any know the Father, except the Son, and he to whom the Son may resolve to reveal [Him].
Mambo yote yamekabidhiwa kwangu kutoka kwa Baba. Na hakuna amjuaye Mwana isipokuwa Baba, na hakuna amjuaye Baba isipokuwa Mwana, na yeyote ambaye Mwana ana hamu ya kumfunulia.
28 Come to Me, all you laboring and burdened ones, and I will give you rest;
Njoni kwangu, nyinyi nyote mnaosumbuka na mnaolemewa na mzigo mzito, nami nitawapumzisha.
29 take up My yoke on you, and learn from Me, because I am meek and humble in heart, and you will find rest to your souls,
Jitieni nira yangu na mjifunze kutoka kwangu, kwa kuwa mimi ni mnyenyekevu na mpole wa moyo na mtapata pumziko la nafsi zenu.
30 for My yoke [is] easy, and My burden is light.”
Kwa kuwa nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.

< Matthew 11 >