< Mark 1 >
1 A beginning of the good news of Jesus Christ, Son of God.
Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 As it has been written in the Prophets: “Behold, I send My messenger before Your face, Who will prepare Your way before You.
Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3 A voice of one calling in the wilderness: Prepare the way of the LORD, Make His paths straight.”
Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
4 John came immersing in the wilderness, and proclaiming an immersion of conversion for forgiveness of sins,
Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5 and there were going forth to him all the region of Judea, and they of Jerusalem, and they were all immersed by him in the river Jordan, confessing their sins.
Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6 And John was clothed with camel’s hair, and a girdle of skin around his loins, and eating locusts and honey of the field,
Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7 and he proclaimed, saying, “He comes—who is mightier than I—after me, of whom I am not worthy—having stooped down—to loose the strap of His sandals;
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8 I indeed immersed you in water, but He will immerse you in the Holy Spirit.”
Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 And it came to pass in those days, Jesus came from Nazareth of Galilee, and was immersed by John in the Jordan;
Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10 and immediately coming up from the water, He saw the heavens dividing, and the Spirit coming down on Him as a dove;
Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11 and a voice came out of the heavens, “You are My Son, the Beloved, in whom I delighted.”
Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
12 And immediately the Spirit puts Him forth into the wilderness,
Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13 and He was there in the wilderness forty days, being tempted by Satan, and He was with the beasts, and the messengers were ministering to Him.
akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14 And after the delivering up of John, Jesus came to Galilee, proclaiming the good news of the Kingdom of God,
Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15 and saying, “The time has been fulfilled, and the Kingdom of God has come near, convert and believe in the good news.”
“Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
16 And walking by the Sea of Galilee, He saw Simon, and his brother Andrew, casting a drag into the sea, for they were fishers,
Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17 and Jesus said to them, “Come after Me, and I will make you to become fishers of men”;
Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
18 and immediately, having left their nets, they followed Him.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19 And having gone on there a little, He saw James of Zebedee, and his brother John, and they were in the boat refitting the nets,
Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 and immediately He called them, and having left their father Zebedee in the boat with the hired servants, they went away after Him.
Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21 And they go on to Capernaum, and immediately, on the Sabbaths, having gone into the synagogue, He was teaching,
Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22 and they were astonished at His teaching, for He was teaching them as having authority, and not as the scribes.
Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23 And there was in their synagogue a man with an unclean spirit, and he cried out,
Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24 saying, “What [regards] us and You, Jesus the Nazarene? You came to destroy us; I have known You, who You are—the Holy One of God.”
akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
25 And Jesus rebuked him, saying, “Be silenced, and come forth out of him,”
Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
26 and the unclean spirit having convulsed him, and having cried with a great voice, came forth out of him,
Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27 and they were all amazed, so as to reason among themselves, saying, “What is this? What new teaching [is] this? That with authority He also commands the unclean spirits, and they obey Him!”
Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 And the fame of Him went forth immediately to all the region of Galilee.
Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29 And immediately, having come forth out of the synagogue, they went into the house of Simon and Andrew, with James and John,
Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30 and the mother-in-law of Simon was lying fevered, and immediately they tell Him about her,
Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31 and having come near, He raised her up, having laid hold of her hand, and the fever left her immediately, and she was ministering to them.
Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32 And evening having come, when the sun set, they brought to Him all who were ill and who were demoniacs,
Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33 and the whole city was gathered together near the door,
Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34 and He healed many who were ill of manifold diseases, and He cast forth many demons, and was not permitting the demons to speak, because they knew Him.
Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35 And very early, it being yet night, having risen, He went forth, and went away to a desolate place, and was praying there;
Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36 and Simon and those with him went in quest of Him,
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37 and having found Him, they say to Him, “All seek You”;
Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
38 and He says to them, “We may go into the next towns, that there also I may preach, for—for this I came forth.”
Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
39 And He was preaching in their synagogues, in all Galilee, and is casting out the demons,
Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40 and there comes to Him a leper, calling on Him, and kneeling to Him, and saying to Him, “If You may will, You are able to cleanse me.”
Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
41 And Jesus having been moved with compassion, having stretched forth the hand, touched him and says to him, “I will, be cleansed”;
Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
42 and He having spoken, immediately the leprosy went away from him, and he was cleansed.
Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43 And having sternly charged him, immediately He put him forth,
Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44 and says to him, “See [that] you may say nothing to anyone, but go away, show yourself to the priest, and bring near for your cleansing the things Moses directed, for a testimony to them.”
“Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
45 And he, having gone forth, began to proclaim much, and to spread the thing abroad, so that He was no longer able to openly enter into the city, but He was outside in desolate places, and they were coming to Him from every quarter.
Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.