< Mark 9 >

1 And He said to them, “Truly I say to you that there are certain of those standing here, who may not taste of death until they see the Kingdom of God having come in power.”
Yesu akaendelea kuwaambia, “Amin, nawaambia, kuna watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
2 And after six days Jesus takes Peter, and James, and John, and brings them up to a high mountain by themselves, alone, and He was transfigured before them,
Baada ya siku sita, Yesu akawachukua Petro, Yakobo na Yohana, akawapeleka juu ya mlima mrefu, mahali walipokuwa faraghani. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao.
3 and His garments became glittering, exceedingly white, as snow, so as a launderer on the earth is not able to whiten [them].
Mavazi yake yakawa na weupe wa kuzima macho, meupe kuliko ambavyo mtu yeyote duniani angaliweza kuyangʼarisha.
4 And there appeared to them Elijah with Moses, and they were talking with Jesus.
Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza na Yesu.
5 And Peter answering says to Jesus, “Rabbi, it is good to us to be here; and we may make three shelters, for You one, and for Moses one, and for Elijah one”:
Petro akamwambia Yesu, “Rabi, ni vyema sisi tukae hapa. Turuhusu tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.”
6 for he was not knowing what he might say, for they were greatly afraid.
Petro hakujua aseme nini kwa maana yeye na wenzake walikuwa wameogopa sana.
7 And there came a cloud overshadowing them, and there came a voice out of the cloud, saying, “This is My Son, the Beloved, hear Him”;
Ndipo pakatokea wingu, likawafunika, nayo sauti kutoka lile wingu ikasema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Msikieni yeye.”
8 and suddenly, having looked around, they saw no one anymore, but Jesus only with themselves.
Mara walipotazama huku na huku, hawakuona tena mtu mwingine yeyote pamoja nao isipokuwa Yesu.
9 And as they are coming down from the mountain, He charged them that they may declare to no one the things that they saw, except when the Son of Man may rise out of the dead;
Walipokuwa wakishuka kutoka mlimani, Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote mambo waliyoona, mpaka Mwana wa Adamu atakapokuwa amefufuka kutoka kwa wafu.
10 and the thing they kept to themselves, questioning together what the rising out of the dead is.
Wakalihifadhi jambo hilo wao wenyewe, lakini wakawa wanajiuliza, “Huku kufufuka kwa wafu maana yake nini?”
11 And they were questioning Him, saying that the scribes say that Elijah must come first.
Wakamuuliza, “Kwa nini walimu wa sheria husema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?”
12 And He answering said to them, “Elijah indeed, having come first, restores all things; and how has it been written concerning the Son of Man, that He may suffer many things, and be set at nothing?
Yesu akawajibu, “Ni kweli, Eliya yuaja kwanza ili kutengeneza mambo yote. Mbona basi imeandikwa kwamba Mwana wa Adamu ni lazima ateseke sana na kudharauliwa?
13 But I say to you that also Elijah has come, and they did to him what they willed, as it has been written of him.”
Lakini ninawaambia, Eliya amekwisha kuja, nao wakamtendea walivyopenda, kama ilivyoandikwa kumhusu yeye.”
14 And having come to the disciples, He saw a great multitude around them, and scribes questioning with them,
Walipowafikia wale wanafunzi wengine, wakawakuta wamezungukwa na umati mkubwa wa watu na baadhi ya walimu wa sheria wakibishana nao.
15 and immediately, all the multitude having seen Him, were amazed, and running near, were greeting Him.
Mara wale watu walipomwona Yesu, wakastaajabu sana, wakamkimbilia ili kumsalimu.
16 And He questioned the scribes, “What do you dispute with them?”
Akawauliza wanafunzi wake, “Mnabishana nao kuhusu nini?”
17 And one out of the multitude answering said, “Teacher, I brought my son to You, having a mute spirit;
Mtu mmoja miongoni mwa ule umati wa watu akajibu, “Mwalimu, nilimleta kwako mwanangu ambaye ana pepo mchafu anayemfanya asiweze kuongea.
18 and wherever it seizes him, it tears him, and he foams, and gnashes his teeth, and pines away; and I spoke to Your disciples that they may cast it out, and they were not able.”
Kila mara huyo pepo mchafu ampagaapo mwanangu, humwangusha chini na kumfanya atokwe povu mdomoni na kusaga meno, kisha mwili wake hukauka. Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo mchafu, lakini hawakuweza.”
19 And He answering him, said, “O generation unbelieving, until when will I be with you? Until when will I suffer you? Bring him to Me”;
Yesu akawaambia, “Enyi kizazi kisicho na imani! Nitakuwa pamoja nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni mvulana kwangu.”
20 and they brought him to Him, and he having seen Him, immediately the spirit convulsed him, and he, having fallen on the earth, was wallowing—foaming.
Nao wakamleta yule mvulana. Yule pepo mchafu alipomwona Yesu, mara akamtia yule mvulana kifafa, akaanguka, akagaagaa chini huku akitokwa na povu kinywani.
21 And He questioned his father, “How much time is it since this came to him?” And he said, “From childhood,
Yesu akamuuliza baba yake, “Mwanao amekuwa katika hali hii tangu lini?” Akamjibu, “Tangu utoto wake.
22 and many times it also cast him into fire, and into water, that it might destroy him; but if You are able to do anything, help us, having compassion on us.”
Mara kwa mara huyo pepo mchafu amekuwa akimwangusha kwenye moto au kwenye maji ili kumwangamiza. Lakini kama unaweza kufanya jambo lolote, tafadhali tuhurumie utusaidie.”
23 And Jesus said to him, “If you are able to believe! All things are possible to the one that is believing”;
Yesu akamwambia, “Kama ukiweza kuamini, yote yawezekana kwake yeye aaminiye.”
24 and immediately the father of the child, having cried out with tears, said, “I believe, Lord; be helping my unbelief.”
Mara baba yake yule mvulana akapiga kelele akisema, “Ninaamini. Nisaidie kutokuamini kwangu!”
25 Jesus having seen that a multitude runs together, rebuked the unclean spirit, saying to it, “Spirit—mute and deaf—I charge you, come forth out of him, and you may no longer enter into him”;
Yesu alipoona kwamba umati wa watu unakusanyika pamoja mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akimwambia, “Wewe pepo bubu na kiziwi, nakuamuru umtoke, wala usimwingie tena!”
26 and having cried, and convulsed him much, it came forth, and he became as dead, so that many said that he was dead,
Yule pepo mchafu akiisha kupiga kelele, akamtia kifafa kwa nguvu, na akamtoka. Yule mvulana alikuwa kama maiti, hivyo watu wengi wakasema, “Amekufa.”
27 but Jesus, having taken him by the hand, lifted him up, and he arose.
Lakini Yesu akamshika mkono, akamwinua, naye akasimama.
28 And He having come into the house, His disciples were questioning Him by Himself, “Why were we not able to cast it forth?”
Baada ya Yesu kuingia ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza wakiwa peke yao, “Mbona sisi hatukuweza kumtoa huyo pepo mchafu?”
29 And He said to them, “This kind is able to come forth with nothing except with prayer and fasting.”
Yesu akawajibu, “Hali hii haiwezi kutoka isipokuwa kwa kuomba na kufunga.”
30 And having gone forth there, they were passing through Galilee, and He did not wish that any may know,
Wakaondoka huko, wakapitia Galilaya. Yesu hakutaka mtu yeyote afahamu mahali walipo,
31 for He was teaching His disciples, and He said to them, “The Son of Man is being delivered into the hands of men, and they will kill Him, and having been killed, the third day He will rise,”
kwa maana alikuwa anawafundisha wanafunzi wake. Akawaambia, “Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu. Nao watamuua, lakini siku tatu baada ya kuuawa atafufuka.”
32 but they were not understanding the saying, and they were afraid to question Him.
Lakini wao hawakuelewa kile alimaanisha, nao waliogopa kumuuliza maana yake.
33 And He came to Capernaum, and being in the house, He was questioning them, “What were you reasoning in the way among yourselves?”
Basi wakafika Kapernaumu na baada ya kuingia nyumbani akawauliza, “Mlikuwa mnabishana nini kule njiani?”
34 And they were silent, for they reasoned with one another in the way who is greater;
Lakini hawakumjibu, kwa sababu njiani walikuwa wakibishana kuhusu nani miongoni mwao alikuwa mkuu zaidi ya wote.
35 and having sat down He called the Twelve, and He says to them, “If any wills to be first, he will be last of all, and minister of all.”
Akaketi chini, akawaita wote kumi na wawili, akawaambia: “Kama mtu yeyote akitaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa wa mwisho na mtumishi wa wote.”
36 And having taken a child, He set him in the midst of them, and having taken him in His arms, said to them,
Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha katikati yao. Akamkumbatia, akawaambia,
37 “Whoever may receive one of such children in My Name, receives Me, and whoever may receive Me, does not receive Me, but Him who sent Me.”
“Mtu yeyote amkaribishaye mmoja wa hawa watoto wadogo kwa Jina langu, anikaribisha mimi. Naye anikaribishaye mimi, amkaribisha Baba yangu aliyenituma.”
38 And John answered Him, saying, “Teacher, we saw a certain one casting out demons in Your Name, who does not follow us, and we forbade him, because he does not follow us.”
Yohana akamwambia, “Mwalimu, tumemwona mtu akitoa pepo wachafu kwa jina lako, nasi tukamkataza, kwa sababu yeye si mmoja wetu.”
39 And Jesus said, “Do not forbid him, for there is no one who will do a mighty work in My Name, and will be readily able to speak evil of Me:
Yesu akasema, “Msimkataze, kwa kuwa hakuna yeyote atendaye miujiza kwa Jina langu ambaye baada ya kitambo kidogo aweza kunena lolote baya dhidi yangu.
40 for he who is not against us is for us;
Kwa maana yeyote asiye kinyume chetu, yuko upande wetu.
41 for whoever may give you to drink a cup of water in My Name, because you are Christ’s, truly I say to you, he may not lose his reward;
Amin, nawaambia, yeyote awapaye ninyi kikombe cha maji kwa Jina langu kwa sababu ninyi ni mali ya Kristo, hakika hataikosa thawabu yake.”
42 and whoever may cause to stumble one of the little ones believing in Me, better is it for him if a millstone is hanged around his neck, and he has been cast into the sea.
“Kama mtu yeyote akimsababisha mmojawapo wa wadogo hawa wanaoniamini kutenda dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake, na kutoswa baharini.
43 And if your hand may cause you to stumble, cut it off; it is better for you to enter into life maimed, than having the two hands, to go away into Gehenna, into the fire—the unquenchable— (Geenna g1067)
Kama mkono wako ukikusababisha kutenda dhambi, ukate. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili lakini ukaingia jehanamu, mahali ambako moto hauzimiki. [ (Geenna g1067)
44 [[where their worm is not dying, and the fire is not being quenched.]]
Mahali ambako funza wake hawafi wala moto wake hauzimiki.]
45 And if your foot may cause you to stumble, cut it off; it is better for you to enter into life lame, than having the two feet to be cast into Gehenna, into the fire—the unquenchable— (Geenna g1067)
Kama mguu wako ukikusababisha kutenda dhambi, ukate. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili lakini ukaingia jehanamu. [ (Geenna g1067)
46 [[where their worm is not dying, and the fire is not being quenched.]]
Mahali ambako funza wake hawafi wala moto hauzimiki.]
47 And if your eye may cause you to stumble, cast it out; it is better for you to enter into the Kingdom of God one-eyed, than having two eyes, to be cast into the Gehenna of fire— (Geenna g1067)
Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe. Ni afadhali kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa jehanamu, (Geenna g1067)
48 where their worm is not dying, and the fire is not being quenched;
mahali ambako “‘funza wake hawafi, wala moto wake hauzimiki.’
49 for everyone will be salted with fire, and every sacrifice will be salted with salt.
Kila mmoja atatiwa chumvi kwa moto.
50 The salt [is] good, but if the salt may become saltless, in what will you season [it]? Have in yourselves salt, and have peace in one another.”
“Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake utaifanyaje ili iweze kukolea tena? Mwe na chumvi ndani yenu, mkaishi kwa amani, kila mmoja na mwenzake.”

< Mark 9 >